Mwanamitindo maarufu bongo na nchi za nje anaefanya vizuri tangu kipindi cha nyuma ambae pia anaweza kusemwa kama moja ya watu waliokuza sana tasnia ya mitindo nchini mustafa hasananri amempa hongera nyingi mwanamitindo mashuhuli na model wa siku nyingi Millen Magese kwa moyo wake wa kujitoa kwa kina mama wenzake na kuwapa elimu juu ya ugonjwa uliowahi kumsumbua kwa muda mrefu na kumsababisha kushindwa kupata mtoto.
Hassanaari amempongeza Millen kwa kitendo chake cha kuandaa Collection mpya yenye theme ya Endomitrisis iliyofanyika nchini Nigeria katika arise fashion week nchini humo kwa mwaka huu.
Millen ameamua kufanya hivyo ili kuonyesha kuwa wanawake wanaweza kuweka juhudi zao kama alizoamua kuweka yeye katika kupigana na ugonjwa huo ambao ulimfanya aishi maisha ya mateso kwa muda mrefu bila kupta amtoto na hata baada ya kutokukta tamaa mwanamitindo huyo alibahatika kupata mtoto mmoja wa kiume .
Millen pia amemshukuru sana hassanari kwa kumuona na kuona juhudi zake katika kufanya hilo.Millen ni moja ya wanamitindo maarufu na wanaoheshimika sana nchini Nigeria.