Chemical Awatolea Povu Wanaomsema Kuhusu Mavazi.
Msanii raper wa kike nchini Chemical amejikuta akiwatolea povu kali mashabiki zake katika kurasa mbalimbali za instagram na mitandao ya kijamii kutokana na kuwa wanamsema jinsi anavyovaa haiendani na jinsia yake.
Chemical amejikuta akiingia katika wakati mgumu na kuwajibu mashabiki zake kuhusu swala hilo huko akisema kuwa hakuna mwanaume anaeweza kuvaa nguo zake.
kama kuna mwanaume anavaaa nguo zangu basi ajijue kabisa kuwa yeye sio mwanaume , na wewe ambae kila siku unakaa ku-judge nguo zangu basi ujue kabisa kuwa huna kazi ya kufanya , mimi ninavaa ninavyojisikia kuvaa na uanamke wangu haupo katika mavazi.
