Ndoa Haijazima Muziki Wangu- Shilole

Mwanamuziki wa Bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kuweka wazi kuwa ndoa yake haijaweza kuzima  hata kidogo muziki wake.

Shilole alifunga ndoa ya siri na mume wake Asharaf Uchebe mwaka jana mwishoni lakini tangu hapo hajasikika Tena akiwa na Wimbo Mpya ambapo imedaiwa ndoa imembana kufanya Muziki Tena.

Kwenye mahojiano aliyofanya na vyombo vya habari Kwenye shoo ya Davido mwishoni mwa wiki iliyopita, Shilole amesema amebanwa tu na biashara  nyingine nje ya muziki lakini sio ndoa yake:

Sio kweli, mimi ningekuwa nimepungua kwenye game usingenifanyia interview sasa hivi. Sio kweli nina kazi nyingi za kuniingizia fedha kuliko muziki”.

Wimbo wa mwisho wa Shilole kutoa unaitwa Kigori ambao ulitoka August 07, 2017 ambao ulikuwa ni Miezi kadhaa kabla ya ndoa yake.

Shilole ameweka wazi kinachombana ni biashara zakke nyingine ambazo ni mgahawa wake wa Shishi Food na pia anamiliki chili yake na hivi karibuni anakuja na kitabu chake.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.