Muigizaji Elizabeth Michael akana taarifa za ndoa yake na Majay

Elizabeth Michael hivi karibuni alikuwa anasemekana kuwa anatarajia kufunga ndoa na mpenzi wake Majay ambaye pia ni bosi wa EFM na TVE. Taarifa hii ilienea baada ya magazeti kadhaa ya Tanzania yalioandika kusema kuwa walifanya mahojiano na mrembo huyo.

Hata hivyo Elizabeth Micheal anaejulikana kama Lulu amekana taarifa hizi kupitia mtandao wa Twitter baada ya kuandika ujumbe uliosema…

“Hivi kwa Akili yenu Ndoa inatangazwaga Kwenye Magazeti!??Muwege mnajiongeza kabla ya kuparamia Story…!.”

Hii inakuja baada ya gazeti la Mtanzania lilikiri kwa kumnukuu muigizaji huyo…

“Siku zinakaribia na karibu tarehe ya ndoa yangu itatangazwa kwa uwezo wa Mungu. Hapo ndipo waliotamani tuachane wataziba midomo, maana natarajiwa kuwa mke halali hivi karibuni.”

Kwa hivi sasa inaonekana kuwa Lulu hana mipango ya kuolewa.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.