Mzazi Mwenzie na Shilole Afariki Dunia,
Mwana dada mpambananji , Zuwena Mohamed amefikwa na msiba wa kuondokewa na mzazi mwenzie walie bahatika kupata nae mtoto mmoja wa kike wa kwanza,mwanaume huyo aliekuwa akiitwa Elias makala amefariki leo huko Igunga Mkoani Tabora ambapo alikuwa haugui kitu chochote.
Shiloleh amethibitisha kifo icho cha mzazi mwenzie baada ya kusema kuwa marehemu hakuwa anaumwa chochote ila alikuwa akitoka katika sherehe na kurudi nyumba na ndipo mauti yalipomkuta.
Shiloleh anasema kuwa marehemu alikuwa mzima na mara ya mwisho kuwasiliana nae ilikuwa miezi miwili iliyopita , Lakini kwa taarifa alizozipata kutoka kwa ndugu zinasema hakuwa na ugonjwa wowote uliomsumbua kabla.
Marehemu na msanii Shiloleh walifanikiw akupata mtoto wa kike ambae ndie mtoto wa kwanza wa shilole ambae sasa hivi ana miaka 14.