Msanii anaefanya vizuri sana katika muziki tangu miaka ya 90 mpaka sasa Lady Jay Dee aliamua kufunguka na kutoa ufafanuzi juu ya video iliyosambaa ikimuonyesha anacheza alipokuwa akifanya video ya wimbo wake mpya wa anaweza ambapo mwanadada huyo alikatiza kucheza kutokana na wigi alilokuwa amevaa kichwani kuangauka,
Wadada wengi wamekuwa wakivaa mawigi ili kuficha nywele zao kichwani na wengine kupata aibu sehemu za watu hasa pale ambapo wigi linlaegea na kushindwa kukaa kichwani.
Akiongea na bongo 5 huku akicheka , lady jay dee alisema kuwa hiyo ni ajali kazini”lilianguka..ilikuwa kwamba wigi lilianguka chini na ikawa ni kama ajali kazini“-huku akicheka Jay Dee aliongea.
Huku akifafanua kama kuna uwepo wa project nyingine baada ya hii ya anaweza. Jay Dee anasema kuwa ni mapema sana kwa sasa kuzungumzia swala hilo kwa sababu hata hii iliyopo sasa bado ndio kwanza imepokelewa hivyo anawaacha mashabiki kufurahia swala hilo kwa sasa.
