Madee anyenyekea baada ya Wolper kumchambua mtandaoni

Msanii wa bongo Madee amejieleza baada ya ishu kubwa kutokea kati yake na muigizaji wa filamu za bongo Wolper.

Hii ilitokea baada ya Madee kutumia picha ya katuni inayofanana na Wolper kwenye wimbo wake mpya aliomshirikisha Tekno.

Kulingana na Wolper, Madee hakumuomba ruhusa ya kutumia picha yake na ndioi ikasababisha ishu hii.

Hata hivyo, akizungumza na Showbiz, Madee alisema, kuwa Tekno alitaka kutumia msichana mweupe na mwenye sifa tofautitofauti na ndipo Madee aliwaza na kumtumia Wolper. Lakini aliomba msamaha kwa makosa yake alisema;

“Nilikosea kumtumia Wolper kwa sababu kwanza sikumuomba. Wolper ni mshkaji nitawasiliana naye ili tuweze kulimaliza,”

 

 

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.