“Siwezi Kuingilia Mahusiano Ya Diamond”-Mbosso

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka katika label ya WCB, Maromboso almaarufu kama Mbosso ameweka wazi kuwa hawezi kuingilia Mahusiano ya Bosi wake Diamond Platnumz.

Diamond ambaye ni Mkurugenzi wa label ya WCB amekuwa kivutio sana Kwenye mitandao ya kijamii hasa linapokuja suala la Mahusiano Yake binafsi na Familia yake.

Mbosso ambaye alijiunga Rasmi WCB Miezi michache iliyopita amefunguka na kusema hawezi hata siku moja kuingilia Mahusiano binafsi ya Diamond.

Suala hilo liliibuka Kwenye mahojiano aliyokuwa anafanya na Sam Misago Tv, ambapo aliulizwa kama anaweza kumpa ushauri gani Diamond hasa linapokuja suala lake la Mahusiano.

Mahusiano Yake bwana Chibu daaah siwezi kumuingilia huko! Naomba niishie hapa siwezi kuingilia mahusiano yake, Unajua ndio displini niliyojiwekea kuna vitu naweza kuviingilia na kuna vitu siwezi kabisaa”.

Mapema mwaka huu mpiga picha maarufu wa Diamond anayejulikana kama Kifesi alifukuzwa kazi baada ya kuingilia Mahusiano ya Diamond baada ya kumshauri arudiane na Zari badala ya Hamisa.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.