Nay Ana Wanawake Wengi Sana.:Nini.

Mwanadada nini mbae hivi karibuni alijikuta akiingia matatani baada ya kuamua kutangaza katika mitandao na vyombo vya habari kuhusu kuwa single na kwamba ameachana na nay wa mitego ambae alikuwa mpenzi wake na mahusiano yao waliyafanya kwa siri kwa muda wote.

Huku watu wakihoji kwa nini ilikuwa siri na sasa hivi wameachana na wameamua kutangaza au kwanini wawili hao wameachana, ndipo Nini alipoamua kufunguka kwa waandishi na kusema kuwa swala kubwa ni kutokana na tabia ya Nay wa mitego kutokuwa na mapezni ya kweli kwake na kwamba amekuwa na mahusiano na wanawake wengine wengi.

Nay ana wanawake wengi sana , nimevumilia na nikaona kuwa basi kila mtu na achukue hamsini zake tu,nimeshamsisitza zaidi ya mara mbili lakini nikaona hanisikilizi kwaio nimeona bora nikae pembeni’ Aliongea Nini alipokuwa akihojiwa na Sam misago.

Pamoja na kwamba Nini aliwahi kugombana na uongozi wake kwa sababu ya uhusiano wake na Nay na kuwafanya wawili hao kuanza kufanya kazi pamoja, Nini anasema kuwa swala hilo halimaanishi kuwa  limekwamisha na kuua muziki wake bali yuko pale pale.

Nini Akanusha Kuachana na Nay Kisa Wazazi.

Mwanadada mabe ni msanii wa bongo fleva nchini Nini amefunguka na kusema kuwa hakuna sababu ya wazazi iliyomsababisha yeye kuachana na mpenzi wake ambae pia alikuwa akifanya nae kazi Nay wa mitego.

Akiongea na Soudy Brown , nini anasema kuwa pamoja na kwamba Nay alisema kuwa wazazi wake ndio chanzo kikubwa vha yeye kuachana na mwanaume huyo lakini sio kweli kwa sababu wazazi wake hawajawahi kuingilia kabisa mahusinao yao .

Hata hivyo baada ya nini kuulizwa sababu kubwa ya kuachana na Nay , alisema kuwa alichoshwa na  vituko vya mwanaume huyo ukizingatia kuwa alikuwa akimfanyia vitu vya kinyama na kutembea na wanawake wengine huku wengne akiwaleta ndani na yeye mwenyewe akiwepo hivyo alivumilia kwa muda mrefu na sasa amechoka na kuamua kuachana nae.

Nini pia amekanusha tetesi zilizokuwa zikisambaa kuwa alikuwa akikaa na Nay nyumba moja hivyo walivyogombana na Nay kwa sasa amerudi nyumbani kwao kwamba sio kweli kuhusu hilo.

Mahusiano na Nay na Nini yalikuwa ya chii chini huku kila anayeulizwa anashindwa kukubali kuwa wapo katika mahusiano lakini cha kushangaza wamegombana kila mmoja amejikuta anatangaza katika ktandao ya kijamii.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.