Ney Wa Mitego Ahofia Kuongelea Hali ya Usalama Nchini

Msanii wa Bongo fleva nchini Ney wa Mitego anayejulikana kwa uwezo wake wa kupaza sauti na kuongea ukweli kuhusiana na mambo mbalimbali  katika jamii kwa mara ya kwanza amefunguka na kuhusu hali ya usalama ilivyo hapa nchini kufuatia mauaji ya na shambulio la risasi la Tundu Lissu ambalo limetikisa nchi nzima.

Ney amesema ingawa wasanii ndio watu wakipaza sauti zinaeleweka kwa wingi hata kwa wasiofatilia siasa, lakini ameona bora ayaache mambo hayo kwa  wenyewe wanasiasa kutokana na uoga aliokuwa nao.

Ney ameendelea kufunguka kuwa anatamani kuongea lakini kutokana na hali ilivyo kwa sasa anahofia usalama wake na familia yake kwani hata familia yake humkalisha chini na kumuonya na yeye kuamua kukaa kimya, na kuwaachia wanasiasa waendelee kupambana wenyewe.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.