Tuliwahi Kununiana na Mume Wangu Karibia Mwezi :-Upendo Nkone
Msanii wa nyimbo za injili Upendo Nkone amejaribu ku-share experience ya maisha yake ya ndoa na mashabiki wake kutokana na mawazo ambayo watu waengi wamkuwa nayo kuhusu watumishi wa mungu katika kupambana na matatizo yao.
Upendo Nkone anasema kuwa hata yeye katika maisha yake ya ndoa amekuwa na changamoto mbalimbali kama wanazopitia watu wengi huku akisema kuwa kuna muda hata yeye na mume wake huwa wanagombana.
Japokuwa mume wangu ni mchungaji lakini kuna muda huwa tunagombana na huwa tunalianzisha ,tunafunga na milanngo, tuliwahi kununiana ndani karibia mwezi.kwa mfano unakuwa kuna siku ninakuwa sijapika na huo ndio ugomvi wetu mkubwa na yeye,apike mdada wa kazi alafu unakuta chakula hakijakaa sawa hapo ndo utamjua mbena ni nani.-Anasema Upendo Nkone.
