Wema Sepetu: “Sijakatwa Utumbo, Nimekonda Kwa Mawazo”.

Msanii wa Bongo movie Wema Sepetu ameibuka na kuweka wazi kuwa yeye hajakonda Kwajili ya kukatwa utumbo kama inavyodaiwa bali amekonda kwa ajili ya mawazo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Wema kwa mara ya kwanza aliweka ‘plain’ kuwa kipindi alichopitia kwenye lile sakata la kuvuja kwa picha zake za chumbani na Patric Christopher ‘PCK’ kilikuwa kigumu mno kwani alikuwa anapitisha hata siku tatu bila kula chochote mpaka anapepesuka.

Watu nawashangaa sana, wanaona kukatwa utumbo ni kitu rahisi ee? Mimi nimekon­da kwa sababu ya mawazo makali niliyokuwa nayo na si vitu vingine maana nilikuwa kwenye wakati mgumu sana”.

Lakini pia Wema ameongeza kwa kusema kwamba, licha ya kupungua anaufurahia muonekano wake mpya kwani kuwa mnene zaidi nayo siyo poa.

Yaani hujui tu ninavyoufura­hia huu mwili wangu wa sasa, nimekuwa sio mzito tena na navaa nguo ambazo nataka na napendeza zaidi tofauti na ilivyokuwa huko nyuma, kwa kifupi najipenda hivi nilivyo“.

 

About this writer:


Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.