Grace Msalame to sue organisers of Miss Curvy Uganda for using her image

Media personality Grace Msalame might be heading to court soon after Ministry of Tourism in Uganda used her photo to promote a curvy ladies’ event.

Msalame took to Twitter to share that MissCurvyUganda2019 has used her photo to promote the pageant without her consent.

“I take great exception to the fact that my image and likeness are being used to propagate, disseminate and encourage the objectification of women’s bodies. I do not endorse or agree with such a message,” her statement read. 

Women who are blessed

The law suit comes just days after Uganda announced that it’s planning to use it’s curvy women as a tourist attraction. According to Tourism Minister Godfrey Kiwanda, the country has well endowed women and the nation plans to capitalize on that.

Grace, however, doesn’t understand why they have used her image if that’s so.

“Miss Curvy Uganda’s deliberate and calculated use of my image and likeliness to promote and encourage violation of women’s bodies has defamed my character and reputation, damaged a brand I have worked for many years to establish, and subjected me to unwarranted and undeserved cyber bullying,” she went on. 

https://twitter.com/GraceMsalame/status/1093469861026635776?ref_src=twsrc%5Etfw%7Ctwcamp%5Etweetembed%7Ctwterm%5E1093469861026635776&ref_url=https%3A%2F%2Fwww.tuko.co.ke%2F298020-tv-siren-grace-msalame-threatens-sue-organisers-miss-curvy-uganda-using-photos.html

 

Video ya mtoto wa Rayvanny na Fahyma akiwa na Diamond Platnumz

Jaydanvanny ambaye ni mtoto wa kwanza wa mkali wa Wasafi records Rayvanny na mpenzi wake Fahyma ni miongoni mwa watoto maarufu Tanzania.

Ingawa bado yeye ni mchanga, mtoto huyu akona mashabiki wengi mitandaoni na hivi karibuni alipata fursa ya kukutana na mjomba wake, Diamond Platnumz huku wengi wakitamani maisha yake.

Kwenye video hiyo, Jaydan anaonekana kutulia huku Platnumz akicheza na yeye. Tazama video hiyo hapa;

https://instagram.com/p/BYTrlHvAnDB/

Nay wa Mitego adai Diamond Platnumz na Alikiba hawamtishi, hii ndio sababu yake

Msanii wa bongo Nay wa Mitego ni mmoja wa wasanii ambao wanafanya vyema kwenye muziki. Hivi sasa anafanya vyema na wimbo wake mpya ‘Makuzi’ ambayo anaamini kuwa itafanya vizuri.

Akizungumza hivi karibuni kwenye show ya Radio One Nay alifunguka kudai kuwa yeye hana hofu kuwa wimbo wake utafanya vizuri licha ya ishu ya Diamond Platnumz na King Kiba inayowafanya wasanii wengi kutoachilia nyimbo zao kwa sababu wanahofia hazitawafikia mashabiki wao.

Nay alisema;

Watu wanaogopa kutoa nyimbo kwa sababu ya vungu vungu hili, kwangu huwa naona ni vitu ambavyo huwa vinapita haraka sana na huwa siviweki katika akili, ndio maana nikiwa na kitu changu ambacho nahisi kwa wakati huo kinatikiwa kwenda bila kuangalia kuna nini kinaendelea huwa natoa.

Aliendelea kwa kusema;

Muziki wangu una nguvu kuliko vitu vingine, mashabiki wangu ambao wanaamini kwenye kile ambacho nakifanya, so kelele za watu au purukushani za huko na kule hazinizui nikiwa na kitu changu nataka kukifanya.

Chidi Benz azungumza kuhusu ishu ya kukamatwa na dawa za kulevya

Mwanamziki Chidi Benz sasa hivi yuko huru baada ya kudaiwa kukamatwa na polisi baada ya kupatikana na madawa ya kulevya hivi karibuni.

Akizungumza na showbiz Etra ya bongo, Chidi Benz alidai kuwa kwa sasa hana ruhusa ya kuzungumzia ishu hiyo huku akisema kuwa vijana wanapaswa kuwacha kwani zikona madhara yake.

Tazama mahojiano yao hapa kwa hisani ya Showbiz.

Showbiz Extra: Sawa, na hili la wewe kukamatwa na dawa za kulevya liko vipi? Ni kiki ya kutoka na video ya wimbo au kuna ukweli upi ambao umejificha ikizingatiwa wewe umewahi kukiri mara kadhaa kuachana na dawa za kulevya?

Chid Benz: Kuhusu hilo nina ushauri kutoka kwa mama watoto wangu kwamba nisilizungumzie zaidi. Lakini kwa ufupi ni kwamba mtu kukamatwa na dawa za kulevya ni sawa na mtu aliyekamatwa na bangi, mirungi ama chochote kile ambacho kinaonekana kuvunja sheria za nchi! Kwa hiyo nisiingie huko sana lakini jambo la msingi ni kwamba vijana wa Kitanzania wasijaribu na wanaotumia dawa za kulevya waachane nazo, siyo nzuri zaidi wajenge taifa kwa manufaa ya kizazi chetu.

Vanessa Mdee aandikiwa ujumbe huu na Juma Jux

Hata baada ya kuachana na Vanessa Mdee, msanii kutoka bongo Juma Jux ameonekana kuwa bado na hisia za kumpenda mremboh huyu.

Hivi karibuni kupitia mtandao wake wa kijamii, Jux aliandika ujumbe ambao umewaacha mashabiki wakifikiria kuwa ujumbe huo ulikuwa wa Vanessa Mdee.

Aliandika kusema;

Nakumbuka mara ya mwisho kufanya party ya Birthday yangu ilikuwa 2013, Miaka minne iliyopita. Sikuwahi kufanya party yoyote tena sababu nilikuwa na rafiki, mpenzi na mtu wa karibu kuliko mtu yoyote kwenye maisha yangu. Miaka yote iliyofata nilikuwa na yeye mpaka sasa atuko tena karibu kama mwanzo, Tumebaki kuwa marafiki wa kawaida tu. Uwepo wake tu ulikuwa ni zaidi ya chochote kwenye siku yangu ya kuzaliwa, Kuongea na yeye au txt yake tu ilitosha kukamilisha siku yangu. Ila sasa sidhani kama itakuwa kama mwanzo. Nitafarijika sana kama nitamuona hiyo siku. This time nataka kuparty na watu wangu nani anataka kuparty na mimi katika siku ya birthday yangu ?

Zari adaiwa kupungua mwili Kisa na sababu, Hamisa Mobetto

Mrembo na mama watoto wa Diamond Platnumz, Zari Hassan anasemekana kuwa na mawazo mengi ambayo yamemfanya kupungua kimwili sababu ya kufikiria sana.

Habari hizi ziliwekwa wazi na chanzo kimoja kilichozungumza na Global Publisherz kueleza hali ya Zari inavyoendelea tangu Hamisa Mobetto kuweka wazi kuwa Abdul Naseeb ni mtoto wa Diamond Platnumz. Chanzo hicho kilisema;

“Zari kapungua mwili kweli jamani. Mobeto amemponza. Amemsababishia watu wamtukane sana Zari kiasi ambacho amekosa amani kabisa. Masikini mtoto wa watu kakonda kweli sasa hivi.Ukitazama picha za Zari sasa hivi si Zari yule aliyetoka kujifungua. Tena kwa kawaida tunajua mtu ukitoka kujifungua unanenepa lakini kwa Zari mambo yamekuwa tofauti. Ngoja niwatumie picha yake ya sasa muone,”

 

Hata hivyo maneno haya yanauwezekano ya kuwa ya kweli kwani kwenye picha za Sasa, Zari anaonekana kupugua mwili sana.

 

 

Zari
Zari

Juma Jux afunguka kuhusu suala la kujiunga na Wasafi Records

Jux  ambaye ni msanii mkubwa bongo anaonekana kufanya vyema na wimbo wake mpya utaniua.

Hatah ivyo akizungumza na Planet Bongo ya EA Radio msanii huyo alisema kuwa Wasafi record ni label nzuri lakini hajawahi kufikirikia kujiunga na label hiyo.

Ni kitu kizuri sio kibaya kwa sababu ile ni record label, hiyo nafasi ikipatika sio mbaya lakini kwa mimi sikuwahi kufikiria kwa hapa Tanzania au kwa Africa kwa kweli.

Hata hivyo yeye binafsi hana shida yoyote ya kujiunga na label hiyo iwapo watazingatia mkataba wake kwa sababu hafanyi muziki peke yake.

Iwe ni kampuni au sehemu ambayo itanichukua mimi kama kunimeneji pale nilipokuwa wafanye vitu extra zaidi. Sawa wanaweza ikawa wanaweza kwa mkataba kama watakuja na mkataba ambao nitautaka na vitu vyangu ambavyo navihitaji naweza nikasaini kwa sababu mimi ni mfanyabiashara lakini kwa sasa hivi hatukuwahi kuongea au kufikiria.

Aunt Ezekiel hana mipango ya kuolewa na Mose Iyobo, hii ndio Sababu yake

Muigizaji wa muvi za Kibongo Aunt Ezekiel ambaye sasa anatoka kimapenzi na Mose Iyobo hivi karibuni alifunguka kueleza mambo kadhaa kuhusu mapenzi yao huku akiwaacha wengi na maswali mingi.

Aunt Ezekiel alisema kuwa kuna wakati Mose Iyobo amemfumia na kupata meseji kutoka watu wanaomtaka na pia yeye amewahi kuzipata meseji hizo lakini anaelewa kuwa vitu kama hizo hufanyika.

Nilishawahi kumfumania mara mingi nyingi na yeye alishawahi kubamba meseji kwenye simu yangu lakini inaonesha labda mtu alikuwa ananipenda na mimi nikampotezea na ishu kama hiyo ya kufumania ni lazima itokee hasa kwa sisi tuna majina

Kuhusu swala la kuolewa, Aunt aliambia Risasi hana mipango ya kuolewa na Iyobo huku alisema:

Unajua ishu ya ndoa ni mwanaume ndiyo anaamua kuoa mtu f’lani lakini pia kufunga ndoa ni makaratasi tu kikubwa zaidi ni jinsi gani unaishi na mwenzako na mnaelewana kiasi gani.

 

Mwana FA afunguka kuhusu kumhonga mwanamke iliampende

Rapa mkali kutoka Tanzania Mwana FA ni mmoja wa wasanii wanaofanya vizuri katika muziki. Ameweza kuachia nyimbo ambazo zimevuma Afrika Mashariki.

Kwa mara ya kwanza msanii huyo alifunguka kuhusu ishu ya wanaume kuwahonga wanawaka ili wawapende. Kulingana na yeye, hajawai kumhonga mwanamke yeyote katika maisha yake.

 

Akiongea na Risasi Vibes, Mwana FA alisema;

“Nihonge ili nipate nini, sijawahi kuhonga hata siku moja najua wengi wanaweza wasiamini lakini ndiyo hivyo, tabia hizo naishia kuziona kwa washkaji zangu huku mtaani lakini kwangu hazijawahi kuwepo maana kitendo hicho nakichukulia kama biashara ya kikahaba ambayo binafsi naichukia” alisema Mwana FA

Shamsa Ford afunguka kwa nini anatamani kuokoka lakini anashindwa

Muigizaji wa filamu za Bongo Shamsa Ford kwa Sasa anatamani sana kuzifuata nyayo za Mzee Yusuf kwa kuokoka na kuacha mambo ya dunia.

Mrembo huyu anadai kuwa siku za mwisho zimekaribia na ndio maana anaonelea kubadilisha mienendo Yale. Akizungumza na Risasi Jumamosi, Shamsa alisema kuwa,

Shamsa Ford

Nimejaribu kusali sala tano kila siku. Kuna wakati ninasahau lakini kuna siku ninasali zote, ninaamini taratibu nitakuwa kama Mzee Yusuf, ninamuomba sana Mungu.

Baada ya Seduce me ya Alikiba kufikisha 2M YouTube, Christina Shusho amuandikia King Kiba ujumbe huu

King Kiba anaonekana kuwa yeye ndiye Mfalme Wa Nyimbo za bongo na hii ni baada ya msanii huyo kuachia wimbo wake mpya Seduce me ambao umefikisha milioni 2 siku tatu baada ya kuiwachia.

Mashabiki wake pia wameonekana kupenda wimbo huu ikiwemo Wema Sepetu na wengine Kama muimbaji wa nyimbo za injili, Christina Shusho. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Christina alionyesha mapemzi yake kwa wimbo huu wa King Kiba kwa kuandika;

“Leo unaweza kukuta mtu kaitwa kanisani aongoze wimbo wa sifa halafu akalianzisha Seduce Me, Eeh jamani Kiba we noma, wimbo ni mzuri sana kitaaluma kama anavyopenda kusema bosi Ruge. Hauna picha za aibu , naweza kuuangalia nikiwa na familia, labda sijui maana ya Seduce Me. Timu Kigoma Wamanyema oyeeeee. Cha mwisho Ali Kiba basi siku nyingine tutembelee kanisani ukiwa mfalme huchagui dini wote wako”

Hata hivyo kwa sasa ameweka rekodi mpya ya kuwa msanii wa kwanza Afrika Mashariki kufikisha 2 Million view YouTube na siku tatu.

Harmorapa akana kumdiss Majani kwenye wimbo wake mpya

Rappa kutoka bongo, Harmorapa ameachia nyimbo mpya itwaayo Ajitokeze hivi karibuni lakini wimbo huo umezua ngumzo mitandaoni kwani Harmorapa anasemekana kuwa alimdiss aliyekuwa meneja wake wa zamani, P Funk Majani. Kwenye wimbo huo anaskikaa kisema;

“Nishakuwa mfagizi chini ya miti, nazijua kero za majani, maana majani hayafadhiliki, ndiyo maana sipatani na majani”

Hata hivyo Harmorapa amefunguka kuhusu ishu hii na kukana kuwa wimbo huo unamlenga Majani. Harmorapa alikiri kuwa Sasa hivi Majani sio meneja wake lakini hii sio sababu ya kumdiss kwenye wimbo Kama wengi wanavyodai.

“Ni kweli kwa sasa P Funk Majani siyo meneja wangu, ila siyo kweli kwamba nimemdiss kwenye ngoma yangu, kwa sababu hatuko pamoja kikazi ila bado tuna mahusiano mazuri na hatuna ugomvi, wala hajawahi kunitimua hizo ni fununu tu. Ngoma yangu ya Ajitokeze ni ngoma inayonizungumzia mimi, kwamba hakuna anayeweza kutokea akawa kama mimi na kama yupo basi ajitokeze, ila siyo dongo kwa Majani,”

King Kiba atisha baada ya kuweka rekodi mpya YouTube

Alikiba ama ukipenda King Kiba ameweka rekodi mpya Afrika Mashariki kama msanii ambaye video yake imepata kutazamwa na watu milioni masaa 38 baada ya kuiwachia.

Seduce me imeweka rekodi ya kipekee ambayo hata wakalik ama Diamond Platnumz na Vanessa Mdee bado hawajaweza kufikisha. Kupitia ukurasa wake wa instagram, King Kiba aliweka post akiwashukuru mashabiki wake kwa kufanikisha kuvunja rekodi hiyo. Aliandika;

“Ahsanteni sana kwa upendo, nisingebarikiwa zaidi na kupendelewa bila nyinyi, nyinyi ni wa maana sana kwangu na nafanya haya kwa ajili yenu”,

kampuni ya Rockstar ambayo inamsimamia Kiba pia iliandika ujumbe kusema kuwa wimbo huu umevunja rekodi ya kipekee na ni video zinazotrend Tanzania na Kenya.

“Historia ya kunjwa rekodi imewekwa, Mfalme Kiba na wimbo wake mpya wa ‘Seduce me‘ umekuwa wa kwanza na kipee kwa msanii wa Afrika Mashariki kufikia kutazamwa mara milioni 1 kwenye Vevo/YouTube ndani ya masaa 38 tu, ina ‘trend’namba 1 Tanzania na namba 1 Kenya kwa ‘weekend’ nzima, rekodi imevunjwa.”

Aunt Ezekiel afunguka kuhusu mapenzi yake na Mose Iyobo

Muigizaji wa filamu za bongo Aunt Ezekiel hivi karibuni alifunguka kueleza mambo kadhaa kuhusu mapenzi yake na Mose Iyobo na sababu hawezi achana na yeye.

Akizungumza na Over ze Weekend ya Tanzania, mama cookie alidai kuwa yeye na Mose wanasikizana sana kwa mazungumzo na pia ndoto zao za kimaisha zinaambatana.

Mose Iyobo na Aunty Ezekiel

Tazama mahojiano yao hisani ya Over se weekend;

Over Ze Weekend: Mara nyingi mastaa huwa hawadumu na wapenzi lakini wewe na Iyobo mpaka sasa mna takribani miaka mitatu na miezi unaweza kutuambia siri ni nini?

Aunt: Kikubwa ni kuzungumza na moyo wako ulipotua ni mahali sahihi na je, unapata faraja unapokuwa hapo? Mi na Iyobo tunasikiliza sana.

Over Ze Weekend: Ni kitu gani kabisa ulikipenda kwa Iyobo?
Aunt: Unajua napenda sana mwanaume asiyekuwa na kero, asiyependa kuzungumza sana yaani kiufupi sipendi gubu, sasa kwa Iyobo vitu vyote hivyo hana.

Over Ze Weekend: Zamani ulikuwa gumzo kwa kubadilisha wanaume, mara Hatman, Silver, Joff na Jack Pemba nini kimekufanya ukaamua kutulia?

Aunt: Teknolojia sasa imekua, nimetulia na nina mtoto huyu Cookie (anamshika begani), anaweza kufungua kwenye mitandao na kumkuta mama yake ana skendo mbaya itakuwa siyo poa kabisa hivyo kila kitu kina wakati wake.

Over Ze Weekend: Unahisi kwa Iyobo umefika?

Aunt: Ndiyo, kwanza kabisa nasema hivyo kwa sababu kubwa amekuwa ni baba bora kwa mtoto wetu, mara nyingi nasikia malalamiko kwa baadhi
ya marafiki zangu kwa waume zao kutowajali watoto lakini mimi naweza kumuacha mtoto wangu na baba yake na nisiwe na wasiwasi hata kidogo.

Over Ze Weekend: Ikitokea aliyekuwa mumeo, Sunday akatokea na kuja kukuchukua kama mke wake wa zamani utafanyaje?

Aunt: Kisheria ya dini na hata kibinadamu nisingeweza kukaa muda huo ambao anatumikia kifungo na hata yeye mwenyewe alishawahi kuniambia hawezi kunilaumu kwa maamuzi yoyote ambayo ningechukua, kwa sababu hata alivyopata matatizo nilikuwa nikijaribu kuyashughulikia karibia mwaka mzima ndipo nikaendelea na mambo mengine.

Over Ze Weekend: Ulishawahi kupigwa hata kofi na Iyobo?

Aunt : Siyo kofi tu tunapigana kabisa lakini baadaye kama akigundua kama alinipiga kwa hasira basi anajirudi tunaombana msamaha na maisha yanaendelea.

Over Ze Weekend: Mara nyingi Iyobo, kazi zake ni za kusafiri na anakutana na watu mbalimbali hilo halileti shida kwenye uhusiano wenu?

Aunt: Yaah inasumbua sana mpaka kuna wakati unahisi unataka kushindwa lakini ukija hata kuangalia meseji anazotumiwa kupitia mitandaoni unagundua wazi kuwa wanampenda tu kwa sababu ni mtu f’lan.

Over Ze Weekend: Ulishawahi kumfumania Iyobo au yeye kukufumania?

Aunt: Nilishawahi kumfumania mara nyingi, na yeye alishawahi kubamba meseji kwenye simu yangu lakini inaonesha labda mtu alikuwa ananipenda na mimi nikampotezea na ishu kama hiyo ya kufumania ni lazima itokee hasa kwa sisi ambao tuna majina. Risasi: Kuna mipango ya kuolewa na Iyobo?

Aunt: Hapana.

Over Ze Weekend: Kwa nini wakati inaonekana mnapendana sana?

Aunt: Unajua ishu ya ndoa ni mwanaume ndiyo anaamua kuoa mtu f’lan lakini pia kufunga ndoa ni makaratasi tu kikubwa zaidi ni jinsi gani unaishi na mwenzako na mnaelewana kiasi gani.

Over Ze Weekend: Kwa kipindi ambacho upo na Iyobo hakuna ushawishi uliwahi kupata kutoka kwa mapedeshee mbalimbali?

Aunt: Hata kama wapo sasa hivi siwezi kurubunika kwa sababu hakuna gari ambalo sijaendesha, viwanja ambavyo sijaenda na hela gani ambayo sijashika hivyo mwisho wa siku unaona yote ni mapito tu.

Over Ze Weekend: Mna mpango wa kuongeza mtoto mwingine?

AUNT: Ndiyo, mmoja lakini siyo kwa sasa hivi.

“Hakuna mtu anayeninunulia nguo wala kunipa pesa” Agnes Masogange ataja sababu asizoogopa kuuza mwili wake

Aliyekuwa video vixen mkali kutoka Bongo Agnes Masogange amefunguka kuhusu maisha yake huku akigusia kuwa watanzania wengi wanapenda kumponda bure.

Katika mahojiano yake na Gazeti la Mwanaspoti mrembo huyu alisema Kuwa hana dhiki ikiwa atafikia kiwango cha kuuza mwili wake ili ajitafutie. Masogange alisema,

Agnes Masogange
Agnes Masogange

“Watu bana!, mimi sina dhiki ya kufikia kuuza mwili wangu eti nipate pesa na kuhusu zile picha kipindi kile nilizopiga hazikuwa za utupu sema basi tu watanzania tunapenda kuzusha sana. Na mtu kuenda Sauzi ndio ameenda kujiuza?,” Masogange aliliambia Gazeti la Mwanaspoti.

Aliongeza kuwa hakuna mtu anayemnunulia mavazi anayovaa wala kumpa pesa ya matumizi yake kwa hivyo hakuna anayeweza kumwambia chochote.

“Mimi nilikuwa na biashara zangu nafanya na wanaosema hivyo hawanisaidii chochote,hakuna mtanzania anayeninunulia nguo,hayupo anayenipa pesa waongee tu. Unajua sisi wadada tuna tabia ya kuoneana wivu akiona unafanya vizuri anaanza kukusemea vitu vya ajabu pembeni,”

Hamisa Mobetto aendelea kudai kuwa maisha yake na ya Abdul Naseeb yako mashakani

Hamisa Mobetto anaendelea kuhofia kuwa maisha yake na mtoto wake aliyezaliwa Agosti 8, mwaka huu.

Kulingana na marafiki wake wa karibu, Hamisa Mobetto anaishi na wasiwasi kutokana na vitisho anazozipata kila siku kutoka kwa baba ya mtoto wake. Chanzo kimoja kutoka familia ya Hamisa kilisema;

“Unajua baada tu ya kujifungua kulienea habari nyingi kuwa mtoto huyo ni wa msanii huyo hasa baada ya Hamisa kumpa mwanaye jina hilo. Kilichofuata, kwanza msanii huyo alikimbilia kwenye media (vyombo cha habari) kukanusha habari hizo ambazo zimekuwa zikizagaa kwa kasi ya moto wa kifuu. Unajua jamaa (msanii huyo) alidhani kuna siri chini ya jua kuwa anaweza kuficha jambo hilo maana watu walikuwa wakimchomea kwa mpenzi wake ambaye amezaa naye.

Aliendelea kusema,

“Ili kumziba mdomo Hamisa, msanii huyo aliona ni bora amkane mapema lakini Hamisa siyo wa mchezomchezo maana aligoma kuficha ishu hiyo. Baada ya kuona anaweza akabumburua ishu, msanii huyo alimpiga biti asizungumze na vyombo vya habari kabla ya kumwekea ulinzi wa chinichini kuhakikisha waandishi hawamfikii Hamisa. Sehemu pekee ambayo Hamisa aliona jamaa huyo hawezi kumzuia ni kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii hasa Instagram na Snapchat ‘so’ akawa anaposti vipande vya baadhi ya viungo vya mtoto huyo. Sasa baada ya kuona hivyo, msanii huyo ambaye alikwenda mara moja tu kumuona mtoto huyo alianza kumpigia simu na kumtumia meseji za vitisho. Wewe fikiria Hamisa na kichanga chake sasa anaishi kwa hofu maana jamaa amemuambia kama atafunguka kuwa amezaa naye atamuondoa uhai yeye na mtoto wake. Hali hiyo imeifanya family ya Mobeto iwe na hofu kubwa na ili kujiweka salama, aliona ni bora aende polisi kuripoti ili kama kutakuwa na jambo lolote baya litakalomkuta yeye na mwanaye, basi mhusika atakuwa ni msanii huyo. Mwanzoni tulidhani ni ishu ndogo lakini kwa vitisho anavyopokea Hamisa, vinamnyima raha na kumfanya alie tu.

Akaongeza kuwa…

Hamisa Mobetto na mwanae
Hamisa Mobetto na mwanae

“Kiukweli Hamisa anatia huruma sana na anahitaji msaada kwa sababu mbali na msanii huyo pia anapata vitisho kutoka kwa mpenzi wa jamaa huyo. Sasa watu wanajiuliza, wakati anatembea naye hakujua kuwa kinaweza kupatikana kiumbe? Na kwa ustaa wake anashindwa nini kulihendo suala hilo kwa busara ili lisimchafulie kuliko kutoa vitisho hivyo?” kilifunguka chanzo chetu hicho na kuongeza. Hata kwenye ukurasa wake wa Snapchat, Hamisa ameshatahadharisha juu ya kutishiwa kuuawa yeye na mwanaye.”
Baada ya kunyetishiwa ubuyu huo, Ijumaa liliperuzi kwenye ukurasa wake huo na kukutana na ujumbe wa Hamisa uliosomeka:
“Mlidhani atafia tumboni enh…au mlijua nitafia leba…. nyie siyo Mungu na hamtakaa kuwa kamwe…& if anything bad and I mean anything bad happens to me or my son hatutawaacha salama!!!”

 

Hamisa na yeye aka sema;

‘MIMI NA MWANANGU TUNAUAWA WAKATI WOWOTE’ Ni kweli mimi na mwanangu tunauawa muda wowote. Nina ushahidi wa kutosha wa vitisho so nimeona ni vyema nitoe taarifa kwenye vyombo vya usalama,”

Alikiba awachia video mpya – seduce me

King Kiba ameachia video ya wimbo wake mpya Seduce me hivi leo miezi kadhaa baada ya kukawia kimya.

Msanii huyo amewachia wimbo huo wakati kuna tetesi kadhaa za kuchambuliwa na Diamond Platnumz kwenye mix ya Fresh.

Wimbo huu umewaacha mashabiki wake kama wameridhika baada ya kusubiriwa kwa hamu. Wimbo huu umetengezwa chini ya kampuni ya Rockstar4000 Music Entertainment and Rockstar Television inayommiliki.

Itazame hapa

 

 

 

Expect more drama! Hessy Wa Dandora issues out a warning to those planning to attend the late GAZA gang leader’s funeral

Funeral plans of the late Mwanii/mwane said to be the ring leader of GAZA gang (a dangerous group of thieves) was shot dead a few days ago and the police are not done with him yet.

From the reports making rounds on several blogs, Mwanii is said to have been killed along side a fellow colleague and the two did not die before trying to put up a fight.

Apparently despite being asked to surrender Mwanii and Collins exchanged a few shots with the police who had learnt that they were living in Witethie Estate in Ruiru which is located along Thika road.

Anyway, Hessy has however issued a warning through his Facebook page saying that those who will be present might experience some drama as the police will be present to attain back their missing AK47 which is missing;

Kwa wale mtaenda mazishi ya huyu Jamaa, nataka mjue yafwtayo: (For those attending Mwangi’s burial, here are a few things you should know)

1. His group is still in possession of another AK47 rifle plus other pistols, and the government is seriously in search of its properties: that means we will be there to see if we can get back our properties

2. No burial permit will be issued to the family, so it’s a clear indication that it is also illegal to bury him. So for those ones willing to attend his burial, expect more drama, ‘own goals’ inclusive. U know it’s always gud to speak the truth!!!!

 

Idris Sultan na Wema Sepetu waendelea kuwatumbuiza mashabiki wao, wanataka kurudiana? (Picha)

Wema Sepetu ambaye ni Tanzania sweetheart na mwanamke maarufu Afrika Mashariki ameonekana kuonyesha uwezekano kuwa bado mapenzi yake kwa Idris Sultan bado yako.

Hii ni baada wawili hao kuonekana mtandaoni wa Instagram wakiongea kwenye comment section. Hata hivyo wawili hao huwa wakitaniana na kulingana na maoni ya mashibiki wao, wawili hawa wanaweza kurudiana.

Kwa sasa hakuna anayejua mpenzi wa Wema Sepetu ama Idris Sultan lakini wengi wanapaswa kuridiana kwa sababu mapenzi yao hayafichiki. Tazama baadhi ya comments zao hapa chini;

Bado hali ya Mzee Majuto haijabadilika, adai kuwa anaumwa

Mchekeshaji kutoka Bongo anayetambulika kama King Majuto bado hajapata nafuu hata baada ya kufanyika upasuaji kutokana na tatizo la ugonjwa wa ngiri (hernia).

Hali yake bado haijabadilika kulingana na alichosema baada ya wanahabari kuzungumza naye hivi karibuni. Mzee majuto alisema kuwa bado anahitaji muda mwingi kulala, iliaweze kusikia nafuu.

Baada ya Global publisherz kuzungumza naye, Mzee Majuto alisema:

“Bado nimelala jamani na sijui unataka nini tena? Naumwa na ninasikia maumivu sana na sitaki kuzungumza zaidi maana nimechoka, elewa tu kwamba bado naumwa na ningependa sana uniache ili nipate muda mwingi wa kupumzika, ni kweli hivi karibuni nilipata nafuu kabisa na kuanza kutembea lakini ndiyo hivyo bwana, bado hali haijakaa sawa,”

“Gombaneni, roganeni mpaka muuane” Huu ndio ujumbe Nay aliowaandikia Ommy Dimpoz, King Kiba na Diamond Platnumz

Rapa wa bongo Nay wa Mitego hatimaye ameingilia vita mpya ya Ommy Dimpoz, Diamond Platnumz na King Kiba kwa kutoa maoni yake.

Kupitia mtandao wa Instagram Nay alifunguka kwa kusema kuwa hakuna anayemuunga mkono lakini jambo linalomkasirisha ni kuwahusisha wazazi kwenye vita hivi vyao vya utoto. Aliandika kusema;

Gombaneni, roganeni mpaka muuane, napenda kusikia changamoto kwenye gemu, ila tusiwaingize wazazi wetu tafadhali, tukananeni matusi yote wenyewe kwa wenyewe ikibidi piganeni kabisa atakaye kufa tutazika na itakuwa historia kama Big na Pac.

Akaendelea kwa kuongeza kuwa;

“Ila kuwaingiza wazazi ni ujinga, sipo upande wowote si kwa Kiba, Dimpoz wala Diamond, endeleeni na vita yenu kama wanawake mmechukuliana mabwana, ila suala la wazazi mnavuka mipaka,”

Rosa Ree afunguka sababu za kuvalia mavazi ya nusu utupu

Msanii wa hip hop bongo ni mmoja wa wasanii wa kike ambao hupenda kuvalia mavazi yanaonyesha mwili wake.

Sio kwa sababu anajaribu kuuza nyimbo zake, lakini ni kwa sababu anapenda kuvalia nguo kama hizo.

Akizungumza kwenye mahojiano Rosa Ree’ amefunguka kusema;

“Navaa mavazi ya nusu utupu kwa sababu napenda, mimi ni mwanamuziki,  lazima nivae tofauti na watu wa kawaida, kwa hiyo wanataka hata nikienda kuoga nivae suruali? Acha waseme, ninaziba masikio mimi naangalia muziki wangu tu,” alisema.

Aunt Ezekiel aeleza sababu hatoweza kumrudia mwanaume aliyemuoa miaka 4 zilizopita

Baada ya mpenzi wa Aunt Ezekiel wa kitambo Sunday Demonte kurejelea Tanzania kutoka Dubai baada ya kutumikia kifungo cha miaka kadhaa, Aunt Ezekiel amesema kuwa hawezi mrudia mwanaume huyu.

Aunty Ezekiel

Akizungumza kwenye mahojiano na Risasi Mchanganyiko Aunt Ezekiel alisema;

“Ngoja niulize, hivi jamani mbona watu siyo waelewa? Nani asiyejua kama mimi niko na mtu hivi sasa? Na ninaamini kabisa hata yeye (Demonte) anajua? Kwa hiyo hata kama ameachiwa huru na akaja, ukweli utabaki kuwa ndiyo huohuo tu, kwamba tayari nina mtu mwingine maana hata yeye asingeweza kusubiri muda wote huo, hivyo ajue tu hana chake,”

Aliendelea kuongeza kuwa Sasa hivi hawezi kumuacha Mose Iyobo kwa sababu wakona mtoto na maisha yake yamesonga.

Staa huyo aliongeza kuwa, kwa hivi sasa ni vigumu kuachana na mzazi mwenziye aliyenaye kwa kuwa tayari wana mtoto ambaye anapenda kuwaona wakiwa pamoja, hivyo hawezi kumuacha Mose Iyobo. Aunt alisema;

“Hebu fikiria, mtoto wangu amezoea kutuona pamoja mimi na baba yake na ni kitu ambacho anakipenda sana, sasa kwa nini nimuumize?”

 

Ommy Dimpoz amuandikia Barua mamake Diamond Platnumz

Wengi wanapodhania kuwa Ommy Dimpoz ameamua kukaa kimwa – basi msanii huyu wa bongo hivi leo amewaacha wengi wameshtuka baada ya kumuandikia bi Sandra barua kupitia mtandao wa Instagram.

Ommy aliweka picha yake na ya mama Diamond hukua kiandika;

BARUA YA WAZI KWA BINTI YANGU MALKIA WA NGUVU

Salam zako nimezipata mwanagu hivi kweli ww wa kukosa adabu kuamua kunichamba baba yako? Sasa Kosa langu mimi nini????kwani kuna ubaya kumtandikia kitanda Baby wako king?
#unanioneakwakuasijuikurap?
#sijuiNamiminimkatae
#kamayeyealivyokataawaMobeto
#Yaniunamkataamjukuuwangu
#unakubalikuleawatotowa5siowako
#umerogwawwsioburemwanangu
#NilikuwanajuanimezaaSIMBA
#kumbenimezaaKIMBA
#DavidonaeanalalamikuhusuENEKA
#UmeletaJanjaJanjakwenyefallonu
#utakujakuniuakwapreshajomonii
#Nnaedhalilikamimibabayako
#hayanendakatungevesinyingine
#Rahayavitausichanguesilaha
#BABAMALKIA

Tazama post yake hapa;

Msanii maarufu wa bongo aweka picha ambayo imezua utata mitandoni kusheherekea siku ya kuzaliwa ya Rayvanny

Diamond Platnumz amekuwa mada ya wiki huu baada ya Hamisa Mobetto kufunua jina la mtoto wake, Abdul Naseeb.

Kwa kufanya hivi, Diamond Platnumz alimbumburushia Mobetto matusi huku akimuita ‘bitch’ na kuwafanya mashabiki wake kumponda kwa kitendo hiki.

Hata hivyo, Diamond Platnumz ameonekana kuendelea kumponda Hamisa kwa kumuwekea picha za kuudhi mitandaoni. Akimsheherekea Rayvanny Leo, Mkali huyo wa Wasafi aliweka picha huku akionekana akimbusu Zari na Vanny akioneka kwenye background.

Kwenye picha hiyo, Simba aliandika;

Jus wanted to wish the guy at the back happy birthday…please tag him!!!

Lakini, mashabiki wake wameonyesha kutoridhika.

“Nitakupa style zote” huu ndio ujumbe aliouandika mke wa Roma

Msanii wa bongo Roma sasa hivi anaonekana kufanya vizuri na wimbo wake mpya aliouachia mwezi Agosti 10th.

Baada ya kuweka wimbo huo YouTube mke wa msanii huyo, Nancy, alitoa ahadi ambayo iliwaacha wengi wameshtuka mitandaoni.

Kulingana na Nancy, video ‘Zimbabwe’ mpya ya mumewe ikipata kufikisha views milioni moja angempa style zote.

Sasa, video hiyo Jana, August 20, 2017 video ya hiyo ilifikisha views milioni katika mtandao wa YouTube tangu ilipoweka. Na kama awali, Nacy kupitia mtandao wa Instagram aliandika;

Finally You Made It #1Milion_Views Ndani ya Week 1 Na siku 3!!! Walahi Mume wangu @roma_zimbabwe#LEO_NITAKUPA_STYLE_ZOTE Kwa Furaha Niliyonayo!!! Hongera Mno!! Much Congrat kwa shemela @nicklassm Nakuona Mbali Saaana!!

 

Fid Q amshirikisha Diamond Platnumz na Rayvanny kwenye mix ya ‘Fresh’ na mashabiki wadai wamemchana Hamisa Mobetto

Fid Q ambaye ni msanii wa muziki wa hip hip Bongo sasa hivi ameachia remix wa wimbo Fresh ambapo ameliwashirikisha Diamond na Rayvanny.

Katika wimbo huu Diamond Platnumz anasikika akirap na kulingana na mashabiki, mwanamuziki huyu anawachambua Kiba na Hamisa Mobetto kwenye maneno aliyotumia.

Rayvanny naye alipewa nafasi ya kuimba chorus na kama kawaida, msanii huyu aliweza kuipa nyimbo hii fleva.

Isikize nyimbo hii hapa;

 

 

 

Uwoya aeleza sababu za muvi za bongo kupotea sokoni

Uwoya ambaye ni mmoja wa waigizaji maarufu Bongo hivi karibuni alifunguka kueleza sababu za soko la muvi za kibongo kwenda chini.

Uwoya
Uwoya

Akizungumza na Global Publisherz, muigizaji huyo alisema kuwa kuna changamoto kadhaa ambazo zimechangia huku akiwalaumu wasambazaji wa muvi za kibongo wanazoziuza muvi hizi kwa bei ya chini.

Tazama mahojiano yake na Global Publisherz hapa;

Swali: Labda mimi siyo mfuatiliaji sana, lakini naona kama filamu zimesimama hivi au?

Uwoya: Zimesimama unamaanisha nini? Yaani hazizalishwi tena au?

Swali: Ninamaanisha haziko kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma, filamu zilikuwa nyingi sokoni na watu wakizigombea, sasa hivi sizioni.

Uwoya: Ni kweli, sasa hivi wasanii wamepunguza kutengeneza kazi mpya, sababu kubwa ni soko, limekuwa gumu sana.

Swali: Limekuwa gumu kivipi?

Uwoya: Hapa pana changamoto nyingi, kwanza kwa wasambazaji wenyewe na pia kwa wanunuzi. Kwa upande wa usambazaji, wananunua kazi kwa bei ambayo inatuumiza na mara nyingi tunakuwa hatuna jinsi, ni bora tufanye kazi tuonekane kuliko kukaa tu nyumbani.

Swali: Huoni kuwa ubora duni wa kazi zenu ulichangia kwa wasambazaji kununua kwa bei ndogo?

Uwoya: Wakati mwingine uduni wa kazi unatokana na haohao wasambazaji ambao wana bei zao.

 

TID akana kumpachika Recho mimba

Msanii wa Bongo TID anasemakana kuwa alimpachika msanii mwenzake Recho mimba lakini kulingana na mkongwe huyu wa muziki, amekana tetesi hizi.

Recho

TID akizungumza na kipindi cha Enewz cha EATV alisema kuwa hatarajii mtoto yeyote na Recho huku akiendelea kusemak kuwa kila mtu anataka kuwa na mimba yake. Alisema;

“Hapana, sitarajii mtoto yeyote na Rachel, sina mimba ya Recho, siyo kweli bwana, hamna mtu mwenye mimba wala nini. Kila mtu anataka kuwa na mimba ya Mnyama, sasa wanawake wangapi wanataka kuwa na ujauzito wa mtoto wangu?”,

Hata hivyo hivi karibuni wawili hao walisemekana kuwa ni wapenzi.

Tazama picha kutoka sherehe ya Romy Jons

Romy Jons ambaye anatambulika kama ndugu mkubwa wa Diamond Platnumz – wikendi hii August 18, 2017 alifanya birthday kubwa huku akivutia wasaniii wengi kusheherekea na yeye.

Waliohudhuria ni wasanii wa WCB, Babu Tale, Vanessa Mdee na wasanii wengine kumpa pongezi Romy kwa kuongeza mwaka Mwingine maishani mwaka.

Kupitia mtandao wa instagram Romy aliwashukuru wote waliohudhuria party hiyo, kwa kuandika

“thanks for everyone who showed up last night…shukran sana kwa kila aliyejitokeza jana!najisikiaga faraja sana kusherehekeaga siku yangu ya kuzaliwa na watu wangu wa karibu na wasiokua wakaribu pia!!!!,”

Tazama picha hizo hapa;

Madee anyenyekea baada ya Wolper kumchambua mtandaoni

Msanii wa bongo Madee amejieleza baada ya ishu kubwa kutokea kati yake na muigizaji wa filamu za bongo Wolper.

Hii ilitokea baada ya Madee kutumia picha ya katuni inayofanana na Wolper kwenye wimbo wake mpya aliomshirikisha Tekno.

Kulingana na Wolper, Madee hakumuomba ruhusa ya kutumia picha yake na ndioi ikasababisha ishu hii.

Hata hivyo, akizungumza na Showbiz, Madee alisema, kuwa Tekno alitaka kutumia msichana mweupe na mwenye sifa tofautitofauti na ndipo Madee aliwaza na kumtumia Wolper. Lakini aliomba msamaha kwa makosa yake alisema;

“Nilikosea kumtumia Wolper kwa sababu kwanza sikumuomba. Wolper ni mshkaji nitawasiliana naye ili tuweze kulimaliza,”

 

 

Mr Nice aeleza kwanini anahisi Wakenya wanamtambua kushinda Watanzania

Lucas Mkena anayetambulika kama Mr Nice amefunguka mara ya kwanza kueleza sababu zake za kupiga show Kenya sana kushinda Tanzania.

Akizungumza na Showbiz ya Tanzania, Mr Nice alifunguka kusema mengi ambayo nimeambanisha hapa courtesy ya Global Publishers.

Isome hapa chini;

Showbiz: Mashabiki Bongo walikumisi kwa muda mrefu wangependa kujua ulikuwa wapi na unafanya nini kwa sasa?

Mr Nice: Maisha yangu kwa sasa yapo Kenya, huko nina zaidi ya miaka mitatu nikifanya muziki wangu, nimeamua kuhamishia makazi huko kwa sababu kule wenzetu mambo ya burudani wako mbali sana hivyo kazi zinapatikana kwa wingi tofauti na Bongo.

Showbiz: Vipi kuhusu mazingira ya huko hayakukupa shida? Mr Nice: Hapana halafu unajua maisha yangu ya muziki yamekuwa ya kwenda hapa na pale nchi mbalimbali hivyo hiyo haikunisumbua. Showbiz: Unazungumziaje habari zilizokuwa zikizagaa kuhusu kifo chako?

Mr Nice: Ni chuki tu za baadhi ya Watanzania wenzangu na ninashindwa kuelewa kwa nini wananichukia kiasi hiki wakati nchi nyingine wananiona lulu? Kwa nini wananifanyia hivyo wakati Kenya naishi kama mfalme maana hata nikiambiwa nije kufanya shoo Tanzania, najifikiria mara mbili mbili kwa sababu naona watu wangu wamenitenga.

Showbiz: Kuna siku ulikuwa ukiimba wimbo wako wa Mama huku ukibubujikwa na machozi na kusema unaumia watu wanasema una ugonjwa wa Ukimwi, unazungumziaje hilo?

Mr Nice: Ni kweli watu walinipakazia hivyo na wimbo ule wa Mama unaniliza kwa sababu najua mama yangu angekuwepo angewakemea waache kuzungumza maneno hayo maana mastaa wenye mama zao wakisakamwa tu, mama zao wanaibuka kukanusha.

Showbiz: Kwa nini unasema baadhi ya Watanzania wanakuchukia?

Mr Nice: Kwa sababu wamekuwa ni watu wa kunidharau, kunidhihaki kwa sababu heshima ambayo ningeipata hapa nyumbani naenda kuipata nchi nyingine.

Showbiz: Mashabiki wako wangependa kufahamu huko Kenya upo na familia yako?

Mr Nice: Kenya, nafanya kazi tu, familia yangu yote ipo Tanzania, lakini sijaoa na wala sitegemei kufanya hivyo kwa sababu tayari nina watoto wawili ambao nataka kuwalea bila karaha ya mama wa kambo.

Showbiz: Najua muigizaji Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ huko nyuma alikuwa ni mpenzi wako vipi unazungumziaje kuhusu matatizo yaliompata?

Mr Nice: Namuombea ila kwa upande wa Watanzania, waache kushabikia mtu anapopatwa na janga na kuanguka. Wamuombee na waache manenomaneno.

Showbiz: Ni faida gani umeipata mpaka sasa kutokana na muziki?

Mr Nice: Nyingi sana, kwanza nina mijengo ya maana minne, nina usafiri wangu na nina mashamba kutokana na muziki huohuo na miradi yangu mingine mingi.

Diamond Platnumz amchana Hamisa Mobetto baada ya mrembo huyo kumpa mwanae jina “Abdul Naseeb”

Hamisa  Mobetto ameonekana kutojali watakacho sema watu na kumpa mwanae wa siku kumi sasa jina la ‘Abdul Naseeb’ ambalo likedhibitisha kuwa ni mtoto wa muimbaji, Diamond Platnumz.

Mrembo huyo ambaye alitokea kwenye nyimbo ya Salome Hata hivyo hajafunguka kuelezea sababu zake lakini, jana usiku Diamond Platnumz anasemekana kuwa alimchana kwa kuandika;

Hata hivyo Hamisa Mobetto hakujibu kwani Diamond Platnumz hakumtaja mtu yeyote kwa jina. Mashabiki nao kwa sasa wanachochea kusikia atakachosema Hamisa.

Mume wa Aunt Ezekiel arejea Dar baada ya kutumikia kifungo chake Dubai

Aliyekuwa mume wa Aunt Ezekiel anasemekana kurujea Dar baada ya kukawia Dubai alikokuwa akitumikia kifungo chake kutokana na kuishi kinyume cha sheria huko Dubai.

Aunt Ezekiel

Habari hizi zilienezwa na Chanzo kilichodhibitisha kuwa Sunday Demonte yuko Tanzania. Hata hivyo Risasi Mchanganyiko ilizungumza na mdogo wa Demonte, ambaye alisema;

“Sunday mbona ameshatoka kitambo, yupo zake uraiani kwa raha zake, ni mwaka huuhuu ametoka japo sikumbuki ulikuwa mwezi wa ngapi maana sikuwepo, kwa sasa yupo hapa Dar, hayupo Dubai, ukitaka kujua mengi ni vizuri nikuunganishe naye mwenyewe ukamuhoji,” alisema.

Mose Iyobo na Aunty Ezekiel

Hata  hivyo bado wengi wanangoja kusikia atakachosema Aunt Ezekiel ambaye sasa anatoka kimapenzi na dancer wa Wasafi records, Mose Iyobo.

Ruby afunguka sababu za kutemana na Soudy Brown wa Clouds FM

Mrembo na msanii wa bongo Ruby amefunguka kwa mara ya kwanza kudai kuwa hapo awali alitoka kimapenzi na mtangazaji wa Clouds FM, Soudy Brown kwa miaka miwili lakini wakaachana.

Kulingana na Ruby aliwachana na Soudy Brown kwa kuwa mtangazaji huyo hakuwa na msimamo. Akiongea kwenye mahojiano Ruby alisema;

“Nikisema nitoke na mastaa wenzangu sio kwamba hawanisumbui wananisumbua sana lakini nawajua tayari the way walivyo. Lakini vitu vingi ambavyo naona wanafanyiwa wasanii wenzangu na mimi kweli nikawe na msanii?

Aliongeza kusema;

”Hapana siwasemi kwa sifa mbaya wasanii lakini mimi siwezi kuisha nao kutokana na tabia zao kwa sababu mimi ni mwepesi sana kuumia. Mimi mwanaume ambaye nimetoka naye kwenye mapenzi na yupo kwenye industry yetu only ni Soudy Brown, na nimeishi naye kwa mwaka mmoja na miezi sita,”

Kuhusu mimba aliyokuwa anasemekana amebeba – Ruby alikana kwa kusema kuwa hajawai kutoa mimba.

 

Hamisa Mobetto ampa mtoto wake jina Kiowa, Abdul Naseeb

Hamisa Mobetto ambaye ni video vixen na model amewaacha wengi wakijiuliza maswali baada ya kumpa mtoto wake jina la Abdul Naseeb. Jina hili limezua maswali mengi huku wengi wakidai kuwa hii ni dhibitisho tosha kuwa ni mtoto wa Diamond Platnumz.

Abdul Naseeb ambaye alizaliwa Agosti 8 mwaka huu amekuwa akifichwa na Hamisa Mobetto ambaye bado anangoja kuonyesha sura ya baby Dully Dee.

Kwa sasa Hamisa Mobetto amebadilisha jina la akaunti ya Instagram kutoka ‘Tanzania Baby’ na kuandika ‘Abdul Naseeb’. Hata hivyo bado tunangoja kusikia atakocho sema Diamond Platnumz kwa sababu mama yake (mama Diamond) wiki iliyopita aliambia Shalawadu Clouds TV walionekana katika hospitali ambayo alijifungilia mrembo huyo.

Mkali wa Wasafi records aachia video mpya ‘Dede’ inayowapa wasanii wenzake wasiwasi kutokana na ubunifu wake

Lava Lava kutoka label ya WCB hatimaye ameachia video ya wimbo wake mpya ‘Dede’ miezi kadhaa baada ya kuachia video yake ya kwanza katika uongozi wa rekodi ya Wasafi, ‘Tuachane’.

Ingawa video yake haina tofauti mingi na Tuachane, nyimbo hii yake imewavutia wengi ambao wanafurahishwa na maudhui aliyotumia kwa lyrics ya Dede.

Video hiyo pia imepata maoni tofauti kutoka kwa mashabiki wake. Hata hivyo itazame hapa na utoe maoni yako.

Chidi Benz akamatwa baada ya kunaswa na Heroine

Chidi Benz ambaye alikuwa ameachia wimbo mpya unaofahamika Kama ‘Muda’ aliyomshirikisha Q Chillah amjipata mashakani baada ya kupatikana na dawa za kulevya aina ya heroine.

Kulingana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni alifunguka kusema kuwa Chid Benz alipatikana baada ya msako na mkali uliofanyika August 12 jioni.

“Chid Benz na wenzake wapo kituo cha Polisi cha msimbazi ambapo tunaendelea na upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani na kiasi cha dawa zilizokamatwa zimepelekwa kwa mkemia mkuu na itajulikana ni kiasi gani za dawa za kulevya zilizokamatwa,”

Chid Benz ambaye ambaye alikuwa anaonekana kubadilika amewashtua wengi kwani hii sio mara yake ya kwanza kupatikana na Sawa za kulevya.

Shilole apata majibu kutoka kwa Dayna

Hapo awali kabla ya kuachia wimbo wake mpya Kigori alifunguka kudai kuwa sababu yake ya kukawia kabla kuachia wimbo mpya ni kwa sababu alikuwa amewapa wasanii wa kike muda kufanyap projects ambazo ni kali kushinda zake lakini, hakuna aliyeweza kumfikia.

Hata hivyo msanii Dayna Nyange amezungumza na E-Newz ya EATV ambapo alijibu ripoti ya Shilole kwa kusema;

“Mimi nafikiri yeye ndio anaweza kuwa majibu yote kwamba kwa nini amekuja kuchukua game yake, labda alikuwa kimya kwa muda mrefu akawa anaona bado nafasi yake ipo. Unajua kila mmoja ana riziki yake kwenye hizi kazi usitengemee kwamba Dayna atakuja kufanya kitu fulani nimpoteze mtu fulani, hapana kila mta na riziki yake na kila mja na wakati wake,”

Akaongeza kwa kusema;

“I think ni wakati wake kama alifanya kitu fulani akaona mafanikio yake lakini akaona huku bado kulikuwa na mafanikio yake au anahitaji zaidi, so ana haki ya kufanya, kusema anachuku game ni misamiti tu ya lugha zetu za kisanii,”

Picha mpya za Vee Money za wazingua mashabiki, Ni kweli kuwa amenenepa? (Picha)

Msanii na mrembo wa bongo Vanesaa Mdee ameachia picha mpya usiku wa kuamkia leo huku akionekana kuwa ameongeza weight katika sehemu ambazo mtu hawawezi kosa kujua.

Vanessa aliwachia picha hizi kupitia mtandaow ake wa Instagram huku akizingua akina idris Sultan na mashabiki wake ambao huwa mkondo wa kwanza kujua anachofanya mkali huyu.

Picha hizi hata hivyo sio siri kuwa ni za kuvutia na nguo yake ya manjano na viatu vyake vya chini.

Rayvanny awachia picha mpya akiwa na mwanae

Msanii wa Wasafi records Rayvanny amewafurahisha wengi baada ya kuachia picha mpya akiwa na mwanae, Jaydanvanny katika mtandao wake wa Instagram.

Picha hii ameiwachia wiki kadhaa baada ya msanii huyu kumueka mtoto wake mitandaoni yake ya kijamii. Hata hivyo iliwavutia wengi hata Diamond Platnumz ambaye alimsifia kwa kuwa yeye ni baba kwa Sasa.

Rayvanny na mpenzi wake Fahyma walibarikiwa na mtoto huyu miezi kadhaai iliyopita na ukilinganisha picha hii na zile za awali;

Zari awapa maneno wanaodai kuwa Nillan sio mtoto wa Diamond Platnumz (Picha)

Zari Hassan ameonekana kukasirishwa na watu wanaodai kuwa Nillan sio mtoto wa Diamond kwa kuweka picha huku wakimfananisha na marehemu Ivan Ssemwanga ambaye alikuwa bwana yake kabla kutemana.

Kupitia mitandao yake ya kijamii, Zari aliwapasha watu hawa kwa maneno makali huku akisema kuwa Nillan ni 5star. Aliendelea kwa kuwakomesha kutoa jina la mtoto wake kwenye vinywa vyao.

Mrembo huyu pia aliongeza kwa kusema kuwa yuko busy na iwapo wataendelea atawapa vouchers za bure za vodacom ili waendelee kuongea.

Tazama picha hizi hapa;

Barnaba amjibu aliyekuwa mke wake kupitia ujumbe huu wa Instagram?

Barnaba na aliyekuwa mke wake wameonekana kupashana kupitia mitndao yao ya Instagram. Hii ni baada ya mrembo huyo aliyekuwa mke wake ambaye pia ni mzazi mwenziye, kuposti picha akiwa na mpenzi wake wa sasa mitandaoni huku akiandika ujumbe unaoelezea sababu za ndoa yao kuvunjika.

Hata hivyo Barnaba naye aliandika ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram huku akiwasifia wanawake – lakini mashabiki wake wanaonelea kuwa alikuwa anamjibu mke wake.

Alindika kusema;

“Mama aliniambia ukimtukana mwanamke basi umenitukana na mimi, siku zote nawaona kama mama zangu, hongera wanawake wote duniani, salamu zangu juu yenu Jumapili ya leo nawapenda sana, na wale mliopoteza mama zenu fanyeni ibada juu yao waweze punguziwa adhabu ya kifo au kufutiwa kabisa, Bwana Yesu asifiwe sana Jumapili ya Mungu tumpe Mungu Wakristo wenzangu”

Hii ndio sababu Faiza Alley anasema kuwa wasanii wa Tanzania hawana ubunifu

Faiza Ally ambaye ni mama ya watoto wawili hivi karibuni aliwachana wasanii wa Tanzaniak kwa kudai kuwa hawana ubunifu wowote wa kutafuta Kiki.

Mrembo huyu aliandika haya kupitia Instagram account alisema;

Faiza Alley

“Nilichogundua sasa hivi kutokana na kipindi ninachosikilizaga redioni ni kwamba wasanii Watanzania hawana akili za ubunifu katika kutafuta kiki, zaidi ya wanaume kutoka na wanawake maarufu na wanawake maarufu zaidi ya kutoka na wanaume maarufu.”

Akamalizia kwa kusema;

“Unapokuwa msanii kiki ni moja ya kazi lakini jaribu kuwa mbunifu kidogo zaidi ya uroda! Sema naomba mnisamehe ni ile uhuru wa kuongea tu sijamlenga mtu lakini najua kuna mstari wa kujifunza”

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.