Diamond aagiza tani 100 za karanga kutoka kwa wakulima

Staa wa Wasafi Diamond Platnumz anapanua biashara yake ya karanga. Hit maker huyo wa ‘Eneka’ ameagiza tani 100 ya karanga kutoka kwa wakulima nchini.

Diamond alitoa ombi hilo kupitia account yake ya Instagram:

FURSA KWA NDUGU ZANGU WAKULIMA WA KARANGA…. sasa waweza kutuuzia karanga mbichi nyeupe zenye rangi ya kwenye picha hapo, Maarufu kama Super Quality Small size….

Kuna nafasi ya kununua hadi Karanga Tani mia moja (Tani 100) kwa kila Mwezi… Usafi na Ubora wa karanga zako ndio nguzo ya kwanza sisi kuweza kuzinunua karanga zako….Wasiliana nasi kwa namba hizi +255714993724 @diamondkaranga #NogewaJirambe ?? MAZINGATIO:

  1. Karanga ndogo Nyeupe (Super Quality Small Size)
  2. Ziwe Safi sana sana.
  3. Zifungwe katika ujazo wa kilo 20 kwa kiloba.
  4. Tunanunua kwa Bei kati ya tsh 2300 – tsh 2700 kwa kilo.
  5. Maitaji yetu ni tani 100 kwa mwezi.
  6. Piga simu: +255-714-993-724

Diamond karanga yaanza kuuzwa Kenya pia

Diamond Platnumz alizindua bidhaa yake mpya ‘Diamond Karanga’ baada ya kumlaki sta wa Wasafi – Rayvanny kutoka Marekani.

Kuzinduliwa kwa Diamond Karanga uliwashangaza watu wengi kwani Baba Tiffah alianza tu kuuza manukato yake ‘Chibu Perfume’ miezi michache iliyopita.

Diamond sasa anauza karanga zake Tanzania nzima na ata Kenya pia; staa huyo amesema Diamond Karanga zauzwa Mombasa kwa sasa.

“USISEME KARANGA SEMA DIAMOND KARANGA!!!!…Habari njema kwa Vijana wenzangu wote, sasa unaweza kujipatia Mtonyo wa ChapChap kupitia @diamondkaranga ambapo utaweza kununua kwa bei ya jumla ya shilingi elfu ishirini (20,000) kwa boksi moja lenye pakiti Mia moja (100) ndani ambazo ukiuza unapata faida ya elfu kumi fanya mawasiliano sasa na mawakala walio karibu yako. Mawasiliano kwa Kununua Jumla:- MOMBASA +254700187727” aliandika Diamond.