Moni Centrozone Afungukia Bifu Lake na Roma

Msanii wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kurap Moni Centrozone amefunguka na kuongelea bifu lake na msanii mwenzake Roma.

Roma alikuwa ni mmoja kati ya watu wa karibu wa Moni kwa muda mrefu walikuwa washkaji na walikuwa wanaonekana wote pamoja lakini Miezi ya hivi karibuni ukaribu huo umepotea.

Kwenye mahojiano na Millard Ayo, Moni anafunguka na kuweka wazi kuwa sababu kubwa iliyofanya wawili hao kupoteza ukaribu ni baada ya Roma kuingia kwenye group na Stamina (Rostam) bila kumpa taarifa yoyote.

Mimi na Roma hatuna ushkaji tangu alipoamua kufanya projects zake na Stamina bila kunipa mimi taarifa kwaiyo nikaona kama nimepunguzwa bila kufanya kosa lolote ndipo na nilipoamua kujiongeza na kuamua kufanya kazi mwenyewe.

Tangu hapo nimefanya projects kadhaa kama matango pori, Bongo supastaa na kusema ukweli nimeweza kufanya vizuri mwenyewe na maisha yanasonga”.

Moni amesisitiza kuwa hana bifu na Roma kwa sasa Lakini pia hana urafiki naye na hataweza kufanya nae kolabo.

Nai Adai Gigy Money ni Mnafiki na Sio Rafiki Mzuri Kwake

Video vixen maarufu Bongo Nai ambaye pia ni mpenzi wa msanii wa Bongo fleva Moni Centrozone ameibuka na kumtolea povu Gigy Money kwa kudai sio rafiki mzuri.

Gigy Money na Nai walionekana kuwa na ukaribu mkubwa siku za hivi karibuni hasa baada ya Gigy Money kuachana na Mo j na Nai kuachana na Moni centrozone.

Lakini ukaribu huo uliingia mdudu baada ya habari kusambaa kuwa Gigy anatoka na Moni na hata alibadilisha jina lake na kujiita Gigy Centrozone Kwenye Instagram.

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, NAi anafunguka na kuweka wazi kuwa ameumizwa na kitendo kilichofanywa na Gigy Money ambaye amekiri kuwa sio rafiki mzuri kwake:

Gigy sio rafiki mzuri kwangu kwa sababu ni mtu ambaye anajaribu kuniongelea vibaya hata kwa Moni ambaye alimposti na kujibadilisha jina na pia kajaribu kumpelekea vitu vya uongo vingi ambavyo vimetufanya mimi na Moni mpaka sasa hatupo sawa.

Na pia naweza kudiriki kusema kuwa Gigy sio rafiki wa kweli kwangu hivyo nimemuweka pembeni nina maisha yangu mwenyewe sihitaji watu wanafiki”.

Nai amekiri kuwa Gigy Money alimtafuta ili wayamalize lakini amesema hataki Tena urafiki naye kwani ameharibu uhusiano wake na mpenzi wake Moni.

Nai Adai Gigy Money ni Mnafiki na Sio Rafiki Mzuri Kwake

Video vixen maarufu Bongo Nai ambaye pia ni mpenzi wa msanii wa Bongo fleva Moni Centrozone ameibuka na kumtolea povu Gigy Money kwa kudai sio rafiki mzuri.

Gigy Money na Nai walionekana kuwa na ukaribu mkubwa siku za hivi karibuni hasa baada ya Gigy Money kuachana na Mo j na Nai kuachana na Moni centrozone.

Lakini ukaribu huo uliingia mdudu baada ya habari kusambaa kuwa Gigy anatoka na Moni na hata alibadilisha jina lake na kujiita Gigy Centrozone Kwenye Instagram.

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, NAi anafunguka na kuweka wazi kuwa ameumizwa na kitendo kilichofanywa na Gigy Money ambaye amekiri kuwa sio rafiki mzuri kwake:

Gigy sio rafiki mzuri kwangu kwa sababu ni mtu ambaye anajaribu kuniongelea vibaya hata kwa Moni ambaye alimposti na kujibadilisha jina na pia kajaribu kumpelekea vitu vya uongo vingi ambavyo vimetufanya mimi na Moni mpaka sasa hatupo sawa.

Na pia naweza kudiriki kusema kuwa Gigy sio rafiki wa kweli kwangu hivyo nimemuweka pembeni nina maisha yangu mwenyewe sihitaji watu wanafiki”.

Nai amekiri kuwa Gigy Money alimtafuta ili wayamalize lakini amesema hataki Tena urafiki naye kwani ameharibu uhusiano wake na mpenzi wake Moni.

Moni Akumbushia Kutekwa Kwao, Ilikuwa Siku Kama Leo

Msanii wa hip-hop Moni Centrozone amekumbishai siku kama ya leo mwaka uliopita walikuwa katikamatatizo mazito kutokana na kutekwa kwao na watu wasiojulikana akiwa na wenzake na mmoja wapo akiwa ni  Roma mkatoliki.

Kupitia ukurasa wake wa instagram , Moni aliandika kuwa siku kama ya leo imekuwa ikikaa kichwani mwake kila saa na huwa hawezi kuisahau,aliandika”

siku kama ya leo mwaka 2017 watu wasiojulikana walikuja na kuingia studio wakajitambulisha na kutubeba kama kuku,tulifungwa mikono na macho na kisha tukapelekwa umbali mrefu , tukasimama sehemu watu wakiwa wananong’onezana kma dakika 20 kisha tukapelekwa kwenye nyumba ambayo tulikula kisago heavy , mijeledi mateke na marungu kwa mara ya kwanza nilisali sala yangu ya mwisho nikijua ndio mwisho wangu.

Siku tatu baada ya kutekwa kwa wasanii hao tarehe 08 mwezi huo, walipatikana na kupelekwa katika kituo cha polisi cha oysterbay kwa mahojiano zaidi ingawa mpaka leo hakuna lililowekwa wazi kuhusu wasanii hao kutekwa.

Moni Amkana Roma Mkatoriki,Asema Hana Mchango Wowote kwake.

Msanii wa musiki wa Hip-Hop nchini Moni Centrozone amefunga na kusema kuwa msanii mwenzie Roma hana mchango wowte katika musiki wake kama watu wanavyokuwa wanafikiria.Moni amesema kuwa watu wengi wamekuwa wakisema kuwa amekuwa msaada mkubwa katika muziki wake lakini ukweli ni kwamba hakuna chochote zaii ya kumpa shida tu tena hasa baada ya kutoa nae wimbo ambao wengi walihisi utasaidia kumtambulisha lakini imezidi kumletea shida.

Moni alitoa majibu hayo baada ya kuulizwa kuhusu kuunganika kwao na Country Boy na kuleta muungano uliojulikana kama MoCo ili kuweza kushindana na muungano wa Rostam ambao ni muunganiko wa Roma na Stamina, ndipo aliposema kuwa kwa upande wake hana mashindano na mtu yoyote zaidi ya kufanya muziki wake.

Moni anasema kuwa katika watu ambao hawezi kuwasahahu katika muziki ni marehemu Langa ambae alikuwa  wa kwanza kugundua kipaji chake tangu zamani na kuweza kumsadia kumpa njia kuingia katika muziki.

Who is Roma kwenye maisha yangu,mimi simfahamu na wala hajawahi kunitoa katika muziki kama watu wanavyodhani.namjua langa ambae alinitoa uswahili na kunileta mjini.sipeni kutajiwa majina ya watu wasiokuwa na umuhimu katika maisha yangu.

Moni ameendelea kusema kuwa kundi alilolianzisha na Country haliwazuhii kufanya muziki wao kama solo artist ,lengo la kundi ni kuleta changamoto kwa wasanii wengine.

Moni na Roma walishawahi kufanya kazi ya pamoja na kumfanya Moni kujulikana sana , ambapo ukaribu wao ulipelekea wawili hao kutekwa mnamo April mwaka huohuo.Baada ya kuachiwa kutoka kusikojulina msanii Roma alitoa wimbo ulijulikana kama Zimbabwe ambao ulielezea kwa ufupi tukio ilo lakini kumbe Moni alichukia  kitendo icho na kusema kuwa Roma ametumia idea ya kutekwa kama tukio ilo lilimpata peke yake ilhali walikuwa wanne.

Moni aeleza kilichotokea alipotekwa nyara aliwa na Roma Mkatoliki

Moni Centrozone amefunguka kuhusu tukio lililofanyika karibu mwezi moja uliopita – alitekwa nyara na watu wasiojulikana akiwa studio.

Rapper huyo alitekwa nyara akiwa na Roma Mkatoliki, producer Bin Laden na Imma wakiwa katika studio za Tongwe Records.

Roma Mkatoliki na Moni Centrozone

Moni alisimulia kilichofanya katika kipindi cha XXL cha Clouds FM. Soma maneno aliyosema hapo chini:

“Yule jamaa wakati ananiambia nimpe simu ya Roma, wakati naifata simu ya Roma akawa ameshaingia akaiwahi, akaichukua akaniambia wewe ndo Moni? Wewe ndio sembe sembe dona? Kaa hapo chini nimekwambia, kaa kwenye kochi simu yako iko wapi? Nikamwambia simu yangu ipo kwenye chaji, akamuuliza na Bin Laden, naye Bin Laden akatoa simu. Akauliza Junior yuko wapi? Mpigie J-Murder sasa ile hali ya vitisho ikawa imeshaanza,

“Kumpigia J-Murder hata kabla sijamaliza maelezo yaani ile bosi kuna watu wamekuja hapa studio, jamaa akanipora simu. Oya inakuwaje J-Murder, sisi hapa tunataka kurecord, tunataka kurecord nyimbo sita.

“Muda ambao nakumbuka nimesali sala zangu za mwisho ni ule pale, nikaona dah basi kama kuna kitu nimefanya au kuna kitu nimekosea basi ni kumuachia Mungu,” Moni Centrozone alisimulia kilichotokea.