Snura akana kupangiwa nyumba na mwanaume wa Kiarabu

Inasemekana kuwa mwanamziki Snura amepangiwa nyumba mpya na mwanaume wa Kiarabua ambaye anaweza kuwa mpenzi wake hivi sasa.

Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa Global Publishers amabao walimtembelea katika nyumba yake huko maeneo ya Tabata, Dar Snura alikana kwa kusema kuwa hana mawanume wa kiarabu ambaye amempangia nyumba.

Aliendelea kusema kuwa alihamia sehemu hiyo ili mwanae awache kuchoka akienda shule. Hivi ndivyo mazungumzo yao yalikuwa.

Snura
Snura

Wikienda: Snura mambo vipi? Mbona kimya sana kimuziki? Au ndiyo mambo ya ubuyu unaosemwa?

Snura: Yapi tena? Mimi mbona nipo najiandaa kutoa kazi? Siyo kila siku kusikika bila mpango. Mimi huwa nasikika kwa kazi ninayoitoa ninyi subirini mtanisikia.

Wikienda: Hata hivyo, tuna ubuyu hapa kuwa nyumba hii umepangishiwa na mwanaume wa Kiarabu ambaye amekuhamisha Mwananyamala kwa sababu alikuwa hapapendi, unalizungumziaje hilo?

Snura: Hahahahaha, mmenichekesha kweli, watu wanajua kuongea sana, mimi nimehama nyumba kwa sababu ya mtoto. Shule anayosoma mwanangu ipo huku Tabata. Mwananyamala ilikuwa ni mbali sana. Mwanangu alikuwa anachoka sana. Hayo mengine ya mwanaume wa Kiarabu ndiyo kwanza nayasikia kwenu.

Wikienda: Nasikia amekununulia na gari la kutembelea maana tunaliona hapa, tunasikia ana mpango wa kukupiga stop kuimba, je, ni kweli?

Snura: Gari nimenunua mwenyewe kwa jasho langu nikimaanisha kazi yangu, huyo Mwarabu mnayemkazania kama yupo hakuna la kufi cha kwani mwisho wa yote atajulikana tu na ataonekana, lakini nahisi labda wanayemzungumzia ni baba mtoto wangu, hahaha…

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.