Niligombana na Mwanangu Kisa Mambo Ya Usanii- Mzee Gerald

Baba mzazi wa marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’ Anayeitwa Mzee Gerald amefunguka na kueleza kuwa alikuwa akigombana sana na mwanaye ambaye alikuwa anamsihi aachane na mambo ya sanaa.

Agnes alijizolea umaarufu miaka ya nyuma kwa mara ya kwanza baada ya kutokea kwenye video ya wimbo wa Msanii wa Bongo fleva Belle 9 Masogange ambao ulipelekea mpaka yeye kuitwa Agnes Masogange Lakini pia marehemu alikuwa ameanza kuwa muigizaji wa Bongo movie.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers kwa mara ya kwanza tangu amzike mwanaye hapo jana, Mzee Gerald amefunguka haya kuhusu binti yake:

Mwanangu alikomea kidato cha pili lakini hata kidato  cha pili hakumaliza kwa sababu ya matatizo. Kuna wakati nilikorofishana naye nikamwambia mimi mambo ya usanii sitaki, akanijibu, ‘sasa baba mimi nitafanya kazi gani wakati unafahamu tangu niko kanisani nilikuwa naimba kwaya?’ Baada ya muda tulikutana tena, tukalimaliza suala hilo, nikamruhusu“.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.