Natukanwa Nikimpost Hamisa:-Esha Buheti

Mwanadada Esha buheti kutoka bongo movies amefunguka na kusema kuwa mashabiki zake wamekuwa wakimtukana kila anapopost baadhi ya mastaa katika page yake kutokana na teams zilizopo katika mitandao ya kijamii.

Hata hivyo Esha anasema hawezi kuacha kumposti kwa sababu wao hawana ugomvi wowote na pia wamekuwa wakisapotiana sana ktika kazi zao hivyo hawezi kusikiliza kila mtu.

Lakini pia Esha Buheti anasema kuwa pamoja na kwamba yeye ni team kiba lakini biashara zake haziingiliani na u-team na ndio maana hata chakulaanachopika anapewa sapoti sana na kina esma platinumz, mama dangote na hata Petiti man ambae ni mume wa Esma ambao hao wote ni familia ya Diamond.

Hamisa  ni mdogo wangu, ninatukamwa sana ninapompost hamisa, esma ni mteja wangu mkubwa wa chakula pia mama dangote,karibia nusu ya Ramadhani yote Esma, Petit walikuwa wateja wangu sana.

Hata hivyo Esha anasema kuwa yeye yupo kwa ajili ya kumsapoti alikiba na hata wakati anataka kwenda kwenye mpira alimuuliza kuhusu hilo na alimjibu ni kweli ameamua kucheza mpira wakaongea na kucheka tu.

Kwa upande mwingine, Esha anasema kuwa wakati wapo katika harusi ya zabibu alisikia watu walikuwa wakisema kuwa msanii huyo kwa sasa ni kama anaumwa kwa sababu sauti yake inakuwa inakuja na kupotea.

Muigizaji wa Bongo movies – Esha Buhet alaumu ujauzito wake kwa mabaya yote anayofanya

Muigizaji Esha Buhet huyo alipata pongezi kutoka kwa mastaa wengi ilipojulikana kuwa ako na mimba, Wema Sepetu alimsifu sana Esha Buhet.

“Mashallah Esha wangu… Staha hadi Raha…. Sijawahi Elewa Wanawake wakishaenda kwenye Maternity shoots kwanini wanataka sana wakae uchi…. This Is Very Beautiful my Darling…. Allah Bariq Tumbo lako ujifungue salama my love… Unajua navyokupenda…. Hii iende kwa wanaokaaga Uchi wakiwa wanapiga picha za Mimba Jamani… @esha.s.buheti,” aliandika Wema.

Esha Buhet

Esha sasa amekiri kuwa mimba aliyonayo inampa kisirani ambayo imemfanya kuwakosea watu wengi bila ya yeye kusudia.

Akiongea na 3-Tamu, Esha aliwaomba watu ambao amewakosea waelewe hali aliyonayo kuwa ni ya mpito hivyo wamsamehe.

“Hali niliyonayo ni ya mpito na huwa inakuja na mambo mengi, hivyo ndugu zangu na jamaa zangu nawaomba wanisamehe sana kama ikitokea nikawaudhi maana naona mimba inanipeleka puta,” alisema Esha Buhet.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.