Msanii Coyo Apewa Kichapo na Mashabiki Kwenye Shoo Tarime

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na kibao chake cha Nyakanyaka, Coyo amedaiwa kutembezewa kipigo kizito na mashabiki zake kwenye shoo aliyofanya Tarime.

Shilawadu wanaripoti kuwa mwishoni mwa wiki iliyopita Coyo alikuwa anafanya shoo mbili moja Ikiwa ni Kenya na nyingine upande wa Tanzania kwa kuwa pale ni mpakani.

Lakini inasemekana alivyomaliza shoo ya Kenya alikuwa ana mpango wa kuwahi Tarime na kwenda kumaliza shoo ya Tanzania lakini usiku mnene ulikuwa umeshaingia hivyo alichelewa kufika na kukuta mashabiki wamevimba.

Unaambiwa alivyofika mashabiki hawakutaka maneno walianza kumtukana matusi mazito na ile anatoka nje wakamdaka wakampa kipigo kitakatifu mpaka Promota alipoenda kumuokoa.

Kwenye mahojiano na Soudy Brown, Coyo alikataa taarifa hizo na kudai kuwa hakuenda Kenya kufanya shoo bali alienda kusalimia marafiki lakini aliporudi kufanya shoo alitaka kufanyiwa utapeli na promota wa shoo yake.

Coyo Anaonyesha Hisia Zake Kwa Vannesa,Atamani Mkewe Awe Kama Yeye

Msanii wa muziki wa bongo fleva  Coyo ,ambae sasa hivi anatamba na kibao chake cha Nyakanyaka  amefunguka wazi na kuonyesha hisia zake kwa mwanamuziki wa kike vannesa mdee na kutamani kuwa mwanamke aliye nae awe kama Vannesa kutokana na sifa nzuri alizonazo msanii huyo hasa kujituma katika kazi na kutambua ni nini anafanya.

Coyo ameongea hayo alipokuwa katika mahojiano na kipindi cha the playlist na kusema kuwa katika wasanii wa kike wanaofanya vizuri na kuijituma basi vannesa mdee ni namba moja na hawezi kufananishwa na msanii mwingine , lakini pia Coyo anasema kuwa Vannesa ni msanii anayefanya kazi kwa kujua ni nini anafanya na amekuwa mwanamke hasiye kuwa na skendo sio kama kina Gigy Money.

Vee anaonekana ni mtu mwenye future ambaye ana mipango , kiufupi ni mwanamke ambaye anajituma kuanzia kwenye  kazi zake na anajua ni kitu gani anafanya, kwaiyo huwa namkubali sana natamani hata wangu angekuwa  kama yeye lakini asiye na skendo kama za Gigy Money .

Hata hivyo Coyo alionekana kutokuwa na wasiwasi wa kumuongelea Gigy Money kwa kumchana na tabia hiyo ya kuwa na skendo na kuongezea kuwa

kitu kizuri kama kiki chenyewe siyo utafute kiki,kuna kitu kimekiki,kuna kitu kimetafuta kiki  na kuna kitu kinatafutiwa kiki , hivyo ni vitu vitatu tofauti.-Aliongezea Coyo akimaaanisha kuwa Gigy Money ni mwanamke anafanya skendo hili kutafuta kiki.

Vannesa Mdee ni moja ya wasanii wa kike kwa sasa ambao wamekuwa wakifanya vizuri na inawezekana akawa ndio msanii wa kike ambae anaongoza kwa kufanya nyimbo nyingi na wasanii wa nje kwa miaka hii miwili ya hivi karibuni, ukiachana na kufanya vizuri na kupendwa bongo lakini pia Vannesa amejitahidi hata kufungua soko lake la muziki hata kwa nchi za nje na amepokelewa vizuri.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.