Nay Wa Mitego- Bado Ninampenda Nini

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya muziki wa kuchana Emanuel Elbariki maarufu kama Nay wa Mitego ameibuka na kudai bado anampenda aliyekuwa mpenzi wake Msanii mwenzake Nini.

Nay wa Mitego walitangaza kuachana wiki chache zilizopita ambapo Nay alikiri kuwa sababu kubwa ya kumwagana ni baada ya Nini kumkamata akiwa na mwanamke mwingine.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Nay amefunguka na kudai moyoni bado anampenda Nini na endapo atapata nafasi nyingine basi atampokea kwa mikono miwili.

Bado ninampenda sana Nini na hata kama akirudi leo hii akahitaji kurudiana na mimi, nitakuwa tayari kumpokea”.

Nini na Nay walificha mapenzi yao kipindi chote walipokuwa wote kutokana na kwamba Nini alikuwa amesainiwa chini ya Label ya Nay Free Nation ambapo Mpaka sasa pamoja na kwamba hawapo wote lakini Nini bado anafanya kazi chini ya Label hiyo.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.