Penny Ategemea Ndoa Mwaka Huu

Mtangazaji maarufu wa luninga  ya afrika magic swahili katika kipindi cha n harusi yetu amewapa moyo mashabiki wake na kuwaambia kuwa mwaka uliopita haukuwa mwaka mzuri sana kwake hasa katika swala la ndoa na mahusiano lakini sasa hivi wakae mkao wa kula kwa sababu  bwana yuko tayari kwa ajili ya harusi,

Penny anasema kuwa mwaka 2017 ulikuwa ni mwaka wenye gundu kwake lakini anashukuru Mungu mwaka huo umepita na  kwa mwaka huu anategemea kila kitu kitakuwa sawa na bwana harusi yuko tayari kwaiyo wategemee ndoa.

mwaka huu ni mwaka wa baraka kwangu  na gundu nyingi zilizokuwepo zilishaondoka  2017,mwaka huu kwangu ni ishara na shela litakaa mwilini mwangu, bwana harusi yupo tayari kwa mwaka huu.

Hata hivyo Penny hakutaka kumsema mwanaume ambae yupo nae katika mahusiano ingawa amewathibitishia mashabiki kuwa ndo mwaka huu ni lazima.

Penny alishawahi kuwa katika mahusiano na msanii mkubwaTtanzania Diamond Platinumz na kupata mimba yake lakini aliitoa mimba hiyo na kusababisha mahusino yao kuvunjika.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.