Penzi la Otile na Vera Sidika Lafika Ukingoni.
Penzi la mwanadada maarufu nchini Kenya Vera Sidika na msanii Otile brown lasemekana kufika pabaya baada ya wawili hao kusadikika kuwa wameachana na kila mtu kwa sasa anaendelea na mambo yake.
Mahusiano hayo ambayo yalikuwa gumzo katika mitandao kutokana na umaarufu wa mwanadada huyo kutoka na kijana huyo ambae alikuwa akionekana mdogo wa umri kwa mwanadada huyo.
Wawili hao ambao walidumu kwa zaidi ya miezi mwili walionekana kuwa pamoja maeneo mengi hasa katika baishara za mwanadada huyo na katika shughuli mbalimbali za kijamii haijaelezwa kitu gani kimevunja mahusiano yao.
katika kurasa zao za instagram, kila mmoja alikuwa akiweka picha nyingi za mwenzie na zile walizokuwa pamoja zinaonekana kufutwa kutoka kila upande.
