Rayvanny Ataja Kilichomsibu Mpaka Kupaka Rangi Nywele

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika Music Label ya WCB, Raymond Mwakyusa maarufu kama Rayvanny amefunguka na kumtaka kilichomsibu Mpaka kubadilisha muonekano Wake.

Hivi karibuni Rayvanny ameonekana na muonekano Mpya kichwani kwani Mbali tu ya kusuka Rasta Lakini pia amezipaka rangi ya Bleach na kuonekana tofauti.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, Rayvanny amesema kuwa kwa kawaida msanii anatakiwa kuwa na muonekano wa tofati tofauti na ndicho alichokifanya kwa sasa.

Muda mwingine msanii unatakiwa uwe unabadilika sio panki kila siku. Mtaanza matusi yenu toa, toa, sitoi huo ndio muonekano wangu”.

Msanii huyo anayefanya vyema na kibao chake cha Paraanawe amepokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki zake ambao hapo Mwanzoni walikuwa wanavutiwa kwa kuwa na nywele fupi za kawaida tofauti na Diamond na Harmonize ambao walikuwa wanasuka na kubleach nywele.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.