Kazi za Diamond Zinajiuza Zenyewe-Meneja wa Diamond UK

Meneja wa msanii Diamond Platinumz alijitambulisha kwa jina moja tu la Dullah amefunguka na kusema kuwa kwake yeye kufanya kazi na Diamond hakumpi shida yoyote kwa sababu jina lake tu limekuwa likijiuza na kwa sababu mwanamuziki huyo ni mchapakazi.

Dullah ambae alikuwa nchini kenya kwa ajili ya uzinduzi wa album ya diamond akipokea mwaliko special kutoka kwa msanii huyo akiwa kama meneja wake amefika kwa ajili ya kufanikisha na kuhudhuria tukio hilo kubwa la kimuziki alilokuwa akifanya msanii wake.

Nimekuja hapa kwa ajili ya uzinduzi wa album yake ya a boy from tandale mimi ni special guest kutoka kwake mwenyewe,nakubali sana azi za diamond kwa sababu ni mtu anaejituma na mimi mwenyewe nina jituma . tulikubaliana tanfu day one kufanya kazi pamoja kwa kuwa aliamini kuwa mimi akinipa kitu chake nina weza kukisimamia.

sifanyi kazi za mtu mwingine kwa zaidi ya zile za diamond, kazi zake zinajiuza zenyewe yaani ukisema diamond unasikia jina tu,kwaio upati shida ya kutafuta show zake , au kumuuza kwakwli its easy to work with Diamond.

Dullah anasema kuwa yeye kwa sasa amekuwa kama kaka mlezi wa wasanii wote wa WCB, na anawashukuru sana wasanii hao kwa sababu wamekuwa wanamsapoti sana yeye na ndio maana hata yeye pia anakuwa na moyo wa kuwasapoti.

Lakini pia menejea huyo anasema kuwa kwake yeye diamond sio mfanyakazi tu bali ni kama familia , hivyo ataendelea kuwasapoti na kufanya nao kazi pamoja kwa kila hali wakiwa chini ya uongoz wa Babu Tale na Sallam K

Kitu kingine anachonivulia dulaah kufanya kazi na diamond ni pale ambapo amekuwa ni msanii wa kusikiliza maoni ya watu wa pembeni, lakini pia wasanii wengi wamezoea kuona msanii anaandaliwa kila kitu kwene show lakini kwa upande wa diamond ni msanii ambae mtakaa na kushirikiana nae kufanya maandalizi kuanzia day one mpaka show inaisha anakuwa pamoja na watu wake karibu.

 

Kivazi cha Kitenge Kilivyotawala Party ya WCB( +Picha)

Wikiendi hii ilikuwa ni party ya wasanii kutoka WCB wakimkaribisha rasmi msanii mwenzao aliyekuwa katika kundi la ya moto band kabla band hiyo  haijavunjika Maromboso.Mboso amekaribishwa na kutambulisha wimbo wake mpya alioanza kuufanyia kazi akiwa WCB.wasanii wa lebel hiyo walitoka kipekee kwa kuhamua kutupia kivazi cha kitenge kama inavyoonekana.

Diamond akiwa na Maromboso katika kivazi cha kitenge.

Rayvanny na Fayma (mama mtoto wake) katika kivazi cha kitenge.

Esma Platinumz na mume wake Petit wakiwa katika pozi kuelekea katika party ya WCB.

Harmonize na mzungu wake wakiingia ukmbini na baadhi ya wageni katika kivazi cha kitenge.

Rommy Jonns akiwa ametupia suruali ya kitenge na kikofia kwa juu.

Queen Darleen akiwa amevaaa kigauni chenye nakshi ya kitenge pembeni.

Mama Diamond na baadhi ya wageni katika muonekano wa kitenge halisi.

Mrembo Tunda katika muonekano wa kitenge nae alikuwepo.

 

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.