Kisa Wema , Diamond Amtolea Povu Shabiki.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platinumz amejikuta akimtolea povu zito moja ya mashabiki zake katika mitandao ya kijamii baada ya mashabiki hao kumtolea povu Wema Sepetu na kumkejeli.Shabiki huyo ambae aliweka maoni yake katika post moja wapo ya ambayo walionekana wawili hao wakiwa njiani kuelekea katika party ya Rommy Jones.
Diamond alionekana kumkingia kifua Madam Wema na kusema kuwa kushikana na wema ni moja ya sehemu ya kazi yake hivyo hawezi kuacha kufanya hivyo.


