“Natamani BASATA Waniruhusu Kuperfom Mwanza”- Rayvanny

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB Rayvanny ameibuka na kuwaomba tena BASATA wampe ruhusa ya kuperfom wimbo wa Mwanza stejini.

Wiki chache ziliopita Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) liliufungia rasmi wimbo wa ‘Mwanza’ wa Rayvanny aliomshirikisha Diamond Platnumz kwa madai ya kukiuka maadili ya Kitanzania kwa kuimba matusi.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Rayvanny alisema angetamani sana kwa mara ya kwanza apafomu Wimbo wa Mwanza katika jukwaa la Wasafi Festival lakini anashindwa kutokana na adhabu ya Basata ya kuufungia wimbo huo ambao yeye anakiri kuwa hakuutunga kwa nia ya kupotosha watu bali kuburudisha.

Kiukweli natamani sana wangeniruhusu tu japo nipafomu katika shoo zangu maana mapokezi ya huu wimbo ni makubwa mno mpaka yananifanya nitamani kuupafomu katika jukwaa la Wasafi Festival Jumamosi hii”.

WCB wanategemea kupigwa bonge la shoo kwenye tamasha Lao la Wasafi Festival linalotarajiwa kufunguliwa rasmi Jumamosi hii tarehe 24 mkoani Mtwara.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.