Shilole: Mimi namkubali zaidi Diamond Platnumz kuliko Ali Kiba

Shilole ameeleza sababu ya kumkubali Diamond Platnumz kuliko Ali Kiba – wawili hao (Ali Kiba na Diamond) ni maadui wakubwa kimuziki.

Nani kati Diamond na Ali Kiba ndo mfalme wa muziki Tanzania? Mjadala huu huzua utata kila mara unapoulizwa. Mashabiki wa Diamond watasema Simba ndo anaweza na wale wa Ali Kiba watasema yeye ndo bingwa.

Zuwena Muhamed alimaarufu kama Shilole amesema yeye ni Team Diamond Platnumz. Akiongea kwenye kipindi cha Kikaangoni live kinachofanyika kupitia ukurasa wa facebook wa EATV, Shilole alisema yeye anamkubali sana Diamond.

“Mimi namkubali zaidi Diamond Platnumz kuliko Alikiba, nampenda Diamond kutoka na mambo yake na vile alivyo, kwa hiyo kila mtu ana watu anaowakubali na kuwapenda” alisema Shilole.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.