“Dogo Janja Sio Mwanaume Wa Dar”- JCB

Mwanamuziki mkongwe wa Hip hop toka Arusha JCB amefungukia ishu ya Dogo Janja kumuoa Uwoya na kusema siyo mwanaume wa Dar kama watu wengi wanavyofikiria.

JCB amefunguka na kumsifia Dogo Janja baada ya kufanikiwa kumuoa mtoto mzuri kama Wolper na kudai amewababr watu wa Arusha na kusisitiza kuwa Dogo Janja sio mtu wa Dar.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Enews ya East Africa Tv, JCB amefunguka na kumsifia Dogo Janja kwa kitendo chake cha kufanikiwa kumuoa Irene Uwoya:

Unajua kwa Dogo Janja kumuoa mama kama yule pale ametupa Big up na kutupandisha na kutufanya sisi watu wa kaskazini sio wanaume wa Dar yaani tuna nguvu kwa upande huo tu wa kuwa na yule mwanamke yaani Nampa Big up sana Dogo kama anamchukua yule mtoto ametuwakilisha watu wa Arusha vizuri”.

Lakini Pia JCB alipima uzito suala la Dogo Janja kujigeuza mwanamke kwa ajili ya video yake ya wimbo wake wa Wayu wayu ambapo ameweka wazi kuwa hajui Dogo Janja alikuwa anafikiria nini kufanya vile lakini kile ni kitendo ambacho hawezi kufanya.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.