Diamond Adaiwa Kutelekeza Watoto

Msanii Diamond Platinumz anadaiwa kutelekeza watoto wake wawili aliozaa na mwanamama Zari the bossy kutoka Uganda kama ilivyokuwa ikiripotiwa na mwanamama huyo Katika mitandao ya kijamii katika kurasa zake akijibu watu katika upande wa maoni.

Mwanamama huyo ambae amekuwa akiwajibu watu kuwa kwa sasa amekuwa akilea watoto yeye mwenyewe imetasfiri na watu kuwa inawezekana mwanamama huyo ni kweli ameamua kutoa siri hiyo kwa watu kuhusu malezi ya watoto hao.

Hata hivyo maoni ya mwanamama huyo yanazidi kuibua hisia kali kwa mashabiki kuhusu diamond kubagua baadhi ya watu wake wa karibu kwa kuwahudumia ukizingatia kuwa hivi karibuni amekuwa na na  tuhuma za kukataa kumuhudumia baba yake mzazi ambae amekuwa mgonjwa kitandani pamoja na kwamba amekuwa akiomba msaada kupitia mitandao.

 

Zari Amtolea Povu Diamond Kuhusu Malezi kwa Watoto Wake.

Mwanadada Zari The Bossy ameshindwa kuvumilia yale ya moyoni na kuamua kusema kile anachokiona kwa msanii Diamond Platinumz kuhusu malezi kwa watoto wake.

Zari ambae ameachana na Diamond kwa muda mrefu sasa na kuamua kukaa na watoto wake aliowapta an amsanii huyo anasema kuwa anamshangaa sana Diamond kwa kitendo cha kukubali kutumia muda wake mwingi kwa ajili ya kufanya starehe na sio kuwajali na kuwa karibu na watoto wake mpaka anasaidiwa na wanaume wenzake.

Akitupa bango hilo katika ukurasa wake wa snapchat, zari aliandika “too bad your kids will have all this  beautiful memeries with somebody else..the simple things money cant buy.”

Pamoja na kwamba diamond amekuwa akionekana yuko afrika ya kusini akiwa na watoto hoa, kwa mujibu wa zari anaona kuwa watoto hao hawapati muda mzuri na wa kutosha kukaa na baba yao hivyo wamekua wakipewa mapenzi ya baba  na watu wengine.

Lakini pia Zari anasema kuwa pamoja na kwamba Diamond amekua na pesa lakini kuna vitu haw=viwezi kununuliwa kwa pesa ikiwepo hilo.

Zari Athibitisha Maneno ya Diamond Kuwaita Watoto Kima

Mwanadada  Zari the bossy aliamua kumuwish ba awa watoto wake diamond platinumzkheri ya  kmbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwake  ambapo , kama ilivyo hapo awali zari nae alipokea salamu hizo kutoka kwaDiamond.

Ingawa hali imekuwa ni tofauti kwa Diamond na kwa zari kwa sababu Diamond alimuandikia Zari maneno matamu sana yaliyofurahisha wengi lakii hii imekuwa tofauti kwake.

Katika ukurasa wake wa instagram, Zari aliweka picha ya watoto wake wawili aliozaa na Diamond na kisha kuandika “HAPPY BIRTHDAY MWENYE KIMA VYAKE” Kitendo achmbo inawezekana wengi hawakukitegemea kabisa kutoka kwa mwanamama huyo.

Hata hivyo neno la kima lilitoka kwa diamond mwenyewe hapo kipindi cha nyuma alipokuwa akigombana na hawa baby mamas wake na kujikuta akiwaita watoto majina mabaya kama hayo.

Diamond Afunguka Kuhusu Kumuomba Radhi Mama Watoto Wake Zari

Msanii wa bongo fleva maarufu  nchini , Diamond Platinumz kwa mara ya kwanza amefunguka na kuzungumzia swala lake la kuachana na Diamond na kumuomba radhi mwanamama huyo ambapo taarifa za hapo awali ziliwahi kusema kuwa kwa sasa Diamond amekuwa akipiga safari nyingi za Afrika ya Kusini ili kuomba radhi  kwa mwanamke huyo.

Akizungumza na mwandishi wa habari alipoulizwa kuhusu mambo mengi na vijembe vingi ambavyo diamond amekuwa akitupiwa na mwanamama huyo hasa vya hapa karibuni alipokuwa kenya, diamond alisema’hayo ya kenya bwana tuachane nayo, mimi nadhani yameshapita naomba tuendelee na  haya yabsasa itapendeza sana

Hata hivyo, mwandishi hakuishia hapo ndipo alipoamua kumuuliza moja kwa moja kuhusu yeye kuwa akisafiri kwenda afrika ya kusini kwa ajili ya kuomba radhi kwa zari huku akienda kwa siri mara kwa mara na diamond alijjibu kuwa safarizake za afrika ya kusini haziusiani na mambo hayo.

ni kweli ninaenda na so mara moja au mara mbili nimekuwa ninaenda,nakwenda kule sio kwa ajili ya kumuomba msamaha , hapana ila ninakwenda kule kwa ajili ya kumuona wanangu tu,haiwezekani niwe ninatuma pesa za matumizi tu alafu ninafka mpaka afrika ya kusini na nisiende kuwaona wanangu.

hao wanaosema kuwa sijui nimekuwa nikimuangukia nadhani yatakuwa ni maoni yao tu wala sio yangu, ni maneno yasiyokuwa na msingi, zari ni mama wa watoto wangu na itabaki kuwa hivyo.

Ni muda sasa umepita tangu wawili hao kutengana na kumekuwa na mogogoro mingi kati yao hasa kupitia katika mitandao ya kijamii lakini hii haijamfanya diamond kuacha kuwa na hamu ya watoto wake , mara kwa mara amekuwa akienda kuwaona kama alivyokiri.

 

Zari Azidi Kudidimiza Penzi La Diamond Platinumz

Yawezekana inakuwa vigumu kwa mtu kutamka wazi  na moja kwa moja kuhusu kutokuwepo tena kwa mahusiano baina yake na mtu wa karibu aliyekuwa akimpenda, akimtangaz kwa watu na kujulikana na watu wote, saa zingine huwa ni maumivu kukubali hadharani kuwa ulimpenda mtu fulani lakini kwa sasa penzi lile limeisha.Hii inaweza pia kuwa ni moja ya sababu labda kwanini Diamond na Zari hawataki kuweka wazi juu ya kinachoendelea katika mahusiano yao.

Wakiwa kama wazazi wenye watoto wawili , ni vigumu kukubali ukweli kuwa inabidi kila mmoja aendelee na maisha yake, lakini vipo baadhi ya viashiria vinavoweza ku-Connect dots kuwa wawili hao kuwa hawapo katika mahusiano mazuri.

Zari the Bossy Lady, mzazi mwenzie na Diamond Platinumz amekuwa akipost picha na kuweka captions zeny maneneo ya kulenga kitu fulani kwa mtu fulani hata kama hasemi moja kwa moja kuwa  inamrenga nani zaidi.Ukimya wa watu hawa wawili na kutokuonekana pamoja pia kunafanya mashabiki kuamini kuwa penzi lao limekwisha.Katika moja ya post zake katika mtandao wa Snapchat jana , Zari The Bossy aliandika”ati nini ,?yule wa wawapi? hana gina ati mama T,unachako huku.Can i be left out of this drama plse.Naomba.” aliandika zari.

Hata hivyo , hivi karibuni ilikuwa Diamond alishereka sikikuu ya kuzaliwa kwake lakini mama mzazi wa watoto wake hakutokea wale kumtakia kheri ya sikikuu ya kuzaliwa.Hii bado haitoshi, Zari The Bossy Lady ameamua kufuta picha zote za Diamond katika ukurasa wake wa instagram, hali ambayo sio ya kawaida kwa watu wanaopendana kufuta picha gafla.lakini bado siku kama mbili zilizopita majina ya accounts za watoto wa Diamond katika instagram yalibadilika na kufutwa kwa jina la pili ambalo ni jina la baba yao mzazi Diamond Platinumz.

Kumekuwa na mambo mengi yanayoendelea kati ya watu hawa wawili ingwa bado hakuna aliyetayari kusema kwa uwazi zaid, hata hivyo vita hizi zilianza mara tu baada ya diamond paltinumz kukubali majukumu ya kuwa mtoto aliyezaliwa na Hamisa Mobeto ni wa kwake.Vita hii haijaisha na kila siku zinavyozidi ndivyo mambo mapya nayo yanazidi kuongezeka.

 

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.