Nitajitahidi Niwe na Roho Mbaya ili Nifanikiwe;-Wema Sepetu

Mwanadada Wema Sepetu amefunguka na kusema kuwa  mara nyingi sana amekuwa akiowaona watu wenye roho ngumu na ucghoyo wamekuwa wakifanikiwa kitu ambacho kwa upande wake anaona kama hawezi kutokana na ule wema wake kwa watu.

Hata hivyo wema anasema kuwa kwa upande wake yeye inakuwa ngumu kuwa na roho mbaya kwa sababu mungu anakuwa tayari amekuumba hivyo hivyo huwezi kubadilika hata kidogo katika hilo.

download latest music    

Lakini amesema kuwa na yeye atajitahidi kuwa na roho mbaya ili aone kama inawezekana kufanikiwa kama wengine.

Wanasemaga watu wenye roho mbaya wanafanikiwa sana, na mimi roho hiyo sina kwa sababu ninachoamini ni kwamba kama umejariwa roho nzuri basi hiyo ni roho yako tu huna haja ya kuwa na roho nyingine, sometimes roho yangu nzuri inaniponza sana.ila nitajitahidi kujifunza roho mbaya.

Akiongelea kuhusu kesi yake iliyoisha hivi karibuni wema ansema hana la kusema zaidi ya kumshukuru mungu kwa kuwa kipindi icho alikuwa katika wakati mgumu wa kufanya mambo mengi kwa kusua sua.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.