Petit Man Ayatetea Mapishi Ya Mke Wake Esma

Hamad Manungwa maarufu kama Petit Man ameibuka na kumkingia kifua mke wake Asmah Khan ‘Esma Platnumz’ baada ya kutuhumiwa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa hajui kupika.

Siku chache zilizopita Esma aliposti picha ya chakula alichomuandalia mume wake kama futari lakini mambo yaligeuka kwani mashabiki walimjia juu na kumsema hajui kupika.

Lakini Petit ameibuka na kusema wote wanaotokwa na maneno kuwa mke wake hajui kupika hawajui wanachokiongea kwani yeye ndio anajua anapikiwa nini kila siku.

Petit alifunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers ambapo alizidi kufunguka:

Unajua mimi sibishani hata siku moja na watu wa mitandaoni kwa sababu najua wazi sio mke wangu aliyepika ile futari. Akipika yeye chakula kinakuwa cha uhakika, nikila nasikia raha hadi najivunia kumuoa, hao wanaosema Esma hajui kupika, wana lao jambo”.

Baada ya Tuhuma hizo kuzidi Esma aliposti chakula kingine huku akisisitiza kuwa chakula watu walichokiona hakupika yeye.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.