Rose Muhando Hoi ICU-Kenya

Hali ya mwanamuziki wa injili Rose Muhando inasemekana kuwa mbaya huku ikisemwa kuwa hali yake wa sasa imekuwa ikiangaliwa na baadhi ya waimbaji wenzake ambao wamekuwa wakifanya siri juu ya afya ya mwanadada huyo.

Habari zinasema kuwa mwanadada huyo amekuwa akisumbuliwa na mkono ambao hapo awali katika baadhi ya picha na video zilizokuwa zikimuonyesha akiombewa kanisani zilimuonyesha kama mtu alievunjika mkono.

Hata hivyo inasemwa kuwa hata wenyeji wake ambao ni waimbaji wenzake wamekuwa wakifanya siri sana kuhusu kutoa taarifa ya kinachomsumbua ilhali mtu huyo yu mautiuti kitandani.

Hata baada ya gazeti la Risasi kupata habari hizo walianza kufatlia ukweli kwa kumuuliza kiongozi wa chama cha wanamuziki wa injili Tanzania, Bi Stella Joel na alisema kuwa hata wao wamesikia tu taarifa hizo lakini hakuna uhakika wowote na wanafatilia kwa karibu na watatoa taarifa.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.