Msamii na mtengenezai wa muziki kutoka Sharobaro rekodi amefunguka na kusema kuwa amekuwa akifurahia amfanikio makubwa aliyoyapata msanii mwenzake Diamond platinumz , ukizingatia amekuwa akijivunia kwa sababu yeye ni mmoja kati ya watu waliomuinua Diamond kimuziki.
Bob juniour anasema kuwa pengine labda hasingeamua kufanya kazi na diamond basi wasingekuwa hapa walipo , au hata wasafi isingezaliwa kwa sababu anaamini kila kinachofanyika basi kinakuwa na sababu .
Ni watu ambao tumetoka mbali sana na tumekuwa tukisaidia sana, pengi ne labda sharobaro ndio imezaa wasafi, pengine labda mimi ninsingefanya kazi na diamond wasafi isingekuwepo, kuna vipaji vingi sana mtaani na wanaimba wanasifia lakini mimi kipindi ninakutana na diamond ilikuwa mita ya magomeni pale kabisa , ni mitaa ya nyumbani, na akawa ananiambia kabisa bob naomba nifanyie kazi bhana nifanyie kazi.
Bob junior anasema kuwa pamoja na hayo , anakumbuka diamond alikuwa akifanya muziki wa ku-rap lakini alimshauri aachane na muziki huo na kufanya muziki wa aina nyingine na akili yake iliamini huko.
kipindi nakutana na Diamond alikuwa anauza duka la nguo na alikuwa akifanya muziki wa kurap,nikamwambia kuwa muziki wa kurap tuachane nao, niliona kama sio .