Mimi ni Mzuri Katika Mapenzi ;- Queen Darlen
Mwanadada Queen Darlen kutoka katika lebo ya WCB amefunguka na kujitapa kuwa yeye ni moja ya wasichana wachache ambao wamekuwa wazuri sana katika mapenzi ila watu hawajui kutokana na kuangalia sana muonekano wake.
Akiongea na waandishi wa habari, mwanadada huyo anasema ‘Mimi ni mzuri sana katika mapenzi kuliko hata vile watu wanavyofikiria, tena sana,”
Queen Darlen ambae amekuwa siku zote akisemwa vibaya kutokana na kuwa na muonekano wa kiume na kwamba watu wengi wamekuwa wakisema kuwa mwanadada huyo hana mahusiano kutokana na vile alivyo.
Licha ya hayo lakini pia haiajwahi kuonekana katika mitandao ya kijamii mwanadada huyo akiwa na mwanaume ambae anaweza kusadkika kuwa mpenzi wake zaidi ya kuwa akizushiwa lakini tetesi hzo zinakuwa hazina ukweli wowote.
Mwanadada huyo ambae ni mwanamke pekee katika kundi hilo amekuwa akionekana kuwa wa tofauti kila mara labda kwa sabab mara nyngi amekuwa akiandamana na wanaume hivyo inakuwa ngumu kwakekujiingiza katika mahusiano kama mashabiki wanavyotaka awe.
