Baada ya kukaa kwa muda mrefu akiwa kimya tangu mkataba wake wa kufaya kazi na Wanene sudio kuisha Producer Lufa ameanza kurudi tena huku akifanya kazi katika studio mpya. Mtayarishaji huyo ameonekana akifanya kazi na Gosby katika studio yao mpya iliyoanza kazi hivi karibuni.
Lufa ambae aliwahi kuweka mkono wake wa baraka katika studio za switch records kwa sasa anaingia rasmi kufanya kazi na 601 world wide records akiwa kama mtayarishaji wa nyimbo katika studio hiyo.
Akiongea hayo msanii Gosby anasema “nimeachia kionjo ca ngoma yetu mpya ambayo imekamilika tayari ,kinachosubiriwa kuingia location ndio tunajiyarisha kwa sasa.Hii ni studio yangu mpya na rafiki yangu Lufa ndio mtayarishaji wetu.”