Muigizaji wa Bongo Zuberi Mohammed adai Wema Sepetu, Uwoya na wengine hawafikii uzuri wa mke wake

Mwanaume ni kujiamini na muigizaji wa Bongo Zuberi Mohammed anaejulikana kama Niva amefunguka kwa kusema kuwa mke wake anauzuri ambao Uwoya, Wema na Kajala hawana.

Wema Sepetu

Akiongea katika interview, muigizaji huyu hakuogopa kwa kuwachana warembo hawa ambao wamekuwa kwenye sekta ya burudani kwa muda sasa. Kulingana na yeye, alibarikiwa na mwanamke ambaye anauzuri ambao bado hajauona katika mwanamke mwingine.

“Nakuambia ukweli kabisa hakuna mwanamke mzuri Bongo Muvi zaidi ya mke wangu Maisala, wewe muamshe usingizini Uwoya, Wema, Kajala halafu muamshe na mke wangu uone nani anavutia zaidi, hakuna kama mke wangu,”

Uwoya
Uwoya

Jibu hili lake lilikuwa la kuwapasha watu ambao wamekuwa wanaosema eti anauwezo wa kumsaliti mkewe kwani kila wakati anaonekana akitembea na wasanii wa Bongo Muvi wakati alifunguka ndoa na nia ya kutulia na kuanza familia.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.