Nay Wa Mitego- Nagombea Uraisi Mwaka 2020

Mwanamuziki wa Bongo fleva amefunguka na kusema sababu pekee inayomfanya awe kimya kwa hivi sasa ni mipango yake ya kugombea uraisi mwaka 2020.

Nay wa Mitego ni msanii ambaye anajulikana kwa vituko Chake ikiwemo Uwezo wake wa kuwachana watu kwenye jamiii hasa wasanii wenzake kuhusu mambo mbali mbali.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Risasi Vibes, Nay alisema kwa sasa ameamua kujitenga na skendo kwani anajiandaa kugombea urais mwaka 2020 japokuwa hawezi kuweka wazi atagombea kwa chama gani hivyo akaona ni vema aachane na skendo zisizokuwa na maana.

Nimeamua kutulia na kuachana na skendo zisizokuwa na maana kwa sababu nina mpango wa kugombea urais mwaka 2020 sasa nikiwa na skendo chafu zitaniharibia“.

Hivi sasa kumekuwa na trend kubwa ya wasanii mbali mbali kujiingiza Kwenye mambo ya siasa na kugombea nafasi mbali mbali kama vile Wasanii wakongwe wa Bongo fleva Profesa Jay na Sugu ambao wote ni wabunge.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.