Show kubwa ya Rayvanny na Akothee yaandaliwa Ujerumani

Ndoa baina ya wasanii kutoka Kenya na Tanzania yazidi kukita mizizi. Ushirikiano kati ya wasanii wa Kenya na haswa wasanii wa Wasafi unazidi kuongezeka kila uchao.

Hivi juzi Rayvanny alifanya collabo na msanii wa nyimbo za Injili kutoka Kenya anayeitwa Bahati. Msanii Willy Paul pia alitia sahihi na Wasafi kuuza wimbo wake kwenye tovuti la Wafasi.com.

Sasa Rayvanny na Akothee watatumbuiza mashabiki katika jiji la Frankfurt nchini Ujerumani. Wawili hao wataperform katika Black Light Centre Costpark Aprili 15.

Akothee ashawahi kufanya collabo na Diamond, wawili hao walitoa wimbo unaoitwa ‘Sweet Love’ Januari mwaka uliyopita.

Reality TV star wa Kenya Mishi Dorah adai kuwa Rayvanny alitaka kumpa mimba

Kilichotokea kati ya Mishi Dorah na Rayvanny hakiwezi julikana kwa kiukweli kwani wawili hao walikutana wakati ambapo hakuna yeyote alijua kuwa wana ‘mahusiano.’

Mishi Dorah

Hata hivyo, Rayvanny amekuwa akimkana mwanamke huyu kwa kusema kuwa anataka kumuharibia nyumba na jina lake. Lakini baada ya Ghafla kumhoji mwigizaji huyo wa Nairobi Diaries, Mishi Dorah alisema kuwa ni kweli aliweza kupatana na Rayvanny kimapenzi.

Mishi Dorah aliendelea kwa kusema kuwa hajapata hedhi zake kwa mwezi mmoja kuonyesha kuwa kunauwezekano wa mwanamke huyu kuwa na mimba ya Rayvanny kutokana na alivyosema. Kulingana na Mishi, Rayvanny alikuwa anataka sana wawili hao wapate mtoto wao wa kwanza kitu ambacho alihisi hawezi kuharikisha kwani hakutaka kuiharibu figure yake.

Lakini swali bado ni…Kati ya mwanamke huyu na Rayvanny nani anasema ukweli? Ebu itazame interview yake hapa.

https://youtu.be/wN6ppPh-TEI

Rayvanny afunguka kuhusu namna alivyoweza kushirikiana kimuziki na Bahati – muimbaji wa Gospel kutoka nchini Kenya

Watu wengi walishangaa baada ya Rayvanny and Bahati kutangaza kuwa wameshirikiana kimuziki, wawili hao walitoa wimbo unaoitwa ‘Nikumbushe’.

Rayvanny sasa ameeliza namna alivyoweza kushirikiana kimuziki na muimbaji huyo wa nyimbo za injili kutoka Kenya.

“Kwanza mimi nimekuwa nikimfuatilia Bahati kwa muda mrefu na nilikuwa nikifikiria nikikutana naye nitaimba wimbo wa aina gani na mimi niliwa narap huko nyuma lakini nimejua kuimba kwa kupitia kanisani. Kwa hiyo haikuwa ngumu kwangu kufanya kwa sababu ni wimbo wakijamii zaidi ndio maana wimbo hauonyeshi kama ni wa Injili au wakidunia,” Rayvanny alisema akiongea katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM.

Tazama ‘Nikumbushe’ kwenye video hapo chini:

“Naona amepanga kunichafua” Rayvanny amkana Mishi Dorah anayemdai kimapenzi

Rayvanny aliyekuwa nchini Kenya hivi majuzi amekana Mishi Dorah amabaye ni mwanake wa makamo na bado anamtaka Vanyny boy kimapenzi.

Staa huyu wa tanzanian amefunguka kwa kusema kuwa amekataa ofa za Mishi Dorah ambaye anaonekana kumharibia jina nchini Kenya na sasa pia Tanzania. Mishi ambaye ni mwigizaji wa reality show amekuwa akitangaza kuwa ashawai kuwa na Rayvanny kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii, wiki iliyopita. Aliskika akisema,

“Ninampenda Rayvanny, nitamtafuta kwa udi na uvumba nimtunuku penzi ili roho yangu itulie, nampenda sana kwa kweli,”

Mishi Dorah

Ata hivyo Rayvanny sasa amefenguka huku akisema kuwa amekuwa akiona anachosema Mishi Dorah, lakini hatakai mambo ya mwanamke huyu kwani anahofia nyumba yake kuvunjika na pia brand yake kuharibika. Akizungumza Rayvanny alisema,

“Yaani sitaki kumuongelea kabisa huyo mwanamke, maana naona amepanga kunichafua kwani nilienda Kenya wakati f’lani nikakuta habari zake, huku nyumbani Bongo ndiyo hivi tena, sina cha kuongea maana mtu akiamua kukuchafua huwezi kuongea kitu.”

Mpenzi wa Rayvanny aonyesha tumbo lake likiwa uchi wiki kidhaa kabla ya kuzaa

Rayvanny na mpenzi wake fahyma wanamtarajia mtoto wao wa kwanza hivi karibuni kulingana na wanachoandika mitandaoni yao ya kijamii.

wawili hawa wanasemekana kuwa walianza mahusiano yao mwaka uliopita na kwa hivi sasa wanatajia familia yao kuongeza kwa sababu Fahyma ana mimba na kulingana na picha anazoziposti kwenye Instagram msichana huyu amebakisha wiki kadhaa kabla kuzaa mtoto wake wa kwanza.

Ingawa wawili hawa hujaribu kuweka mahusiano yao chini ya maji, Fahyma na rafiki wake wa Karibu ambaye alisemekana kuwa mpenzi wa Diamond Platnumz, Official Lynn, wameweza kushare picha mpya za Fahyma akioneshana tumbo lake huku kama amevaa overall ya kinyasa na crop top.

Mashabiki wa Fahyma walimsifu huku wakimpongeza kwa mtoto anayemtarajia hivi karibuni. Ikiwa bado hujaziona picha hizi basi ziangalie hapa chini.

Fahyma
Fahyma
Fahyma na rafiki yake official Lyyn
Fahyma na rafiki yake official Lyyn