Nini Akiri Kuvunjika Kwa Penzi Lake na Nay Wa Mitego Kisa Michepuko

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nini amefunguka na kuweka wazi kuwa penzi lake na msanii mwenzake Nay wa Mitego limefikia ukingoni hivi karibu.

Nay wa Mitego na Nini walidaiwa kuwa Kwenye Mahusiano kwa muda mrefu lakini walikuwa wanakataa kila wakiukizwa walidai kuwa ni marafiki tu lakini wamethibitisha walikuwa wapenzi baada ya kuachana.

Nini ameibuka na kukataa tetesi zinazoendelea kusambaa kuwa kisa chao wao kuachana ni baada ya familia yake kumlazimisha Nay amuoe baada ya kumchukua mtoto wao na kuishi naye bila kujitambulisha wala kumuoa.

Kwenye mahojiano na Clouds Tv,Nini amesema ameamua kuachana na Nay wa Mitego kutokana na kumchukulia poa na kuwa na mahusiano na wanawake wengine.

Ni kweli nimeachana na Nay na niweke hili sawa sijawahi kuishi nyumba moja na Nay na hata hiyo ishu ya wazazi wangu kwenda kwa Nay sio kweli.

Unajua kwenye mahusiano kuna mambo mengi sana na mtu kama mwanaume unaweza ukampenda, ukamuheshimu akawa anakuchukulia poa, anakufanyia drama anakuletea wanawake“.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.