Wanaume Watano Wamejitokeza Wanataka Kunioa- Wema

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali mwanadada Wema Sepetu amefunguka na kueleza jinsi wanaume wanavyomiminika kwao kutaka kutoa posa ili wamuoe.

Wema amefunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda ambapo amedai kuwa kuna muda wanaume watano tofauti walienda kutoa posa kwao lakini aliwakataa wote:

Walijitokeza karibu wanaume watano wanaenda, kwa mama kupeleka barua kinachotokea mama ananiita, ananiuliza mimi, sikubali kwa sababu siwezi kuolewa na mtu ambaye simjui au sijakaa naye“.

Lakini kuhusu Kuolewa hivi sasa Wema amejibu hawezi kuweka wazi lakini ana mpenzi wake ambaye anampenda lakini hawezi kumuweka wazi kwani amekuwa mtu mzima siku hizi.

Wema amefunguka na kumpongeza msanii wa Bongo fleva ambaye pia ni rafiki yake wa karibu Ali Kiba kwa kufunga ndoa hivi karibuni ambapo amesema:

Ninampongeza sana kwa mwanamuziki mkubwa kama yeye kufanya jambo hilo amejijengea heshima kubwa sana, lakini ninaamini mke yupo popote ni jinsi tu Mungu alivyokupangia wapi utampata“.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.