Wastara Ametaja Sababu Zilizomfanya Kuolewa na Kuachika Ndoa Tatu

Muigizaji wa Bongo movie Wastara Juma au maarufu kama Wastara Sajuki amefunguka na kuweka wazi sababu zilizomfanya mpaka hivi sasa awe ameolewa na kuachika katika ndoa tatu tofauti.

Wastara alifunguka hayo alipokuwa mgeni maaalumu katika Tamasha la Single mothers ambalo ni tamasha lililowakutanisha wamama wote wanaolea watoto wao wenyewe bila msaada wa Baba wa watoto kwa lugha nyingine ni Single mothers.

Wastara  alisema kuwa, siri kubwa ya ndoa zake kuvunjika ni kutokana na kukosekana kwa maelewano ndani ya nyumba na siyo kwamba huwa anapenda kuachika.

Unajua kuna vitu ambavyo ningevikubali kuvifanya nilipokuwa ndani ya ndoa, ungekuta sasa hivi nimeshakufa hivyo kuolewa na kuachika siyo kupenda, bali nilishindwa kukubaliana na mambo ambayo nilikuwa ninalazimishwa kuyafanya”.

Tamasha hilo la Single mothers lilifanyika katika hoteli ya De Mag Mwananyamala na liliandaliwa na msanii wa Bongo movie Faiza Ally kwa ajili ya kuwakutanisha wamama wote ambao ni Single mothers ili kuzungumzia mambo mbali mbali na kupeana ushauri.

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.