Actress Jacqueline Wolper and Husband Announce Divorce

Renowned Tanzanian actress Jacqueline Wolper has announced her separation from her husband, Rich Mitindo, revealing that she is in the process of finalizing their divorce.

The couple, who got engaged in 2021 and tied the knot in a high-profile wedding in 2022 attended by celebrities, politicians, and close family, are now parting ways. Wolper shared the news on her Instagram, addressing her followers with gratitude for their messages, prayers, and support.

CHECK OUT:

https://www.ghafla.co.ke/ke/hakuwa-ata-na-kitanda-tulilala-chini-wolper-shares-unknown-details-from-past-relationship-with-harmonize/

She expressed her appreciation, saying, “Mungu awabariki wote mnao nitakia mema, na hata wale wenye nia tofauti na njema pia mbarikiwe” (God bless all of you who wish me well, and even those with different intentions). She also reassured her fans about her well-being, stating, “Naomba niwatoe wasiwasi na mashaka juu ya furaha na amani ya moyo wangu” (I want to put to rest any worries or doubts about the peace and happiness in my heart).

Wolper confirmed her separation from Rich (Baba P) and clarified that while the marriage is over, they will maintain mutual respect as co-parents. She emphasized, “Tutabaki kuheshimiana kama wazazi na kulea watoto wetu” (We will continue to respect each other as parents and raise our children), while asserting, “Swala la mahusiano ya ndoa hilo halipo” (The issue of marriage is no longer there).

The actress also requested privacy regarding her estranged husband, asking not to be involved in matters concerning him as they no longer relate to her. She concluded with heartfelt thanks to her fans, saying, “Nawapenda sana nashukuru kwa msg zenu nyingi za kunitia moyo” (I love you all very much and thank you for your many encouraging messages). Wolper assured her followers that she is focusing on her peace and well-being moving forward.

ALSO CHECK OUT:

https://www.ghafla.co.ke/ke/aibu-harmonize-explains-his-entanglement-with-wolper-and-former-boss-diamond-platnumz/

Harmonize´s ex, Wolper sets terms for his wedding to Italian girlfriend, Sarah

Bongo fashion icon, Jacqueline Wolper who was previously bongo artist, Harmonize´s lover, speaks about her emotional well being if Harmonize proceeds with marriage.

Exclusively to Tanzanian local daily, Wolper cites that the chain of events at her ex´s wedding would really hurt her.

Harmonize and Italian fiancée, Sarah

Harmonize is set to marry his fiancée of Italian descent, Sarah.

The bongo movie actress reveals that she was initially set to wed Harmonize before their breakup and was not made aware of his engagement with Sarah.

Sijazipata habari za Harmonize kumvalisha pete ya uchumba Sara ila ikifanyika ndoa huenda nikapata presha.

Singer, Harmonize and ex, Jacqueline Wolper

Wolper shares that it will definitely put pressure on her, if the marriage between the two is to kick off.

However, it all depends on how the event goes down:

Itatagemea ndoa hiyo itafungwa vipi na yatafanyika mambo gani kama ni ya kuniumiza au ya kawaida kawaida.

This she expresses during the launch of an entertainment spot in Masaki, Dar es Salaam.

Sarah´s proposal

Roughly a month ago, just April, the WCB artist went down on one knee for Sarah while in Rome, Italy, with her family.

https://www.instagram.com/p/Bw0LZsggGcC/

The news was shared across media platforms, an event that only family and close friends witnessed.

The duo was more than excited as pretty Sarah said ¨YES¨ to her then 25-year old King.

Wolper & Harmonize

Soon after the world set foot into 2017, Wolper took to social media to publicly call off her relationship with lover, Harmonize.

Bongo fashion icon and actress, Jacqueline Wolper

Further on, she trashed all videos and snaps the two ever took together.

This soon after saw Harmonize bag himself his current Italian model, Sarah.

Wolper Afunguka Kuwaingilia Harmonize na Sarah Tena

Mbunifu wa Mavazi na Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper ameibuka na kujibu Tuhuma Za kuingilia tena mahusiano ya aliyekuwa Mpenzi Wake Harmonize na Mpenzi Wake Mpya Sarah.

Sakata hilo lilijitokeza siku chache zilizopita baada ya Wolper alionekana kuuimba katika akaunti yake ya instagram wa mapensi mabaya akimaanisha ‘mapenzi mabaya’ na yeye kubadilisha na kuimba kinyume.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Wolper alisema kuwa amejisikia tu kuimba kinyume kuwa mapensi mazuri.

Lakini watu wanazungumza vingine kwamba namchokoza lakini isivyo hivyo. Nimejisikia tu kuimba haijalishi yeye ndiye ameanza kuimba lakini mimi nikaona niimbe kinyume na yeye alivyoimba ni vile nimejisikia tu kufanya hivyo”.

Baada ya video ile kusambaa watu wengi walichukulia kuwa Wolper amefanya vile ili kumsanifu Sarah hasa kwa sababu wawili hao hawaivi kabisa.

 

Wolper Afanya Maamuzi Magumu Ya Kuuza Gari Lake

Mbunifu wa mavazi na Muigizaji wa Bongo movie  Jacqueline Massawe maarufu kama Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa Hivi karibuni alifikia uamuzi wa kuuza gari lake.

Wolper ambaye alikuwa anamiliki gari aina ya Toyota Brevis, ameweka wazi kuwa ameamua kuuza gari lake hilo ambalo lilikuwa ndio Usafiri wake pekee ili anunue matirio za kutengenezea magauni.

Katika mahojiano aliyofanya na Mtandao wa Global Publishers, Wolper ameweka wazi kuwa aliamua kuchukua uamuzi wake huo baada ya kupendezwa na matirio hayo alipokuwa nchini Dubai hivi karibuni.

Unajua mimi ni fundi cherehani hivyo  nilivyofika nchini Dubai na kuwaona wadada wakipendeza kwa kuvaa magauni kama haya na nilipowaangalia niliona kabisa kuwa nayamudu kuyadizaini.

Nilichoamua kufanya ni kuuza gari yangu na kwenda kununua matirio haya na kutengeneza magauni kadhaa ambayo kama hili na mengine nayauza. Kwa sasa natumia usafiri wa kukodi na hilo kwangu sioni shida”.

 

Wolper Alizwa na Vifo Vya Watoto Njombe

Mastaa mbali mbali wamejitokeza kukemea vitendo vya mauaji dhidi ya Watoto ambayo yanaendelea mkoani Njombe Hivi sasa.

Kwa Wiki karibuni chache sasa kumekuwa na mauaji makubwa ambayo yanafanyika katika vijiji vya mkoa wa Njombe ambapo Watoto wamekuwa wakiuliwa kikatili kwa kuchinjwa.

Msanii wa Bongo movie Jacqueline Wolper amekuwa mstari wa mbele kukemea vitendo hivyo ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika maneno haya:

Jesus eti Nini kina endelea sijaelewa ? Hii ni Tanzania Then why ?‍♀️How? Coment This kwa wanaojua Na poleni Wote“.

Lakini pia Haji Manara amekemea pia kitendo gaucho ambapo ameandika:

Tupaze sauti zetu wote kukemea dhulma hii!! Watoto wanayo haki ya kuishi,haki ya kusoma na wanayo haki ya kucheza na kufurahi! Why wauawawe ? Ndugu zangu hili ni jukumu letu sote kuwalinda watoto wetu,kulilinda Taifa letu la baadae,tusikubali udhalimu huu,na tuseme NO!! Inaumiza sana kuona yupo Mtanzania anafanya ukatili huu kisa ni imani potofu za kishirikina!!
Khofu ya Mungu ipo wapi? Ohhh Watoto wetu nn kosa lao? Au kuzaliwa watanzania? ! Mwenyezi Mungu kwako tunakukabidhi wauaji hawa waliolaanika
.”

 

Wolper Adaiwa Kumkuwadia Dogo Janja Kwa Demu Mpya

Muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper ameibuka na kukana kabisa taarifa zinazodai kuwa amemsaliti rafiki yake Irene Uwoya kwa kumkuwadia shoga yake kwa Dogo Janja.

Dogo Janja ana ‘kifaa’ kingine kipya ambaye ni mtoto mkali, mkazi wa jijini Arusha aliyetajwa kwa jina moja la Linna. Baada ya kusambaa kwa video na picha za Dogo Janja ambaye ni msanii wa Bongo Fleva na Linna wakiwa kwenye mahaba mazito ndipo baadhi ya watu wakaibuka na kila mmoja kuanza kusema lake.

Dogo Janja na Mpenzi Wake Linah

Gazeti la Ijumaa linaripoti kuwa kwa sasa uhusiano wa Uwoya na Wolper hauko sawa. Kufuatia bango hilo kuwa na madai mazito ya Uwoya kupaniki huku Wolper akitajwatajwa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wolper alifunguka na kusema haya:

Kikubwa ninafurahi kwa sababu baada ya kupelekewa hiyo ishu, Irene (Uwoya) hakutaka kuamini kwani ananijua jinsi ninavyompenda na kumchukulia. Anajua siwezi kuwa snichi kwake kwani ninamchukulia kama ndugu yangu. “So hata alivyoambiwa alikuwa ndiye mtu wa kwanza kukataa mimi kufanya hivyo.

Anajua mimi siwezi unafiki ndiyo maana hujawahi kuona nikimposti Dogo Janja (kwenye ukurasa wake wa Instagram) na huyo demu ambaye ni mdogo wangu (Linna) maana nitakuwa mchawi. Yaani mchawi kabisa.

Na mimi ninamlaumu Dogo Janja maana Dogo Janja hajui undugu wangu na Linna kwa hiyo ninahisi alitumia uanaume wake kuni-block (mtandaoni). “Mpaka hapa ninakuambia huyo mdogo wangu, Linna siyo mteja wangu tena na hana tena ukaribu na mimi tangu awe na Dogo Janja.

Sasa nikisema Dogo Janja mchawi nitakuwa mwongo? Mchawi ni mtu mharibifu. “Nilishangaa sana kusikia eti mimi ndiye nimemkuwadia wakati Dogo Janja nilikuwa ninamchukulia kama mwanangu na alikuwa shemeji yangu (kwa Uwoya). “Hiyo skendo ndiyo imenifanya niwakalie kimya Linna na Dogo Janja maana Dogo Janja alikuwa rafiki yangu kabla hata ya kuwa na Irene (Uwoya) na huyo aliyenaye ambaye ni mdogo wangu kabisa.

Kinachoniuma sana ni huo uvumi ulivyotokea maana nilimuuliza huyo mdogo wangu (Linna) na Dogo Janja wakakataa katakata na meseji zao ninazo alafu eti leo hii ninaonekana…. (tusi) wakati Irene (Uwoya) ni rafiki yangu na ni mfanyakazi mwenzangu“.

 

 

Jacqueline Wolper- Natamani Kupata Mtoto

Staa katika tasnia ya Bongo movie na mbunifu wa mavazi Jacqueline Wolper ameibuka na kusema katika vitu anatamani mwaka huu ni kupata mtoto  wake  wa kwanza.

Wolper ambaye amethibitisha kuwa kwenye mahusiano na mwanaume ambaye amesisitiza kuwa  hataweza kumuweka hadharani Lakini amesema huu mwaka anatamani kupata mtoto bila kujali kama itakuwa ndani ya ndoa au nje.

 

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la DIMBA Jumatano, Wolper alisema anaamini mwaka huu kwake utakuwa na neema kubwa, ikiwemo kujaaliwa mtoto kama ambavyo amekuwa akitamani iwe hivyo.

Nina mipango mingi sana kwa mwaka huu, unajua kila unapoweka mikakati yako mwanzoni mwa mwaka ndio nafasi nzuri ya kufanya mambo yako kwa umakini zaidi, kwa sasa ninachowaza ni mtoto”.

Wolper ambaye amewahi kuwa muwazi sana kwenye Suala la mahusiano katika siku za nyuma amesema hawezi kufanya hivyo kwa sasa kwani Mitandao ndio iliyoua mahusiano hapo nyuma.

‘I’m on a righteous path now’ Wolper forced to explain why she invited her ex Harmonize and his girlfriend to birthday party

Actress Jacqueline Wolper recently surprised many after inviting her ex Harmonize and his new girlfriend Sarah to her birthday.

The three haven’t been seeing eye-to-eye and the whole industries knows that they don’t like each other so much because of their histories.

Wolper, however, shared that she’s trying to put all this behind a reason why she invited them to his birthday party. In the party, Harmonize was seen in a video singing to the birthday girl while his fiancée presented Wolper with loads of cash.

“(I invited Harmonize and his girlfriend Sarah to my birthday) due to my faith and the people who surround me that know God. So they have set me on a righteous path. Right now even if you poked me in the eye I wouldn’t fight with you because I don’t want to create more enemies. If anyone wants to be my enemy I push them away. Right now I don’t what to make any enemies,” she told Radio & TV Personality Sam Misago during an interview.

Harmonize and Wolper had an ugly, public breakup that was marred with a lot of drama. After he moved to Sarah, the two ladies confronted each other on social media several times while fighting for the singer.

Wolper Akumbwa na Fedheha Ya Aina Yake Mwanza

Muigizaji wa Bongo movie na Mbunifu wa mavazi Jacqueline Wolper amejikuta akipata fedheha ya aina yake Baada ya kula mweleka wa nguvu mbele za watu.

Gazeti la Ijumaa Wikienda linaripoti kuwa mbwembwe zilizmponza Wolper kwenye ukumbi uliopo katika Ufukwe wa Jembe ni Jembe jijini Mwanza ambapo Lebo ya WCB  chini ya Nasibu Abdul ‘Diamond Platinum’ au ‘Mondi’ ilikuwa ikifanya pati ya awali (pre-party) ya onesho lao la Wasafi Festival lililofanyika katika Uwanja wa CCM-Kirumba, juzi.

Katika tukio hilo, wakati watu wakipata kilaji, mastaa ambao walitarajiwa kufanya makamuzi kesho yake kwenye Wasafi Festival walikuwa wakitambulishwa. Ulipofika wakati wa Wolper, yeye aliamua kupanda juu ya meza kama wafanyavyo wanenguaji wa staili ya kusasambua. Akiwa juu ya meza, DJ aliweka Wimbo wa Kwangwaru ambapo Wolper aliendelea kuonesha umahiri wa kukicheza kwa kukata mauno baab’kubwa. Kwa bahati mbaya, wakati akiendelea kufanya yake, maskini mwanadada huyo mrembo alipiga mwereka matata na kuangukia kisogoni.

Hata hivyo, alisaidiwa kunyanyuka na mabaunsa na mashabiki waliokuwa karibu ambao walimuinua kisha wakamkagua na kubaini hakupata maumivu makali hivyo shoo yake ikaishia hapo. Baada ya kushuhudia tukio hilo, baadhi ya mashabiki walisikika wakisema, eti huenda mambo yaliyompata Mondi kule Sumbawanga yalitaka kujirudia kupitia kwa Wolper.

Source- Ijumaa Wikienda

“Siwezi Kurudiana na Mkongo Tena”- Wolper

Muigizaji wa Bongo movie na Mbunifu wa mavazi Jacqueline Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa hawezi tena kurudiana na aliyekuwa Mpenzi Wake anayejulikana Kama Putin maarufu kama Mkongo.

Tetesi za Wolper kurudiana na aliyekuwa mchumba Wake zilisambaa Wiki iliyopita Kupitia mitandao ya kijamii Baada ya Wolper kumposti katika ukurasa Wake wa Instagram.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa, Wolper alisema kuna watu wamekuwa wakivumisha kwamba amerudisha mapenzi kwa Mkongo huyo kwa sababu tu wanapostiana picha kwenye Mtandao wa Kijamii wa Instagram, lakini hiyo siyo sababu ya kurudisha penzi lao la nyuma bali wanafanya hivyo kimazoea tu.

Watu wanaonijua vizuri wanafahamu, siwezi kurudia matapishi yangu hata siku moja. Huyo Putin tumekuwa kama washikaji tuliozoeana, lakini hakuna mapenzi tena na hatuwezi kuwa wapenzi tena”.

Wolper na Putin walikuwa kwenye mahusiano kwa muda mwaka mmoja ambapo walifikia hatua ya kuvalishana pete ya uchumba, lakini waliachana baada ya mwanaume huyo kugundulika kuwa ana mwanamke mwingine nchini kwao.

Lynn Afungukia Mapenzi Yake Kwa Jacqueline Wolper

Video Vixen na msanii wa Bongo fleva Irene Louis maarufu kama Lynn amefunguka na kuweka wazi kuwa anamkubali sana mwanadada mkali wa fasheni Jacqueline Wolper.

Lynn alifunguka hayo Baada ya kuulizwa sababu iliyomfanya Mpaka awe namfuatilia Msanii mmoja tu Bongo kupitia ukurasa wake wa Instagram na sio wasanii wengine.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha habari nchini, Lynn ameweka wazi kuwa sababu ya kwanza ni kuwa anamkubali sana Wolper na pili ndio mtu ambaye kibongo bongo anaendana naye:

Mimi naona toka tujuane tunakuwa tupo sawa tu kishikaji tunaongea, kwa hiyo yeye kama kuna kitu tumefanana ndio maana tumekuwa hivyo. Nahisi damu zetu zimeendana, labda wengine watakuja”.

Siku chache zilizopita  Jacqueline Wolper alifabya bonge la party kwa ajili ya kusherehekea miaka kadhaa ya kuzaliwa kwake, Mwanadada huyo ( Lynn) ni miongoni watu waliojumuika.

Jacqueline Wolper Ashabikia Mapenzi Ya Harmonize na Sarah

Muigizaji wa Bongo movie na mbunifu wa mavazi Jacqueline Wolper ameshangaza wengi Baada ya kuonekana akiwa anashabikia Penzi la hasimu Wake Sarah na Harmonize.

Wiki iliyopita kuna tetesi zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Harmonize na Wolper wamerudiana Baada ya kuonekana wakiwa karibu katika tamasha zima la Wasafi Festival.

Lakini Harmonize na mpenzi Wake Sarah walionekana kuzima tetesi hizo Baada ya kuposti video iliyowaonyesha wawili hao wakiwa wanacheza pamoja na kukumbatiana kwenye nyumba yao.

Siku ya jana ilikuwa ni siku ye kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Wolper ambaye alifanya party yake kubwa na kualika wasanii wakubwa lakini cha kushangaza aliwaalika Harmonize na Sarah pia.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Wolper aliposti video ya Harmonize na Wolper na kuisindikiza na maneno haya:

https://www.instagram.com/p/BrDmRCCnUsh/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=ijbkt2241p33

Katika kuonyesha kuwa Harmonize na yeye Hana tatizo na Wolper alimposti katika ukurasa wake wa Instagram na kumtakia Birthday njema.

Wolper Ajitapa Kuwekewa Ulinzi Mzito na Mpenzi Wake

Msanii wa Bongo movie na mbunifu wa mavazi Jacqueline Wolper amefunguka na kudai kuwa hivi sasa amewekewa ulinzi mkali na Mpenzi Wake kwa sababu ya usalama wake binafsi.

Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa ulinzi mkubwa ambao amewekewa unatokana na Tamasha la Wasafi Festival ambalo anaendelea kushiriki hivyo kila mkoa amewekewa Bodyguard kwa kila mkoa ambao ataenda.

Kwenye mahojiano aliyofanya na mtandao wa  Dizzim Online Wolper amesema kuwa Mpenzi wake huyo sio mtu wa camera hivyo hawezi kuonekana .

Actually Mr wangu kila mkoa ameniwekea Body Guard na dereva kwahiyo ulimuona Body guard wangu , lakini sio mtu wa camera kwahiyo hawezi kuonekana.

Unajua mikoa tuna wapenzi wengi mtu anaweza akakuhug kama vile kwa Diamond wakachukua cheni, kwahiyo hiyo ndio sababu kubwa kwahiyo sio kwamba unakuja na Body guard kwasababu gani nafikiri hiyo ndio sababu kuu, tunawapenda mashabiki zetu hatutaki kuwakosea“.

Jacqueline ni mmoja kati ya wasanii ambao wameonekana kushiriki katika matamasha yote ya Wasafi Festival katika mikoa mbali mbali.

 

 

Harmonize publicly announce reunion with Jacqueline Wolper

Harmonize and Jacqueline Wolper are back together after close to two years apart, the two dated sometimes in 2016 before they broke up in the beginning of 2017.

Wolper dumped Harmonize after he cheated on her with Italian beauty Sarah Michelotti. Harmonize and Sarah got in a relationship after Wolper dumped him.

Now Harmonize and Wolper have gotten back together. The two reignited their love when they met at the inaugural Wasafi Festival in Mtwara on November 23rd, they hugged passionately in public for close to a minute.

https://www.instagram.com/p/BqhuCTKAfwn/?utm_source=ig_embed

Sarah rushed to social media to assert that she was still together with Harmonize following the public display of affection in Mtwara.

Also read: Sarah sets record straight about her relationship with Harmonize after the incident with Wolper at Wasafi Festival

We’re back together

Harmonize himself has since announced that he has reunited with Wolper after they were once again spotted together at Wasafi Festival in Iringa on November 3oth 2018.

The ‘Kwangwaru’ hit maker set the record straight while speaking during an interview with Ijumaa Wikienda at Samora stadium in Iringa at the sideline of Wasafi Festival.

“Naomba niseme wazi hapa hadharani kuwa nimerudi kwa Wolper wangu,” said Harmonize.

 

 

Sarah sets record straight about her relationship with Harmonize after the incident with Wolper at Wasafi Festival

The inaugural Wasafi Festival was not without drama, Diamond Platnumz was mugged of his pure diamond chains worth Kes 1.8 million while Harmonize ‘reunited’ with his ex Jacqueline Wolper.

Wolper and Harmonize met at a hotel in Mtwara and at first she was openly ignoring him, but Harmonize walked to where she was seated and hanged her by force.

https://www.instagram.com/p/BqhuCTKAfwn/

Sarah reacts

The incident in Mtwara made many people believe that Harmonize had broken up with his Italian sweetheart Sarah Michelotti and that he was perhaps reuniting with Wolper.

But Sarah took to social media to set the record straight that Harmonize and her were still tight. She posted a photo of Harmonize and captioned it;

“A lot of people ask me if we are still together … this is my answer …. YES ..?? see you soon bab @harmonize_tz #Nangwanda ?”

https://www.instagram.com/p/BqiLbhgnVIE/

She also shared more posts showing how they were still in love, she was referring herself as ‘Konde girl’ (Harmonize is also refers himself as Konde Boy).

https://www.instagram.com/p/Bqiq_GrnnZw/

 

“Sarah Hajakasirika Nilivyokumbatiwa na Wolper”- Harmonize

Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutokea katika label ya WCB Harmonize ameibuka na kudai kwamba Mpenzi Wake Sarah hajamind kitendo cha yeye kukumbatiana na Ex Wake Wolper.

Wikiend iliyopita mkoani Mtwara kwenye tamasha la Wasafi Festival Harmonize alirekodiwa akikumbatiana na Ex Wake Wolper wakati wa kusalimiana mara moja tetesi zilianza kusambaa kwamba wawili hao wamerudiana.

Tetesi hizo zilizimwa na Mpenzi wa Harmonize, Sarah ambaye Kupitia ukurasa wake wa Instagram alisema yeye na Harmonize hawajaachana na hawategemei kuachana na muda si mrefu angejiunga naye Mtwara kwa ajili ya shoo hiyo.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Harmonize alisisitiza yeye na Wolper ni washkaji tu na wapo kikazi ila Mpenzi Wake ni Sarah na hajamind alivyoona video za wawili hao kukumbatiana:

Wolper ni mtu wangu wa karibu na nilifurahi  kumuona akishiriki tena na Wasafi na kuhusu Sarah najua hawezi kumaindi kwani anaelewa kuwa tupo Mtwara kikazi zaidi”.

Fashion Ya Gauni Yampa Wakati Mgumu Wolper

Muigizaji wa Bongo movie na mbunifu wa mitindo Jacqueline Wolper alijikuta katika wakati mgumu baada ya Gauni alilovaa katika shughuli hivi karibuni kumletea kero.

Global Publishers wanaripoti kuwa tukio lilitokea Wikiend iliyopita katika ukumbi wa Club Next Door Arena, Dar ambapo Wolper alivalia gauni lililomwacha wazi sehemu kubwa ya kifua hivyo kila alipokuwa akiendelea na burudani alikuwa akikosa raha kutokana na sehemu ya matiti kutoka nje kwani kila alipoweka sawa baada ya muda hali ilijirudia ileile.

Baada ya sakata hilo kuendelea kwa muda mrefu Mwanahabari alimuuliza sababu ya kubuni fasheni hiyo ya gauni iliyoonekana kumnyima raha lakini alishindwa kutoa jibu lolote na kusema ana haraka hivyo aachwe akapumzike.

Wolper ambaye anasifika kwa kubuni na kushona mavazi yake anayovaa mwenyewe na hata kuuza katika boutique yake ya Wolper house of stylish, amedaiwa kukosea safari hii.

 

Lord Eyes Afungukia Skendo Ya Mapenzi na Wolper

Msanii mkongwe wa muziki wa hop hop nchini kupokea katika kinda la Weusi Lord Eyes amefungukia tetesi zinazotrend kuwa Ana mahusiano na staa wa Bongo movie Jacqueline Wolper.

Kwa muda mfupi sasa kumekuwa na tetesi kuwa Lord Eyes na Wolper wamekuwa kwenye mahusiano hi ilitokana na picha kadhaa zilizowaonyesha wasanii hao pamoja.

Wiki iliyopita kwenye mahojiano yake na Global Publishers, Wolper alikataa tetesi hizo Lakini pia aliweka hao tatizo Kama ikitokea hivyo:

Unajua hata mimi ambaye naambiwa natoka naye nimeona kwenye mitandao tu lakini pia siku ikitokea, freshi tu.Sio mwanaume mbaya maana ana sifa zote za mwanaume ninayempenda au wamesema hivyo kwa sababu niliimba wimbo wake nikauposti mtandaoni ndio tatizo basi ngoja tuone itakavyokuwa maana Wabongo wape picha tu maneno wataweka wenyewe”.

Lakini pia Lord Eyes amefungukia tetesi hizo kwenye mahojiano na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv na kusema habari hizo hazina Ukweli wowote:

Wolper ni radioing yangu tu na unajua maana ya rafiki ni mtu anayeweza kukusitiri na ndoto unamuita rafiki wa kweli”.

 

Wolper- Sioni Tatizo Kutoka na Lord Eyes

Mbunifu wa mavazi na muigizaji wa Bongo movie Jacqueline Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa hana uhusiano na msanii mkongwe wa muziki wa Hip hop nchini Waziri Makuto maarufu kama Lord Eyes.

Kumekuwa na tetesi zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wolper na Lord Eyes wapo kwenye mahusiano ya kimapenzi lakini Wolper amefungukia madai hayo na kusema kuwa hayana ukweli wowote.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Wolper  alisema yeye ameona kwenye mitandao taarifa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na Lord lakini pia hata siku ikitokea ikawa hivyo sio mbaya kwani sio mwanaume mbaya kwake na pia anavutiwa na jinsi alivyo.

Unajua hata mimi ambaye naambiwa natoka naye nimeona kwenye mitandao tu lakini pia siku ikitokea, freshi tu.Sio mwanaume mbaya maana ana sifa zote za mwanaume ninayempenda au wamesema hivyo kwa sababu niliimba wimbo wake nikauposti mtandaoni ndio tatizo basi ngoja tuone itakavyokuwa maana Wabongo wape picha tu maneno wataweka mwenyewe.” 

 

 

Mbasha Apangua Tetesi Za Kupombeka na Wolper

Msanii wa nyimbo za injili nchini Emmanuel Mbasha ameibuka na kupanguia tetesi zote zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii ya kwamba mtumishi huyo wa Mungu alikuwa amekaa na msanii wa Bongo movie Jacqueline Wolper wakinywa pombe.

Kwenye interview aliyofanya na kituo kimoja habari, Mbasha amekanusha tetesi hizo na kudai kuwa alikuwa anakunywa soda. Mbasha amesema watu wamemjia juu kwa kukaa karibu na Wolper na kusema akiendelea kukaa karibu na  Wolper atampoteza na pengine anaweza akafanya mambo ambayo hayaendani na wokovu wake kama watu walivyomzoea kwamba yeye ni mtu wa dini.

Mimi na Wolper ni marafiki wa karibu na ukweli ni kwamba mimi nampenda Wolper kama dada yangu na namkubali kwa kazi zake anazozifanya hata hivyo naamini kwamba na yeye ananipenda kwa kuwa tumekuwa karibu kwa muda mrefu sasa”.

Lakini pia Mbasha alimalizia huku akitolea maelezo picha ambazo zimesambaa mitandano zikimuonyesha akiwa karibu na Wolper na kusema kwamba picha hizo zilitokana na kazi ambayo waliipata kwa pamoja ikawakutanisha na kuwaweka karibu.

 

 

Jacqueline Wolper Ahaidi Kupambana na Marafiki Wanafki

Msanii wa filamu za Bongo Movie na mwanamitindo maarufu Jacqueline Wolper ametoa neno kwa marafiki wote ambao wamekuwa na tabia za kinafki na kuhaidi kupambana nao.

Wolper amefunguka na kudai siku akimkamata mtu ambaye wanafahamiana vizuri akiwa anamsema kwenye Mtandao wa Instagram atafurahia shoo kwa atakachomfanya.

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers, Wolper kama mtu mnajuana na ukaona amekosea ni vyema ukamfuata mwenyewe na kumwambia kuliko kuandika unavyotaka Instagram kwani huo ni unafiki.

Siamini kabisa mtu mwenye mapenzi ya dhati na wewe anaweza kukuandikia ujumbe kwenye Instagram. Mimi huo ninauita unafiki na siku nikimkamata mtu wa aina hiyo atanijua“.

Siku chache zilizopita Wolper aliingia kwenye mgogoro na msanii mwenzake Esha Buheti baada ya kuamua kumsema Wema Kupitia Kwenye ukurasa wake wa Instagram jambo ambalo Wolper alidai hajapenda na kumtaka Esha amfuate pembeni na kumsema Wema badala ya kumsema Instagram.

Harmonize Amwagia Povu Zito Wolper Baada Ya Tetesi Za Kurudiana

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Harmonize amejikuta anamtolea povu zito aliyekuwa mpenzi wake Staa wa Bongo movie Jacqueline Wolper baada ya kusambaa kwa taarifa za Kurudiana.

Siku chache zilizopita kuna taarifa zilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wolper na Harmonize wamerudiana baada ya Wolper kuposti jina la Harmonize.

Sakata hili lilianza baada ya Wolper kuposti picha kadhaa alizoziambatanisha na Jina la Raj ambalo lilikuwa ni Jina alilomuita Harmonize kipindi cha Mahusiano jambo lililoibua tetesi za wawili hao Kurudiana.

Lakini kabla ya Tetesi hizo kusambaa vizuri Harmonize alimjia juu Wolper baada ya kuulizwa na mashabiki zake kama kweli amemtosa Mzungu wake Sarah na kuamua kuwa na Wolper ambapo alijibu:

Anajitekenya mwenyewe na kucheka mwenyewe bila hata haya wakati tuma msiba wa ndugu yetu, na mwingine katekwa yeye analeta pombe zake hapa”.

Tangu Harmonize man wolper walipoachana wamekuwa maadui wakubwa huku mara kwa mara wakirushiana vijembe Kupitia social media na mara ya mwisho Harmonize alianika Orishas ya wanaume wote ambao Wolper alibanjuka nao.

Wolper- Wanaume Wengi Wanatumia Wasanii Wa Kike Kwa Kiki

Muigizaji wa Bongo Movie na Mwanamitindo maarufu Jacqueline Wolper ameibuka na kudai ni ngumu kwa Mastaa wengi wa kike kupata wanaume wenye mapenzi ya dhati kwani wengi wao wanataka kuwa nao kwa ajili ya umaarufu.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Amani, Wolper alisema kuwa mara ny­ingi wanaume wamewachuku­lia wasanii kama daraja la kusonga mbele au kukuza majina yao lakini siyo mapenzi ya dhati.

Ni hivi mas­taa wengi hasa kwenye tasnia ya uigizaji wameamua kufanya maisha yao wenyewe na kusahau kabisa kama kuna jambo la kuolewa na ndiyo maana unaweza kukaa hata miaka mitano bila kusikia msanii wa kike ameolewa”.

Wolper amekuwa na Mahusiano na wanaume kadhaa ambao kiukweli aliwapa umaarufu wakati wa Mahusiano yao kati yao ni pamoja na staa wa Bongo fleva Harmonize ambaye alijizolea umaarufu sana alipokuwa na Wolper na muziki wake kukua.

Wolper Awaombea Msamaha Soudy Brown na Maua Sama Wanaosota Rumande

Msanii wa filamu za Bongo Movie na mjasiriamali Mrembo Jacqueline Wolper ameibuka na kuwaombea msamaha mtangazaji wa Clouds Fm Soudy Brown na msanii wa Bongo fleva Maua Sama.

Maua na Soudy wamewekwa ndani tangu siku ya Jumapili mpaka leo hawajapata dhamana baada ya kuonekana kwenye video clips wakiwa wanakanyaga pesa.

Wolper amejikuta akiguswa na kitendo hicho cha kuwekwa ndani ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram, amesema anaomba viongozi wakubwa wa nchi wawaachie wasanii hao kwani walikuwa kwenye utafutaji na badala yake adhabu waliyoipata kwa siku hizi tatu liwe funzo kwa wengine.

 

Katika utafutaji Kuna mitihani Mingi Sana. Nachoweza kusema Nikuomba Tuu wakubwa muwasamehe vijana wenzetu Naamini katika Hili lililotokea Basi wengine wengi watajifunza kitu kupitia hili Naomba niwaombee masamaha wa Dhati kabisa Ndugu zetu Na wawe huru kuendelea Na majukumu yao inshallah. Maua & Soudy na wengine wore mliopo Ndani Juu ya hili sio sawa kutaja wote lakini hawa niwawakilishi poleni saanaa Jamani Ndani sio kuzuri“.

Mpaka sasa inadaiwa wawili hao bado wapo ndani bila dhamana.

Wolper Amwaga Povu Zito Kisa Muna

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo maarufu Jacqueline Wolper amejikuta akiporomosha mvua ya matusi pale alipoulizwa kuhusu sakata la Muna.

Muna ametawala vichwa vya habari kwa wiki kadhaa kufuatia skendo yake ya kumtelekeza mtoto wake wa kwanza anayeitwa Brian na majibizano a familia yake Kwenye vyombo vya habari.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Jacqueline Wolper amewajia juu watu wanaoingilia ugomvi wa familia za watu wanaowaona Kwenye mitandao ya kijamii.

Watu wa Instagram ni washenzi na hawajielewi, tena ni wapuuzi na wapumbavu. Kazi kufuatilia maisha ya watu tu, kwa nini wasimuache Muna mambo yake na familia yake, kila mtu abebe msalaba wake”.

 

Nina Ndoto Ya Kumvalisha Rihanna Kwenye Video Zake-Wolper

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo Jacqueline Wolper ambaye amekuwa akishona nguo zake kama fundi cherehani amefunguka na kudai anataka kumvisha staa wa kimataifa Rihanna.

Wolper amevaa cha watu midomo wazi baada ya kusema Yupo katika harakati za kumtafuta Mwanamuziki wa kimataifa kutoka Marekani Rihanna ili aweze kumshonea nguo ili aweze kuvaa.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Waandishi wa habari katika red carpet ya event ya Jibebe Challenge Wolper alifunguka:

 Kwa sasa bado naendelea kusoma nikimaliza nadhani nitaendelea na preocess za kumtafuta Rihanna kwa ajili ya kumvalisha na shukurani kwa mitandao ya kijamii ambayo imenipa wepesi wa kumtafuta Rihanna”.

Wolper ameswashangaa wanaodai haitawezekana kwake yeye kuwavalisha mastaa wakubwa kama Rihanna na kusema kila kitu kinawezekana ni kuweka juhudi Kwenye kazi.

Jacqueline Wolper targets Kobi Kihara and other Instagram slay queens with hard-hitting message

Bongo movie star-cum-fashionista Jacqueline Wolper Massawe has turned the heat on Instagram slay queens in the wake of Kobi Kihara scandal.

On August 24th 2018 Kobi Kihara was exposed for living a fake lifestyle. The former NTV anchor was lifting photos from other sites to fool her fans on social media that she was living large in US where she relocated to.

Kenyans on Twitter (KOT) went HAM on Kobi Kihara using #KobiKiharaChallenge to poke fun at the former NTV presenter. She quit social media altogether.

Also read: Deleting stolen photos wasn’t enough! Kobi Kihara ultimately quits social media

Fake lifestyle

 

Jacqueline Wolper took a dig at slay queens faking life on social media during an interview with Ijumaa Wikienda. She stressed that whatever she posts on social media portrays her real life.

“Hakuna kitu ninakichukia kama maisha ya kuigiza kwenye mitandao ya kijamii, ninayachukia kwa sababu ipo siku mtu atakuja kuona maisha yangu halisi ashangae. Hivyo inapaswa kila mmoja kuishi vile Mungu amempangia na siyo kuigiza, hayo maisha feki tuyatupe kule,” said Wolper.

 

 

 

 

Wolper Awashukia Wasanii Wanaoishi Maisha Feki

Muigizaji wa Bongo movie na mwanamitindo Jacqueline Wolper amewatolea povu mastaa ambao wamekuwa wakidanganya maisha yao kwa kuweka vitu feki Kwenye mitandao ya kijamii.

Wolper amefunguka na kudai huu ndio mwaka wa mastaa hao kutupilia mbali maisha feki feki wanayoishi na kuanza maisha yao ya kihalisia waachane na yale ya mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Ijumaa Wikienda, Wolper alisema wengi wanajipotosha wenyewe kwa kudanganya maisha waliyonayo, jambo ambalo siyo sawa kwa sababu wanapaswa kubuni vitu vingi vya maendeleo kuliko kujionesha kwenye mitandao kuwa maisha yao ni bomba kumbe hakuna chochote

Hakuna kitu ninakichukia kama maisha ya kuigiza kwenye mitandao ya kijamii, ninayachukia kwa sababu ipo siku mtu atakuja kuona maisha yangu halisi ashangae hivyo inapaswa kila mmoja kuishi vile Mungu amempangia na siyo kuigiza, hayo maisha feki tuyatupe kule”.

 

Wolper- Mapenzi na Ali Kiba Yalikuwa Bora Zaidi

Staa wa filamu za Bongo Movie na mjasiriamali Jacqueline Wolper ameibuka na kudai hakuna mwanaume ambaye alikuwa mpenzi bora kwake kama ilivyokuwa kwa staa wa Bongo fleva Ali Kiba.

Wolper ambaye siku za nyuma amewahi kukiri kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi kwa muda mrefu na Ali Kiba ingawa hawakuyaweka hadharani na kujulikana na mashabiki.

Kwenye mahojiano aliyiwahi kufanya na East Africa Television, Wolper amefunguka na kuongea haya:

Katika Mahusiano yangu yote ambayo nimewahi kuwa nayo, ambayo naweza kuyapa namba moja na yalikuwa mazuri na ni the best ni yale nilipokuwa na Ali Kiba. Lakini sio kwamba namiss hapana ila tu ninasema yalikuwa Mahusiano bora niliyowahi kuwa nayo”.

Mbali na Ali Kiba, Wolper ameshawahi kuwa Kwenye Mahusiano na mastaa wengine kama Harmonize, Juma Jux na wengineo.

Jacqueline Wolper: Harmonize still loves me and wants me, I try my best to avoid him

Jacqueline Wolper has revealed that she always snubs her ex boyfriends even when they meet at a public place. She sensationally claimed all of her exes including Harmonize were still in love with her.

“Ujue mimi kila nikiachana na mwanaume anakuwa bado ananipenda, pale nilikimbia kwa sababu nikiachana na boyfriend, huwa sipendi niendelee kuwasiliana naye wala kusogeleana naye, sipendi kusalimiana na ex,” said Wolper during an interview with journalists.

Wolper and Harmonize dated for a long time before they broke up and the latter went on to date an Italian woman called Sarah Michelotti.

Fell for an ex

Wolper reveals that she avoids her exes because she once fell for an ex boyfriend and ended up messing. She says that she will go see a pastor to pray for her because she still has the urge in her to reconnect with some of her exes.

“Ilishawahi kutokea ex ananihitaji kwa ajili ya mambo ya kibiashara lakini kwa sababu nakuwa sihitaji kabisa kuwasiliana nao nili-crash halafu nikakosa dili, hilo ni pepo ambalo ninalo nadhani nitamwambia mchungaji aniombee,” said Wolper.

Watch the full interview below:

Wolper-Wanaume Wote Nilioachana Nao Bado Wananipenda

Msanii wa filamu za Bongo Movie na mjasiriamali Diva Jacqueline Wolper ameibukana kudai kuwa katika Mahusiano yake yote ambayo amewahi kuwa nayo wanaume anaoachana nao bado wanakuwa wanampenda.

Wolper amefunguka kuwa katika maisha yake yote anapokuwa anaachana na wanaume aliokuwa nao Kwenye Mahusiano wote wanakuwa bado wanamuhitaji licha ya yeye kuwatema na kutowahitaji tena.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Wolper ambaye ameshawahi kuwa Kwenye Mahusiano na mastaa kadhaa Bongo ikiwemo staa wa Bongo fleva Harmonize amefunguka:

Ujue mimi kila nikiachana na mwanaume anakuwa bado ananipenda, pale nilikimbia kwa sababu nikiachana na boyfriend, huwa sipendi niendelee kuwasiliana naye wala kusogeleana naye, sipendi kusalimiana na X.

Ilishawahi kutokea X ananihitaji kwa ajili ya mambo ya kibiashara lakini kwa sababu nakuwa sihitaji kabisa kuwasiliana nao nili-crash halafu nikakosa dili, hilo ni pepo ambalo ninalo nadhani nitamwambia mchungaji aniombee”.

Lakini pia alizungumzia sakata la kutemwa kama jaji wa shindano la Miss Lake Zone na amedai kuwa waandaji wa shindano hilo walitumia jina lake kutafutia kiki baada ya Shindano lao kubuma.

Jacqueline Wolper splashes Kes 300,000 to buy album of musician featured in King Kaka’s song ‘Radhi’

Jacqueline Wolper has showed her appreciation to Bongo singer Barnaba Classic by buying his new album for a whopping $3000 or Kes 301,701.

For starters, Barnaba Classic is a fast rising Bongo star, King Kaka featured him in his song ‘Radhi’ which was released in March 2018.

Barnaba Classic has released a new album dubbed ‘Gold’. The singer launched the album on Thursday night August 30th 2018 and Jacqueline Wolper was among the first people to buy the album.

Kind gesture

Asked why she splashed Kes 300,000 to buy Barnaba’s new album, Jacqueline Wolper stated that it was a kind gesture to appreciate the support Barnaba gave her while she was still struggling.

“Kabla ya mimi kuwa boss lady (Barnaba) alikuwa ankuja na kukesha katika sho zangu bure, kwahio kwangu mimi ni mtu muhimu sana hata kununua album hiyo kwa dola 3000 ni kumsapoti mtu muhimu sana kwangu,” said Jacqueline Wolper.

 

 

 

Wolper Atangaza Kuokoka na Kumrudia Mungu

Msanii maarufu wa Bongo movie na mfanyabiashara Jacqueline Wolper amefunguka na kudai ameamua kumrudia Mungu na kuokoka ili aweze kuishi maisha ya wokovu.

Wolper amedai kuwa hivi sasa amemrudia Yesu na kumtumikia kiukweli kweli na kusema anampenda sana Yesu.

Kwenye mahojiano na Global Publishers , Wolper alisema ameamua kuokoka kwa sababu anatambua mbali na maisha ya duniani kuna maisha ya mbinguni, kwa hiyo ni vyema akaandaa maisha hayo pia na siyo kujisahau kana kwamba hataondoka duniani.

Kiukweli kwa sasa nimeamua kuokoka na kumrudia Mungu, nina uhakika kwa kufanya kwangu hivi niko kwenye mikono salama na mambo yangu yataninyookea zaidi kuhusu uvaaji wangu siyo tatizo kwa sababu siku hizi tunaokoka kisasa”.

Lakini pia Kwenye Interview hiyo Wolper aneweka wazi sababu iliyomfanya ahamishe makazi yake kutoka Tanzania kwenda nchi ya jirani ya Kenya ni masomo kwani kwa sasa anasomea masuala ya ngozi na urembo.

The price of lateness! Jacqueline Wolper blocked from judging Miss Tanzania pageant

Jacqueline Wolper was selected among judges to preside over 2018 Miss Tanzania beauty pageant, but unfortunately her name was dropped from the list.

There were a lot of speculations why Wolper was blocked from judging the forthcoming beauty pageant will be held on September 8th 2018.

Event organizer The Look has since offered an explanation why Wolper’s name was dropped from the list. Director General Basila Mwanukazi revealed that Wolper has herself to blame for missing the golden opportunity.

Jacqueline Wolper
Jacqueline Wolper
Lateness

Speaking to the press, Basila revealed that Jacqueline Wolper was late to a seminar where judges were being taken through how they would preside over the Miss Tanzania pageant.

“Majaji wanapewa semina, Wolper alichelewa kufika katika semina hivyo… ataingiaje katika majaji wakati hajaongozwa? Sio kuwa super star basi uje kujaji, hapana kuna miongozo maarumu ambayo alitakiwa kupata endapoa agehudhuria kama wale majaji wengine walivyopewa , lakini yeye kafika semeina ieshaisha,” said Basila Mwanukazi.

 

 

 

 

Wolper Atamani Mahusiano Ya Kimapenzi na Raisi

Msanii wa filamu za Bongo Movie na mfanyabiashara Jacqueline Wolper amefunguka na kudai anatamani sana kama angetoa Penzi lake kwa Raisi.

Wolper amedai anaona ni bora kama atakuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi kwa sasa statute Penzi pa Raisi yoyote Afrika kwani atakuwa salama zaidi kuliko kufaidi Penzi na wadananda wengine.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Wolper alisema mara nyingi amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na wanaume ambao mwishoni wanamsaliti jambo ambalo halipendi na linamkera, lakini anaamini akimpa moyo wake wa upendo Rais yeyote Afrika anaona atakuwa salama.

Unajua ndoto yangu mimi ningependa kutoa penzi langu kwa Rais maana najua kabisa, kwanza atakuwa ananiheshimu na itakuwa ni ngumu sana kunitenda kama wafanyavyo wengine na hapo nitatulia kabisa wala sitakumbuka wanaume wazugaji“.

Wolper amekuwa muwazi kuhusu maumivu anayokutana nayo Kwenye  mapenzi yake ambapo uhusiano wake na staa wa Bongo fleva Harmonize uliisha baada ya kumuacha na Harmonize kuanza Mahusiano na sarah ambaye ana kipato kikubwa.

Jacqueline Wolper: Sina Tatizo na Zari

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali maarufu Jacqueline Wolper amefunguka na kuweka wazi kuwa hana bifu na mzazi mwenza wa Diamond Platnumz Zari The Bosslady.

Wolper amefunguka hayo siku chache baada ya Zari kuingia kwenye bifu zito baada ya kuwaambia wasanii hao wasikanyage kwake maana watachafua na wasanii kadhaa wa Bongo movie ambao ni Wema,Aunty Ezekiel, Faiza Ally, Shamsa Ford na wengineo.

Wasanii hao ambao wamerushiana maneno na Zari Mtandaoni wameweka wazi kuwa hawawezi kwenda Tena Kwenye Birthday ya Tiffah huko nchini South Africa kutokana na maneno ya Zari.

Jacqueline Wolper yeye alidai kuwa hana tatizo na Zari kabisa, wanaheshimiana iwapo atakuwa amerejea kutoka shule ambapo anasoma kwa sasa, atakwenda tu.

Shule ndio inaweza kunizuia lakini nikiwa nimerejea nitakwenda tu kwani sina tatizo na Zari“.

 

Wolper Adai Hataki Penzi La Mwanaume Ambaye Sio Mtanzania

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali maarufu Jacqueline Wolper amefunguka na kudai hawezi kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na mwanaume ambaye sio Mtanzania.

Wolper ameweka wazi kuwa hawezi Tena kuwa Kwenye Mahusiano na mwanaume ambaye sio Mtanzania kwani alishajifunza siku za nyuma hivyo hawezi kurudia tena.

Kwenye mahojiano na gazeti la Amani, Wolper alisema kama ni kumpata mpenzi ambaye anaamini atamfaa basi lazima atoke ndani ya nchi yake japokuwa kuna watu walianza minong’ono kuwa alipokuwa nchini Kenya hivi karibuni, alikuwa na mpenzi raia wa nchi hiyo.

Sifikirii kabisa kutoa penzi langu kwa mwanaume ambaye siyo raia wa nchi yangu kwa sasa kwa sababu huko nyuma nilipitia huko lakini sasa sihitaji tena kama nimeamua kupendana na mwanaume basi atakuwa ni wa nchi yangu tu”.

Wolper ambaye kwa sasa aneweka makao nchini Kenya ameshawahi kuwa Kwenye na raia wa Kongo.

Jacqueline Wolper no longer interested in dating Kenyan men

About a week ago, Jacqueline Wolper revealed she was yearning for an exotic man, she specifically said she wanted to get pregnant for a Kenyan man.

Wolper expressed her love for Kenya on an Instagram post where she shared a photo of president Uhuru Kenyatta and First Lady Margaret Kenyatta and captioned it ‘Mr president #my second home Kenya’.

She opened up about her desire to date a Kenyan man on the comment section where she said she will get pregnant for the next Kenyan man she dates.

Also read: “Nkipata mwanaume kutoka Kenya ni mimba tu” Hormonize’s ex Jacqueline Wolper expresses desire to date Kenyan man

Only Tanzanian men
Jacqueline Wolper
Jacqueline Wolper

In an interview with Amani newspaper, Wolper stressed that she was no longer interested in dating exotic men. Wolper, who has previously dated a Congolese man, said that she doesn’t want to fall in love with any man who is not Tanzanian.

“Sifikirii kabisa kutoa penzi langu kwa mwanaume ambaye siyo raia wa nchi yangu kwa sasa kwa sababu huko nyuma nilipitia huko lakini sasa sihitaji tena kama nimeamua kupendana na mwanaume basi atakuwa ni wa nchi yangu tu,” said Wolper.

 

 

 

Wolper Amkingia Kifua Steve Nyerere Kwenye Suala la Rambirambi

Msanii wa filamu za Bongo Movie Jacqueline Wolper ameibuka na kumkingia kifua msanii mwenzake Steve Nyerere na kumtaka asivunjike moyo kusaidia wengine.

Steve Nyerere amekuwa Kwenye headlines za mitandao ya kijamii kwa muda sasa huku skendo ambayo imekuwa ikimuandama ni ya kila pesa za rambi rambi anazokusanya Kwenye misiba ya watu.

Na ishu hii imerudi  kwa kasi Tena mara baada ya Steve Nyerere kuonekana akiwa mstari wa mbele siku ya leo kwa ajili ya kuandaa msiba wa msanii Mzee Majuto.

Wolper ameibuka na kumkingia Steve na kumpa moyo kwa kazi nzuri anayofanya ya kuwasaidia watu ambao ni wafiwa na kumtaka ayapuuze maneno ambayo yamekuwa yakisemwa juu yake:

https://www.instagram.com/p/BmPJJuDlj1d/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=gh0ae9yptkq7

“Nkipata mwanaume kutoka Kenya ni mimba tu” Hormonize’s ex Jacqueline Wolper expresses desire to date Kenyan man

Jacqueline Wolper is in search of a sweetheart from Kenya. The Tanzanian actress considers Kenya her second home and as such wants to date a man from the 254.

Wolper expressed her love for Kenya on an Instagram post where she shared a photo of president Uhuru Kenyatta and First Lady Margaret Kenyatta and captioned it ‘Mr president #my second home Kenya’.

She opened up about her desire to date a Kenyan man on the comment section where she said she will get pregnant for the next Kenyan man she dates.

 

Fashion house

Wolper revealed plans to open House of Stylish in Nairobi to cater for her Kenyan customers when she last visited the country in May this year. She said  she was motivated to open the Kenyan store because customers have been struggling to reach her in Tanzania.

Jacqueline Wolper reaches out to Vera Sidika to offer her apology 

Tanzanian fashionista Jacqueline Wolper was among high profile guests that Vera Sidika invited to the launch of her beauty parlor a week ago.

The white and gold themed event was was graced by Vera’s friends and celebrities including Anita Nderu, Bonfire CEO Simon Kabu, Martin Kimathi. Of course Vera’s boyfriend Otile Brown didn’t miss.

Wolper however failed to show up at the launch which was held at Western Heights in Westlands, Nairobi. The Bongo actress has since reached out to Vera to explain everything.

I’ll come for my nail

Wolper says she knows she disappointed Vera when she failed to show up but promises to make it up to her. In a written apology on social media, Wolper tells Vera that she will personally explain to her why she missed the launch, she however promises to get her nails done at her parlor.

“Hongera sana my bby gal The boss lady herself, sasa stopata Tabu Tena kenya Mambo yote ya Urembo ?Classic from my baby Queen Vee?kesho mapema I will come for my Nails darling..
Najua ulinuna kidogo sikuja lkn unalijua Tatizo ??
I love u so Much, Acha Tupambane so that we Make That money baby.. Once again congratulations my love ??
I am proud of u.
@queenveebosset ????,” wrote Wolper.

 

Jacqueline Wolper Akiri Kuteswa Na Mapenzi

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Jacqueline Wolper amefunguka na kutaja vitu ambavyo vinamtesa akiwa kwenye mahusiano ya kimapenzi.

Katika Interview yake na Wasafi Tv, Wolper ameweka wazi kuwa vitu viwili ambavyo ni  muda na uongo ni vitu vinavyomtesa akiwa Kwenye Mahusiano ya kimapenzi.

Kitu kinachonitesa na kunipa stress kwenye kwenye mahusiano ni uongo na muda. Nafanya sana kazi lakini nahitaji sana muda wa kuwa na mtu wangu, kwa hiyo uongo na muda ni tatizo sana kwenye mahusiano.

Mtu akiaanza kunidanganya au kunipa muda mchache wa kuwa naye na kuwa out of mood kabisa na ninaweza nikaamka nikamwambia it’s over bila kujali chochote”.

Lakini pia Wolper amesema uongo pekee ana kukubali Kwenye Mahusiano ni uongo mzuri:

Uongo ninaouhitaji mimi ni ule kunidanganya kuwa unanipenda, tangu nizaliwe sijawahi kuona mwanamke mzuri kama wewe, huo ndio uongo unahitajika kwa kila mwanamke”.

 

Jacqueline Wolper sets the record straight on her alleged romantic relationship with Mr. Nice 

Jacqueline Wolper has come out to address claims she is dating onetime Bongo superstar Mr Nice. The Bongo actress is currently single, she dated at least two men after her breakup with Harmonize.

Rumors about Wolper and Mr Nice dating started when the two were seen hanging out together at a club in Nairobi sometimes in May this year.

https://www.instagram.com/p/BjIxk2Oguea/?

Working on a project

Wolper dismissed the dating rumors while speaking to Risasi Mchanganyiko. She explained that Mr Nice and her are only working together in an upcoming project.

“Watu wajue sisi tupo kikazi zaidi kwani kuonekana na mtu ni lazima awe mpenzi wako? Si lazima, huyu ni kaka yangu na bosi wetu ni mmoja, projekti yetu ikiwa tayari tutaitangaza itajulikana tu lakini kwa sasa bado ni mapema kuitangaza,” said Jacqueline Wolper.

 

 

 

Ghafla!
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.