Nilishapata Proposal za Kwenda kwa Waganga Nyingi :-Kareen

Mwanadada Kareen lil ambae sasa hivi anatamba na wimbo wa lawana kutoka THT amefunguka na kusema kuwa amekuwa akipokea proposal nyingi kutoka kwa watu wakimwambia kuwa ili muziki wake ufanye vizuri basi aende kwa waganga wa kienyeji kuloga ili kuwa na nyota.

Kareen anasema kuwa hata hivyo hawezi kufanya kitu kama hicho kwa sababu familia yake haijamkuza katika malezi hayo ukizingatia kwao wanamfuata sana Mungu na wanasali sana hivyo sala za babu na bibi zake kwake ni baraka tosha.

Akiongezea kuhusu mziki wake Kareen anasema kuwa amekuwa akivutiwa sana na mwana dada vannesa kutokana na kuwa mni mwanamkziki wa kike anaefanya kazi na kufika mbali kwa nguvu zake mwenyewe .

Kareen ambae ni mtoto wa mtangazaji maarufu wa radio Gadner G Habash anasema kuwa kwa kiasi flani pia jinala baba yake limekuwa likisaidia ku-push mziki wake na amekuwa akipata shavu lakini pia muziki wake mzuri umemfikisha alipo.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.