Nai Adai Gigy Money ni Mnafiki na Sio Rafiki Mzuri Kwake

Video vixen maarufu Bongo Nai ambaye pia ni mpenzi wa msanii wa Bongo fleva Moni Centrozone ameibuka na kumtolea povu Gigy Money kwa kudai sio rafiki mzuri.

Gigy Money na Nai walionekana kuwa na ukaribu mkubwa siku za hivi karibuni hasa baada ya Gigy Money kuachana na Mo j na Nai kuachana na Moni centrozone.

Lakini ukaribu huo uliingia mdudu baada ya habari kusambaa kuwa Gigy anatoka na Moni na hata alibadilisha jina lake na kujiita Gigy Centrozone Kwenye Instagram.

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, NAi anafunguka na kuweka wazi kuwa ameumizwa na kitendo kilichofanywa na Gigy Money ambaye amekiri kuwa sio rafiki mzuri kwake:

Gigy sio rafiki mzuri kwangu kwa sababu ni mtu ambaye anajaribu kuniongelea vibaya hata kwa Moni ambaye alimposti na kujibadilisha jina na pia kajaribu kumpelekea vitu vya uongo vingi ambavyo vimetufanya mimi na Moni mpaka sasa hatupo sawa.

Na pia naweza kudiriki kusema kuwa Gigy sio rafiki wa kweli kwangu hivyo nimemuweka pembeni nina maisha yangu mwenyewe sihitaji watu wanafiki”.

Nai amekiri kuwa Gigy Money alimtafuta ili wayamalize lakini amesema hataki Tena urafiki naye kwani ameharibu uhusiano wake na mpenzi wake Moni.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.