Rosa Ree Afunguka Kuhusu Kujiunga WCB

Msanii wa Bongo fleva Rosary Robert ‘Rosa Ree’ aliyejizolea umaarufu kutokana na  miondoko yake ya kuchana amefunguka juu ya mipango ya kusaini na Label maarufu nchini WCB.

Rosa Ree ambaye amekuwa akiulizwa mara kwa mara kama ana mpango wa kujiunga na label hiyo ameweka wazi kuwa hajwahi kufikiria kujiunga WCB.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Rosa Ree ambaye awali kabisa alikuwa katika label ya The Industry amesema  kuwa hawajawahi kuzungumza hilo ila ni watu ambao wamekuwa bega kwa bega na yeye katika muziki wake.

Hapana ilikuwa hamna, ndiyo timu mzima ya WCB wamekuwa wakinisapoti katika muziki wangu. Nafurahia hilo ila hatukuwahi kufikia hatua hiyo”.

Rosa Ree aliondoka The Industry, record label inayomilikiwa na Nahreel na Aikah wa Navy Kenzo mwaka jana oktoba na amekaa bila management kwa miezi kadhaa mpaka aliposainiwa mapema mwezi huu.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.