Faiza Amwaga Machozi Baada ya Kubeba Mimba Nyingine.
Mwanadada Faiza Ally amejikuta akiingia katika wakati mgumu baada ya kunasa mimba nyingine ya tatu huku mtoto wake wa kiume wa pili akiwa bado na umri wa miezi nane tu huku yeye mwnyewe akiwa anajipa moyo kuwa hawezi kupata mimba kwa sababu alikuwa akitumia vidonge vya kuzuia mimba.
Alikuwa akitoa taarifa juu ya swala hilo anasema kuwa Faiza hakujua kama angeweza kubeba mimba kwa sababu alikuwa anatumia njia ya kuzuia mimba lakini kwa bahati mbaya laipata mimba huku akiendelea kunywwa dawa hizo ambazo zilikwedna na kuharibu mimba hivyo kuanza kuumwa bila kujua anaumwa nini.
Msemaji huyo anasema kuwa baada ya hapo alikwenda hospitali ambapo alikwenda na kugundua tatizo kuwa alikuwa na mimba iliyoharibka kutokana na kutumia vidonge hivyo,alipofika hospitali waligundua tatizo hilo huku wakiona kuwa mimba ilikuwa imeharibika hivyo kuamua kumsafisha ili kumuweka sawa.
Baada ya kuongea na msemaji huyo gazeti Moja waliamua kumtafuta faiza ally mwenywe ilikuthibitisha habari hizo na ndipo aliposema haya”ni kweli nilikuwa mjamzito, unajua mimi na baba yake mtoto tunakaa mbalimbali kwahiyo inabidi tutumie dawa za kuzuia mimba, kumbe dawa tulizokuwa tukitumia hazikuwa za kuzia zilikuwa ni za kuharibu kabia kwaio hata ilipoingia kwa bahatimbaya iliharibiwa na dawa hizo, lakini haukutoka vizuri ndio nikawa najisikia vibaya na kuumwa mpaka nilipokwenda hospitali.
Hata hivyo Faiza Ally alipoulizwa kama angekuwa tayari kuzaa kama mimba hiyo isingeharibika huku wakikariri amneno yake ya mwanzo kuwa watoto wawili wanatosha alijibu kuwa kwa sababu mimba iliingia kwa bahati mbaya hasingeweza kuitoa hata kidogo kwa sababu hawezi kufanya hivyo.
