Mboso Awaonya Wanaomfananisha na Aslay
Msanii Mboso kutoka katika kundi la WCB amefunguka na kuwaonya baadhi ya watu ambao wamekuwa wakimfananisha na msanii mwenzake Aslay ambae amkuwa akifanya muziki kwa kujitegemea tangu kuondoka kwa kundi lao la ya moto.
Mboso anasema kuwa hawezi kufafanishwa na Aslay kwa sababu Aslay alianza muziki kabla yake na kabla hata ya kuundwa kwa kundi walikuwa wakifanya kazi hivyo hawawezi kulingana katika hilo.
hakuna kitu ninachokiona alafu nikajisikia vibaya kama ninapoona ninafananishwa na Aslay, yuke mimi ni kaka yangu na isitoshe mimi nimeanza music kama solo artist nikiwa na miezi 9 tu lakini yeye kaanza muziki tangu mwaka 2011.Ukinifananisha nae unakuwa unamvunjia heshima yake.
Mboso , Aslay na wasani wengine wawili walikuwa wakifanya kazi katika kundi moja lakini baada ya kundi hilo kuvunjika kila mmoja alianza kuimba kama msanii wa kujitegemea huku Mboso akisajiriwa na WCB kuwa chini yao.
