Marioo brings Maua Sama on board for ‘Corona’ (Video)

Bongo star Marioo has linked up with his countrymate Maua Sama to sensitize the public about Coronavirus that has killed more than 11,000 people worldwide so far.

Also read: Kenyan musicians have so much to learn from their Tanzanian counterparts

In the song titled Corona, the musicians asks people to be careful so that they do not contract the deadly virus which kills within a few days, especially when one’s immunity is low.

Maua Sama

The musicians urge people to take the disease seriously and adhere to the rules and regulations that have been put in place by the government to protect them.

They include; thoroughly washing your hands using clean water and sanitizing, avoiding large crowds and travelling  from one place to the other, educating others about the virus and seeking help when you have symptoms.

They say that the only way we can stop Coronavirus from spreading is by protecting one another and being cautious when we are in public.

Marioo
Marioo

Other than the powerful message that it carries, I’m sure after listening to Corona, you’ll agree with me that it’s such a beautiful composition.

If you are a fan of both Marioo and Maua Sama, like I am, then you know that they have an amazing voices and they put it into good use in this track to highlight the seriousness of the disease.

As you listen to them, you can tell that they are pained by what is going on around the world and you get to connect with him on a personal level. The instrumentation of this track is dope because it allows the message to sink in.

Listen to Corona below and tell us what you think.

https://www.youtube.com/watch?v=GQ6kPJI8Upg

Maua Sama drops classic love ballad ‘Nioneshe’ (Video)

I’m a big fan of Tanzanian songstress Maua Sama so when I heard that she had released a new song, I was naturally excited and I hope that you will be too after listening to it.

Also read: Kenyan musicians have so much to learn from their Tanzanian counterparts

So, the jam is titled Nioneshe, which is Swahili for show me and it’s such a beautiful composition. If you’re into love ballads, I have a feeling that you will be listening to it on replay for a very long time.

Maua Sama

From my understanding, Maua Sama is not too sure whether a certain chap loves her. As such, she wants he wants him to show her that he really loves her through his actions.

I only started jamming to Bongo recently so when I tell you that this track is dope, you better believe me. You really should ladies and gentlemen.

For starters, Maua Sama has a lovely voice, the kind that most men, including myself, wouldn’t mind listening to all day. She really sounds like an angel, wait how do they even sound?

Maua Sama

She has a way of expressing herself in her songs that makes you feel like she is talking to you and then she is sincere in the way she sings.

To add to that there is a guy with a deep base on the background vocals and I feel their voices blend so well. Although my Swahili is not all that, I feel Nioneshe is lyrically on point.

The beat and instrumentation are not that bad either. If you’ve heard of the name Kimambo then I’m sure you know that he is probably the best beat maker in Tanzania.

The video is also really dope. One of the things I love most about it is it’s crisp quality. Of course, the location, props and scene transitioning were also impeccable. Kudos to Hanscana.

Watch Nioneshe below and tell us what you think.

Maua sama ajivunia mafanikio ya Iokote

Mwanadada Maua Sama ameonyesha kupata mafanikio makubwa kutokana na wimbo ulifanya vizuri sana mwaka 2018 uliojulikana kwa jina lka Iokote ambao ulivuma sana ndani na nje ya tanzania.

Maua sama ansema kuwa idadi kubwa ya mashabiki zake waliopenda wimbo huo walimfanya apate hata nguvu ya kupush wimbo huo kutokana na wao kuupokea vizuri.

Hata hivyo mwanadada huyo anazidi kuwapa moyo mashabiki zake kutokana na mafanikio hayo hasa baada ya kununu gari ya rav4 inayosemwa kuwa na thamani ya zaidi ya milion 20 na hata sasa kununua kwanja tayari kwa ujenzi.

Mwanadada huyo ambae amekuwa kimya asietaka kuonyesha nini anafanya, Amfanya vizuri sana kwa mwaka uliopita huku mashabiki wakisubiri ujio mpyta baada ya Iokote.

Mafanikio Ya ‘Iokote’ Yampelekea Maua Sama Kuporomosha Mjengo

Msanii wa muziki wa Bongo fleva ambaye mwaka jana alifanya vyema na wimbo wake wa ‘Iokote’ amefunguka na kusema nguvu ya mashabiki katika kumpa sapoti kumemsaidia kuweza kununua gari na sasa kujenga Nyumba.

Maua Sama ambaye siku si nyingi aliweka wazi gari aina ya Toyota Rav 4 ambalo alikiri kuwa alinunua kutokana na wimbo wake wa Iokote kufanya vyema Lakini sasa amesema ameweza kununua kiwanja kwa ajili ya kujenga Nyumba yake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Mchanganyiko, Maua Sama alisema kuwa kwa sasa ameanza ujenzi wa ‘bangaloo hatari’ maeneo ya Mbweni jijini Dar.

Mashabiki wangu ndiyo wamenipa mafanikio na kunifanya niweze kununua kitu ambacho nakitaka, hata hili gari limetoka kwao hakuna mtu mwingine zaidi ya mashabiki wangu na nipo mbioni kumalizia mjengo wangu kwa nguvu zao”.

 

Kamwe Sitakaa Niusahau Mwaka 2018- Maua Sama

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Maua Sama aliyefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Iokote’ amefunguka na kuweka wazi kuwa kamwe hatakaa asahau mwaka 2018.

Mwaka jana Maua Sama alijikuta katika wakati mgumu mara Baada ya kuwekwa mahabusu kwa muda wa siku 10 bila dhamana Baada ya kudaiwa kuidharau na kuichezea pesa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Maua Sama amesema kuwa anaukaribisha Mwaka Mpya wa 2019 vizuri, lakini hatausahau 2018 kwani alipitia Mengi na kujifunza mengi.

Namshukuru sana Mungu nimemaliza mwaka salama japokuwa nimekutana na changamoto kubwa ambayo sikuitarajia kuipata ile ya kuwekwa ndani kutokana na ngoma hiyo ya Iokote.

Lakini nashukuru soo liliisha salama na nilijifunza ninatakiwa kuheshimu kila kitu, kwa hiyo sitarajii kitokee kitu kama kile tena katika maisha yangu.

Kwa sasa ninajikita zaidi kwenye kazi ya sanaa kwa kuwa najua nimejaliwa kipaji na nitatoa kazi ambazo wapenzi wa Maua wanahitaji ili niweze kukonga nyoyo zao”.

 

Maua Sama Haogopi Nafasi ya Iokote Kutambulisha Wimbo Mpya.

Mwanadada Maua sama anasema kuwa katika maisha yake ya muziki kwa sasa pamoja na kwama wimbo wake wa Iokote ni wimbo ulifanya kazi vizuri sana kwa mwaka huu lakini bado anaona kuwa sio kitu yeye kuogopa kufanya wimbo mwingine akihofia nafasi ya ule uliopita.

Maua anasema kuwa hataki kusumbuliwa na presha ya  Iokote kwa sababu hata wakati anatoa wimbo huo hakuwa amefikiria kama utachukua nafasi kubwa kiasi hicho.

Maua Sama anasema ” Unajua wasanii wengine wamekuwa wakipotea kwa sababu ya kufanansiah nafasi ya wimbo waliotoa na ule uliopita, lakini kwangu ni tofauti kwa sababu tayari nimeshajianda kuja na muziki wangu ambao  ni kawaida kuwakonga nafsi za mashabiki.”

Maua anasema kuwa hakuna wimbo ambao aliona anaweza kukosea kama wimbo wa iokote kwa sababu haikuwa style yake ya muziki lakini ndio umefanya vizuri mpaka anashangaa.

Maua Sama Afuata Nyayo Za Rostam Kwa Hili

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini aliyofanya vyema na ngoma yake ya ‘Iokote’ Maua Sama amefunguka na kuweka wazi anaunga mkono msemo wa wakali wa Hip Hop Roma na Stamina (Rostam).

Roma na Stamina Wameunda msemo wao wa ‘Tunafunga Jumla jumla’ kwa ajili ya kuufungia mwaka 2018 kikazi zaidi kwa njia ya Sanaa ya muziki.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Mchanganyiko, Maua Sama anayetamba na Ngoma ya Iokote alisema kuwa, ametokea kuvutiwa na msemo huo baada ya kuusikia na kwamba anatamani kuja na wimbo wenye jina hilo.

Nimependa kwa kweli, kwa sababu msemo kama huu kutumika mwishoni mwa mwaka huwa mzuri, unaweza kuta mtu umefanya biashara zako sasa unafunga jumla jumla ili ufungue mwaka mwingine.

Nitajaribu kuongea na Rostam ikiwezekana nitatoka na wimbo wa tunafunga jumla jumla baada ya hii ya Iokote”.

Maua Sama licha tu ya kuvutiwa na msemo wa Roma na Stamina ‘Tunafunga jumla jumla’ na kutaka kufanya wimbo Lakini pia wasanii hao wametangaza kufanya baadhi ya shoo pamoja.

Rostam na Maua Sama Wawasanua Mashabiki Zao

Wasanii wa muziki wa Bongo fleva wanaounda kundi la Rostam Roma na Stamina pamoja Maua Sama Wake wateja Mashabiki zao Baada ya kuanzisha msemo wa Tunafunga Jumla jumla.

Katika kurasa zao kwenye mitandao ya kijamii, wawili hao wamekuwa wakiposti picha zao na wakati mwingine wa tukio fulani wa­kiambatanisha na maneno Tunafun­ga Jumla Jumla, jam­bo ambalo mashabiki wengi wamekuwa wak­ishindwa kung’amua maana yake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Jumamosi, Roma alisema neno hilo alianza kuliona kwa Stamina lakini anashangaa wengine wameanza kuliiga huku wengi wakiomba ufafanuzi.

Ukiniuliza maana yake sielewi ila ni misemo kama ilivyo misemo mingine. Mfano Mangi anaweza kufunga duka akasema nafunga jumla jumla, au mama n’tilie, muuza maji, karanga na wengine wengi kwa hiyo suala la biashara kuna kufunga jumla jumla”.

 

Maua Sama Afananishwa na Darasa

Mwanadada Maua Sama ambae kwa sasa amekuwa habari ya mjini kwa wimbo wake wa Iokote anafananishwa na Darasa baada ya wimbo wke huo ku-trend sana kila mahali na hata nje ya nchi huku watu wakipata wasiwasi kuwa isije kuwa kama alivyopotea darasa baada ya kutoa wimbo wa muziki na kisha kuwaancha mashabiki na kiu ya muziki wake.

Ikumbukwe kuwa Darasa alianza taratibu katika muziki na hata baadae kutoa wimbo ambao ulikuwa kama wimbo wa taifa na kupendwa na mashabii wote lakini baada ya muda mchache wimbo huo kufanya vizuri mashabiki walitegemea kuwa Darasa atatoa nyimbo nyingine nzuri kuliko hiyo lakii cha ajabu alikatisha mapenzi ya mashabiki baada ya kupotea abisa.

Ujumbe kwa Maua Sama ni kwamba mashabiki hawataki kuangushwa kama inavyotokea kwa wasanii wengine wenye mfano kama darasa, wanachotaka ni burudani na uwepo wako katika game.

 

Maua Sama Akana Kutumia Uchawi Kupata Mafanikio

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Iokote’ Maua Sama amefunguka na kuweka wazi kuwa hajawahi kutumia nguvu za giza ili kupata mafanikio katika kazi zake za kimuziki.

Maua ametoa siri ya mafanikio yake na kusema ni Mungu pekee ndiye amempa mafaniko katika kazi zake za kimuziki.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Maua alisema anachoamini siku zote kwenye maisha yake kuwa wakati wa Mungu ndio sahihi siku zote hivyo mpaka wimbo wake huo unatokea kupendwa hivyo ni kwamba amewapa mashabiki wake wanachotaka.

Unajua mtu mwingine anaweza kujua ni uchawi kumbe sio kabisa ni muda sasa wa Mungu ameamua kukurudisha kwa kasi kwa mashabiki wako na hicho ndio kitu muhimu sana”.

Maua amezidi kung’aa na wimbo wake huo ambao umekuwa ukihit sana na mpaka sasa unashukilia chati katika vituo mbali mbali vya redio an televisheni lakini pia kuwa na watazamaji mamilioni katika mtandao wa Youtube.

Maua Sama Afungukia Mafanikio Ya ‘Iokote’

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Maua Saleh maarufu kama Maua Sama amefunguka na kuongelea mafanikio ya wimbo wake wa ‘Iokote’ ambao unaendelea kufanya vyema.

Licha ya Maua kufanya nyimbo kadhaa nzuri huko nyuma lakini wimbo wake wa ‘Iokote’ ndio umekuwa kama umemtambulisha sana Kwenye ulimwengu wa Bongo fleva.

Katika mahojiano yake na Global Publishers , Maua aliyeimba wimbo huo kwa kushirikiana na ndugu wa marehemu Banza Stone, Hanstone alisema kuwa, katika maisha yake hajawahi kutegemea kama ataachia wimbo wa kumchanganya kiasi hicho ambapo tangu autoe umezidi kumpa shoo hadi anachanganyikiwa.

Yaani sijui hata nisemaje, Iokote imenifanyia maajabu makubwa sana hata nashindwa nielezeaje, kama huko nje ya nchi hadi sasa napata shoo hadi nachanganyikiwa nitajigawaje. Ukiingia mitaani, kwenye usafiri ndiyo nakuwa chizi kabisa”.

Licha ya mafanikio aliyopata Maua Sama Kupitia wimbo huo Lakini pia alipitia kipindi kigumu mara baada ya kuwekwa rumande kwa muda wa wiki nzima baada ya kukamatwa

Maua Sama Atembea Kifua Mbele kwa WCB.

Mwanadada Maua Sama ameonyesha juhudi zake mbele ya wasanii wengine baada ya wimbo wake wa iokote kufanya vizuri  katika mitandao na station mbalimbali za burudani.Maua ambae hivi karibuni amekuwa katika wakati mgumu kutokana na kuweka rumande kwa zaidi ya siku tano anaonyesha kufurahishwa na jambo hilo.

Wimbo wa Iokote ndio uliomfanya Maua  kuwekwa rumande kutokana na hisia za mashabiki katika wimbo huo na kushtakiwa kwa kosa la kudharirisha pesa ya Tanzania.

Hata hivyo tangu akiwa bado polisi rekodi ya wimbo huo kufanya vizuri ilikuwa ikionekana na  mpaka sasa wimbo huo unaonekana kuendelea kufanya vizuri  na kuwashinda wasanii wa WCB na nyimbo zao mpya ambazo nyingi zimetoka hivi karibuni.

“Nimepitia Kipindi Kigumu Sana” Maua Sama Afunguka Baada Ya Kuachiwa Huru

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema na kibao chake cha ‘Iokote’ Maua Sama amefunguka kwa mara ya kwanza tangu aachiwe huru kwa dhamana na jeshi la polisi.

Maua Sama na Mtangazaji wa Clouds Media Soudy Brown walitiwa mbaroni wiki iliyopita baada ya kuchapisha Kwenye mitandao ya kijamii maudhui ya watu wakicheza na kukanyaga pesa.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Maua Sama amefunguka na kueleza jinsi alivyopitia kipindi kigumu katika siku 10 ambazo alikuwa chini ya ulinzi:

Soudy Brown na Maua Sama Waachiwa Kwa Dhamana

Mtangazaji wa Clouds Fm Soudy Brown na Msanii wa Bongo fleva Maua Sama wameachiwa kwa dhamana na jeshi la polisi baada ya kukaa rumande kwa wiki moja.

Soudy Brown na Maua Sama walishikiliwa na jeshi la polisi baada ya kuhusishwa na video waliyoisambaza Kwenye mitandao ya kijamii iliyoonyesha watu wakichezea na Kukanyagawpes

Soudy Brown, Maua Sama na Meneja wake Fadhili Kondo waliachiwa jana Septemba 25, jioni lakini wote wanatakiwa kesho kuripoti kituo cha kati (Central Police Station) saa 4 asubuhi.

Watatu hao jana walirudishwa mahabusu baada ya kupata dhamana ya kesi ya kwanza ya kuweka maudhui mitandao bila kibali kutoka kwa mamlaka husika, lakini waliendelea kushikiliwa na jeshi la polisi kwa kile kilichodaiwa kuwa bado wanakosa lingine la kujibu, huku Mawakili wao wakizungumzia tukio la kukanyaga fedha ya Tanzania.

Wasanii ni Wanafiki Wanasubiri Kutoa Pole Badala Ya Kusaidia”- Steve Nyerere

Msanii wa Bongo movie na komedian maarufu Steve Nyerere amefunguka na kutaka Wasanii Wenzake waache unafiki na kupaaza sauti sasa ili Soudy Brown na Maua Sama waweze kuachwa huru.

Maua Sama na Soudy Brown wamewekwa  ndani tangu siku ya Ijumaa mpaka leo hawajapata dhamana baada ya kuposti video clip iliyowaonyesha kundi la watu wakicheza wimbo wa Iokote wa Maua Sama huku wakirusha pesa na kuzikanyaga.

Steve Nyerere amewatolea povu wasanii Wenzake na kuwataka wajitoe kuwasaidia wasanii wenzao katika kipindi hiki cha shida badala ya kukaa kimya halafu kuja kutoa pole wakija kutoka hapo baadae.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Steve Nyerere amemwaga povu hili:

Sisi wasanii ni waoga na wanafiki, limeanza kuhusishwa sijui kuna ugomvi na RC Makonda hawa wamekosea, sio wakitoka ndio tuanze kutoa pole, Ndio nilipanga kufanya hivi, Hapana muda ndio huu tuombe radhi kwa serikali vijana wetu wapewe dhamana”.

 

 

Vanessa Mdee Amfariji Maua Sama “Usijali Utatoka Tu”.

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee amefunguki ishu ya Msanii mwenzake Maua Sama kuwekwa Ndani kwa siku tano mfululizo bila ya dhamana.

Maua Sama anewekwa  ndani tangu siku ya Jumapili mpaka leo hajapata dhamana baada ya kuonekana kwenye video clips akiwa anakanyaga  pesa huku akicheza wimbo wake wa ‘Iokote’.

Vanessa ameibuka n kumtaka Maua kuwa mjasiri na kumtaka kuwa mvumilivu kwani siku si nyingi atatoka na akisha toka watacheka na kusahau yote yaliyotokea.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Vanessa Mdee kamuandikia ujumbe huu:

https://www.instagram.com/p/Bn8Tpg3CHhO/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=rtlm6iay8rzk

Wolper Awaombea Msamaha Soudy Brown na Maua Sama Wanaosota Rumande

Msanii wa filamu za Bongo Movie na mjasiriamali Mrembo Jacqueline Wolper ameibuka na kuwaombea msamaha mtangazaji wa Clouds Fm Soudy Brown na msanii wa Bongo fleva Maua Sama.

Maua na Soudy wamewekwa ndani tangu siku ya Jumapili mpaka leo hawajapata dhamana baada ya kuonekana kwenye video clips wakiwa wanakanyaga pesa.

Wolper amejikuta akiguswa na kitendo hicho cha kuwekwa ndani ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram, amesema anaomba viongozi wakubwa wa nchi wawaachie wasanii hao kwani walikuwa kwenye utafutaji na badala yake adhabu waliyoipata kwa siku hizi tatu liwe funzo kwa wengine.

 

Katika utafutaji Kuna mitihani Mingi Sana. Nachoweza kusema Nikuomba Tuu wakubwa muwasamehe vijana wenzetu Naamini katika Hili lililotokea Basi wengine wengi watajifunza kitu kupitia hili Naomba niwaombee masamaha wa Dhati kabisa Ndugu zetu Na wawe huru kuendelea Na majukumu yao inshallah. Maua & Soudy na wengine wore mliopo Ndani Juu ya hili sio sawa kutaja wote lakini hawa niwawakilishi poleni saanaa Jamani Ndani sio kuzuri“.

Mpaka sasa inadaiwa wawili hao bado wapo ndani bila dhamana.

Idris Sultan Amuombea Msamaha Maua Sama

Msanii wa Bongo movie na Comedian maarufu Idris Sultan ameibuka na kumuombea msamaha Msanii wa Bongo fleva Maua Sama baada ya kuwekwa rumande kwa siku tatu.

Siku chache zilizopita Maua Sama na mtangazaji wa Clouds FM, Soudy Brown walitiwa nguvuni na jeshi la polisi baada ya video iliyowaonyesha wakiwa wanakanyaga pesa kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

Baada ya kusambaa kwa video hiyo toka jumapili mpaka leo Soudy Brown na Maua bado hawajapata dhamana.

Idris Sultan ameibuka na kumuombea radhi Maua Sama na kuomba aachwe huru na Awe mfano wa kuigwa na jamii:

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Idris Sultan ameandika:

https://www.instagram.com/p/Bn6REJDhCPF/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1j9q2eztrp313

 

Soudy Brown na Maua Sama Watiwa Mbaroni

Mtangazaji wa kipindi cha Shilawadu cha Clouds Tv, Soudy Brown na msanii wa Bongo fleva anayefanya vyema na ngoma yake ya ‘Iokote’ wamekuwa mbaroni mapema jana.

Soudy Brown na Maua Sama wanadaiwa kukamatwa na Polisi Kinondoni lakini mpaka jana jioni tayari walikuwa wameshahamishiwa Central Polisi.

Bongo 5 wanaripoti kuwa wawili hao walishikwa siku ya jana baada ya kupost video mtandaoni inayowaonekana watu wakicheza wimbo ‘Iokote’ wa Maua Sama huku wakiwa wanakanyaga hela.

Kamanda wa polisi kanda maalumu Dar, Mambosasa amefunguka na kuweka wazi kuwa Polisi inamshikiria mtangazaji Soudy Brown na mwanamuziki Maua Sama  kwa kosa la uharibifu wa mali. Inadaiwa wameonekana mtandaoni wakirusha hela na kuzikanyaga jambo ambalo ni kinyume na sheria.

Maua Sama Afungukia Tetesi Za Kumwagwa na Mzungu

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Maua Sama Amefunguka na kuongelea tetesi zilizosambaa nwneye mitandao ya kijamii kuwa hivi Karibuni ametoswa na mpenzi wake.

Maua Sama ambaye alijizolea umaarufu miaka ya nyuma na ngoma yake ya Amen hivi sasa bado yupo Kwenye gemu na anatamba na ngoma yake ya Iokote ambayo inasikika kila kona.

Pamoja na kufanya vizuri katika muziki wake lakini inadaiwa Msanii huyo hafanyi vizuri sana Kwenye maisha yake binafsi hasa upande wa mapenzi kwani inasemekana Msanii huyo ana ametoswa na mpenzi

Maua ambaye alikuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na mzungu fulani inadaiwa kuwa amejikuta katika kipindi kigumu baada ya kumwagwa.

Kwenye Interview aliyofanya na Global Publishers Maua amekana tetesi hizo na kudai ni maneno ya watu kwani yeye hajaachwa na mtu yoyote:

Hakuna kitu kama hicho. Ujue Wabongo bwana wape picha tu ‘caption’ wataandika wenyewe! Yaani wamejaa kufuatilia mambo ya mtandao na kuyaamini. Kwa sasa nipo katika uhusiano na sipendi kuuweka hadharani“.

 

Solo Thang Akiri Kuzimika na Maua Sama

Msanii mkongwe wa Muziki wa Bongo fleva aliyetamba kwa miondoko yake ya kuchana miaka hiyo Msafiri Kondo maarufu kama Solo Thang amefunguka na kukiri kumkubali msanii mwenzake Maua Sama.

Solo Thang ambaye amekuwa kimya kwa miaka mingi baada ya kuhamia nchini Uongereza amekiri bado anafuatilia kwa ukaribu Bongo fleva na msanii wa kike anayemkuna ni Maua Sama.

Solo Thang

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Solo Thang amesema katika wasanii wa kike Maua ndio anajua muziki pia ni miongoni mwa wadada wa Bongo fleva wanaomkuna sana.

Kiukweli ninapenda anachokifanya Maua Sama, ni mwanamuziki mzuri, ingawa nipo nje namsikiliza sana na anasikilizwa sana pia, lakini mbali na yeye wanamuziki wengine kama Diamond, Ally Kiba, A.Y, Fid Q, kazi zao zinatufikia na tunapata nafasi ya kuzisikiliza“.

Maua Sama anafanya vizuri na wimbo wake unaoitwa Amen aliomshirikisha mkali wa RnB Ben Paul.

Maua Sama Atangaza Ndoa.

Huenda ikawa kweli mwanadada Maua Sama ameamua kufunga pingu za maisha na yule ampendae kutokana na caption zake nyingi katika ukurasa wake wa instagram akionyesha kuwa ana dalili za harusi hivi karibuni.

Lakini pia inawezekana ikawa ni kiki ya wimbo wake mpya kama wanavyojua kufanya wasanii wengi  pale wanapotaka kuachia ngoma mpya kwa kuamua kutengeneza attention kwa mashabiki wao ili ngoma iuze na waweze kufanya vizuri.

basi katika ukurasa wake wa instagram, maua ameweka zaidi ya mara mbili picha zeney caption ya kuashiria jambo fulani linakaribia.akiwa amevalia gauni ya harusi (shela) mau sama aliweka picha hiyo na kuandika “wahenga wanasema utamu wa ngoma ingia ndani mwenyewe ucheze,wacha na mimi nikachze yangu”

Na baada ya maneno hayo katika ukurasa wake wa instagram alianza kuweka picha zinazomuonyesha akiwa karibu na msani mwenie Ben pol na kuandika baadhi ya maneno yaliyoashiria ndoa.

 

Maua Sama Kufunga Ndoa Mwakani

Ndoa ni jambo la kheri sio kwa mwanamke tu, ila hata kwa wanaume, wasanii wengi wa Bongo wamekuwa hawadumu katika mahusiano na kuachana kila baada ya miezi michache,hii imefanya wasanii wengi washindwe kuingia katika ndoa , bado sababu haiko wazi lakini ni wasanii wachache wenye kukaa kwenye mahusiano kwa muda mrefu  na kufikia hatua ya  kufunga ndoa.

Mwanadada mrembo kabisa katika tasnia ya  muziki wa Bongo fleva nchini, Maua Sama ambae kwa sasa anafanya vizuri na kibao chake cha” Katukatu’ amefunguka na kusema kuwa ndoa yake na mwanaume aliyemchumbia hivi karibuni inaweza kufanyika hapo mwakani lakini kwa sasa bado kidogo mipango  ya harusi haijafanyika.Msanii huyo ambae miezi kadhaa hivi iliyopita alichumbiwa na mchumba wake mwenye asili ya kizungu anasema kuwa wanatarajia kufunga ndoa mwakani.

Maua Sama akiongea katika Over the Weekend ya gazeti la Ijumaa, alisema kuwa ana uhakika michongo yote ya harusi itaenda vizuri lakini kwa utaratibu wake na kazi zake kwa sasa  hana mpango wa kufunga ndoa  mwaka huu hadi mwakani.’Bado sana mipango ya ndoa kwa sasa mpaka mwakani.Sasa hivi ninaangalia zaidi muziki wangu,” aliongea Maua

Hata hivyo msanii Maua anasema kuwa anamshukuru sana Mungu maana ameweza kumsimamia na kuweka kukaa kwenye game muda mrefu huku nyimbo zake zikifanya vizuri ,lakini pia ameelezea sababu za msanii kukaa katika game la muziki  kwa muda mrefu ni vile ambavyo msanii anaamua kujiweka  “nashukuru nimeweza  kukaa kwa muda mrefu  bila kuchuja  na hii ni kutokana  na hii ni kutokana na msanii unavyojiweka” aliongezea Maua

Maua SaMa ambae pia ni zao zuri kutoka katika jumba la kulea wasanii wenye vipaji  nchini la THT , amekuwa mmoja wa wanadada wanaofanya vizuri kuanzia katika wimbo wake wa ‘Mahaba niue’ ambao ulikaa muda mrefu kwenye chati, lakini hata baada ya wimbo huo nyimbo zilizofuata ziliendela kufanya vizuri na kupokelewa vizuri na mashabiki wake, akiwa pia ni mmoja wa wasanii wanaozunguka mikoani katika tamsha la Fiesta , maua amekuwa akipokelewa vizuri katika jukwaa la Fiesta.

“Hamna bhana, mimi na Ema tunafanya tu kazi, mimi siko na Ema” Maua Sama

Kwa muda mrefu sasa, imekuwa inadaiwa Maua Sama amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na producer wake Ema the Boy.

Maua Sama alizungumzia jambo hili na Soudy Brown na kukana hili jambo. Alieleza uhusiano wao ulikuwa wa kazi tu na hamna jambo lingine kati yao.

”Hamna bhana, mimi na Ema tunafanya tu kazi, mimi siko na Ema na watu wanatangaza tu kwani mimi ni mtu wa kwanza kutangaziwa vitu vya namna hiyo..?” Alinena.

Ema pia alimuunga mkono na kusema hivi;

“Sijui chochote kuhusu hizo habari. Mara nyingi tunakuwa tunarecord hamna kitu cha zaidi ya hapo. Wewe unajua mambo ya muziki yanavyokuwa, muda mwingine mnaweza kutoka asubuhi ukamrudisha anapokaa au usiku mkaenda wote kutafuta chakula lakini hamna chochote ni muziki tu.”

Na ndio hiyo sasa.

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.