Ray C atoa sababu ya yeye kuwa single

Ray C hana haraka na mapenzi, muimbaji huyo amedhibitisha haya hivi karibuni ambapo pia alitoa sababu zake za kutaka kuwa single bado.

Akiongea kwenye kipindi cha FNL ya EATV, Ray C alisema hana muda na mwanaume yeyote kwani malengo yake ni kuvuma tena kwa kutoa ngoma kalikali.

Ray C alieleza kuwa alipoteza muda mingi kwa kujihusisha na mahusiano ambayo haikumpeleka kokote, alisema akili yake sasa iko kwa kazi tu.

“Mimi hapana sipo kwenye mahusiano na mtu yeyote, kwa muda niliopoteza, hakuna tena muda wa kupoteza wa kumpa tena mtu mwingine naona kama muda umenipita sana, kwa hiyo akili yangu ipo kwenye kazi. Sioni kama ninaweza nikashare muda wangu na mtu mwingine, sina hata hizo feeling kwa bahati mbaya sana,” amesema Ray C.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.