Nandy na Diamond Platnumz Wang’ara Tuzo za AEAUSA

Wasanii wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz kutoka WCB na Faustina  Charles maarufu kama Nandy na wasanii wengine kutoka Tanzania wameng’ara katika tuzo za African Entertainment Awards USA (AEAUSA).

Mbali na wasanii hao wa Kitanzania kushinda tuzo lakini pia kuna wasanii kutoka katika nchi za Afrika Mashariki waliofanikiwa kushinda tuzo.

Wasanii waliofanikiwa kushinda tuzo ni pamoja na Diamond Platnumz ambaye ameshinda tuzo mbili, ikiwemo tuzo ya Msanii bora wa mwaka ( Best artist of the year pamoja na Best Collaboration akishirikiana na Omarion kutoka nchini Marekani.

Msanii Nandy ameshinda katika kipengele cha Best Female Single kupitia wimbo wa Kivuruge, huku Rayvanny akishinda tuzo ya Best Vocalist na Dj wa Diamond Rom Jones akishinda tuzo ya best DJ in Africa.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.